Monday 8 July 2013

KAGASHEKI CUP: KITENDAGURO 1 vs NYANGA 0


Benchi la timu ya Kitendag
Benchi la timu ya Nyanga

Patashika kwenye goli la Kitendaguro

Bao la kujifunga dakikia ya 52 kipindi cha pili limepeleka kilio kwa timu ya Nyanga la mchezaji namba 12 alilojifunga kwa kupiga mpira upande wa pili. na kufanya mpira uishe timu yake ikiwa patupu pila kuziona nyavu za timu ya Kitendaguro. Licha ya timu ya Kitendaguro kuongoza bao hilo kipindi cha pili wameshindwa kutema cheche zao baada ya kukusa kosa mabao kadhaa.

Watazamaji pia leo waliingia kwa wingi kucheki mtanange wa leo hii

wadau wa soka wakifatilia mtanange wa leo hii.

Watazamaji

Mchezaji wa Nyanga akitembea na mpira kuelekea upande wa goli la Kitendaguro


wadau wa soka wakielekeza macho yao yote mawili kwenye kipute Kaitaba

Patashika hapa Mchezaji wa Kitendaguro na Nyanga akigombea mpira
Watangazaji wa radio Kasibante Fm 88.5 nao walikuwepo kutazama mtanange unaodhaminiwa na Mh.Kagasheki.
kagasheki cup ....2013 hakuna kulala kilometa 0!!
Wadau
Watazamaji wakitazama mtanange leo hii kwenye uwanja wa Kaitaba leo hii

Mtanange umeisha timu ya Kitendaguro ikiwa na ushindi wa bao 1-0

Waamuzi wa soka la leo hii wakitoka uwanjani baada ya mpira kuisha timu ya Kitendaguro ikiwa imeibuka kidedea kwa kushinda bao 1-0 bao walilojifunga wao wenyewe kipindi cha pili dakika ya 52 kupitia mchezaji wao Jackson Paul.

Kesho ni Kibeta na Kagondo saa 8:00 Mchana ikifuatiwa na mtanange mkali wa Nshambya na Bilele.
Kumbuka ndugu Mtazamaji na mpenzi wa mtandao huu wa jamcobk.blogspot.com KAGASHEKI CUP ni Mjumuiko wa kata zote 14 za Bukoba na Zimegawanywa kwenye makundi mawili "A" na "B" huku kundi A ikiwa na Timu 7 na Kundi B ikiwa na Timu 7.

KUNDI "A"  ni Rwamishenye, Buhembe, Bilele, Nshambya, Kibeta, Kagondo na Miembeni.

KUNDI "B" ni Kitendaguro, Nyanga, Kashai, Hamugembe, Ijuganyondo, Bakoba na Kahororo.

No comments:

Post a Comment