Wednesday 8 November 2017

RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI AWATAKA KAGERA SUGAR KUONGEZA UZALISHAJI WA SUKARI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ametembelea kiwanda cha sukari, Kagera sugar na kujionea  shughuli mbalimbali zinazofanyika kiwandani hapo, Rais Magufuli alitembelea mashamba ya miwa na  kujionea hatua  za uandaaji mashamba, kupanda mpaka kufikia hatua ya kuvuna miwa, Pia alitembelea kiwanda  na kujionea shughuli za uzalishaji sukari, Mh Rais Magufuli alipata wasaa  kuongea na wafanyakazi na amewataka kufanya kazi kwa bidii na kuutaka uongozi wajitahidi kuongeza uzalishaji ili waweze kuzalisha sukari kwa asilimia 75 kufikia mwaka ujao ,tofauti na sasa wanazalisha kati ya asilimia 60-63 kwa mwaka.
 Maeneo ya kiwanda.
 Katikati Mh  Waziri wa kilimo Charles Tizeba akizungumza na viongozi wa Kagera sugar.
 Wafanyakazi wa kagera sugar.
 Bw Rwakabamba na mkewe, mmoja mwa mawaziri nchini Rwanda.


RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI ZZINDUA BARABARA YA KYAKA BUGENE.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt John Pombe Magufuli amezindua barabara ya Kyaka Bugene yenye urefu wa km 59.1 yenye kiwango cha lami.Rais Magufuli amesema wakati akiwa waziri wa wizara ya ujenzi  katika serikali ya awamu ya nne ulianza ujenzi wa barabara hii na leo akiwa rais anaizindua,amewataka wananchi kuilinda na kutumia  fursa ya barabara hii katika uzalishaji mbalimbali na kuwaletea maendeleo.Hafla ya uzinduzi ilifanyika katika mji wa Kayanga Karagwe na kuudhuliwa na mawaziri, makatibu wakuu, wabunge, viongozi wa chama tawala  na vyama vya kisiasa,na wananchi.
Mzee Mavunde Mc wa shughuli nzima.