Wednesday 27 June 2018

MAWAKALA WA NMB KAGERA WAKUTANA ,WAPIGWA MSASA NA KUELEZA CHANGAMOTO ZAO.

Katika mkakati maalumu wa kuhakikisha NMB Benki inatoa huduma bora na kwa haraka kwa wateja wengi zaidi maeneo mbalimbali Nchini, Mawakala Mkoa wa Kagera wamekutana na uongozi  wa kanda ya ziwa na uongozi wa Tawi la Bukoba na kukaa pamoja na kuzungumza kwa pamoja mambo mbalimbali na changamoto zinazojitokeza katika kutoa huduma ya pesa kwa wananchi mbalimbali katika maeneo yao , Mjumuiko wa Mawakala umefanyika katika ukumbi wa St Thereza Bukoba Manispaa.(katika picha kulia mwenye Tai ni  Meneja Wakala NMB Kanda ya ziwa, wafanyakazi wa NMB Bukoba na Mawakala  kutoka maeneo tofauti.)
Tumia huduma za NMB, Ni salama na za uhakika.

MKURUGENZI WA VIWANJA VYA NDEGE NCHINI ATOA ZAWADI ZA VYAKULA KITUO CHA WAZEE KILIMA BUKOBA.

 Mkurugenzi wa viwanja vya ndege Nchini ametoa zawadi ya vyakula katika kituo cha wazee wasiojiweza lilichopo Mkoa wa Kagera Wilaya ya Bukoba, kituo hicho cha Kilima wanaishi wazee wasiojiweza wenye mahitaji mbalimbali, Akikabidhi vyakula hivyo kwa niaba ya Mkurugenzi wa viwanja vya ndege Nchini Bi   Dorice Uhagile Meneja wa uwanja wa ndege wa Bukoba ametoa wito kwa mashirika, Taasisi na watu binafsi kusaidia vituo mbalimbali kwani serikali haiwezi peke yake, ni vizuri kuguswa na kuwa na moyo wa kusaidia kwani kila mmoja wetu ni mzee mtarajiwa.Pia Meneja alipata wasaa kabla ya Eid Liftri kupata futari ya pamoja na wafanyakazi wa Uwanja wa ndege Bukoba na wadau mbalimbali, kwa niaba ya Mkuregenzi wa viwanja vya ndege Nchini.(katika picha Meneja wa Uwanja wa ndege Bukoba Bi  Dorice  Uhagile akikabidhi zawadi kwa wazee.)
 Vyakula mbalimbali.
 Baadhi ya Wazee wanaoishi kituo cha Kilima.
 Wa pili kushoto, Meneja wa uwanja wa ndege Bukoba Bi Dorice akiwa katika kituo cha Kilima.
 Picha ya pamoja ya wazee kituo cha Kilima.
 Wada mbalimbali wakipata futari ya pamoja kipindi cha mwezi mtukufu waRamadhani.

 Picha ya pamoja na wadau mbalimbali baada ya kufuturu.
Kwa habari za uhakika tembelea Jamcoblog.

NMB BUKOBA YAWAJENGA WATOTO KISAIKOLOGIA,KUJIWEKEA AKIBA BENKI.

 Katika kusherekea siku ya Baba duniani, Benki ya NMB  imeandaa hafla maalumu iliyokutanisha watoto wa shule za awali mpaka Darasa la saba, Hafla hiyo ilifanyika katika tawi la Bukoba. Mbali na mambo mengine watoto hao walipata fursa ya kutembelea maeneo mbalimbali ya benki na kufundishwa namna shughuli za kibenki zinavyofanyika,Watoto walipata zawadi mbalimbali kwa ajili ya matumizi ya masomo yao shuleni, walijengwa kisaikologia kutambua umuhimu wa kufungua akaunti na namna ya kuweka akiba kwa ajili ya karo na matumizi yao,Pia walishiriki viburudisho mbalimbali na kukata keki kuashiria na kutambua siku ya Baba duniani.(KATIKA PICHA AFISA WA NMB AKIKATA KEKI NA WATOTO)


Watoto wakiulizwa maswali na Afisa wa benki baada ya  kufundishwa shughuli za benki.
 Watoto wakionyeshwa maeneo mbalimbali ya Benki, hapo eneo la ulinzi na usalama.
 Watoto wakionyeshwa eneo la huduma ya ATM.
 Watoto wakionyeshwa eneo la kupanga mstari wakati wa kuweka na kutoa pesa.
 Watoto wakipata viburudisho.
 Zawadi mbalimbali walizopewa watoto.
 Watoto wakiwa na zawadi zao.
 Wakati wa keki.
Mjenge mwanao mapema ili atambue umuhimu wa kuweka akiba benki, na hasa benki ya NMB.