Wednesday 8 November 2017

RAIS DKT JOHN POMBE MAGUFULI AWATAKA KAGERA SUGAR KUONGEZA UZALISHAJI WA SUKARI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ametembelea kiwanda cha sukari, Kagera sugar na kujionea  shughuli mbalimbali zinazofanyika kiwandani hapo, Rais Magufuli alitembelea mashamba ya miwa na  kujionea hatua  za uandaaji mashamba, kupanda mpaka kufikia hatua ya kuvuna miwa, Pia alitembelea kiwanda  na kujionea shughuli za uzalishaji sukari, Mh Rais Magufuli alipata wasaa  kuongea na wafanyakazi na amewataka kufanya kazi kwa bidii na kuutaka uongozi wajitahidi kuongeza uzalishaji ili waweze kuzalisha sukari kwa asilimia 75 kufikia mwaka ujao ,tofauti na sasa wanazalisha kati ya asilimia 60-63 kwa mwaka.
 Maeneo ya kiwanda.
 Katikati Mh  Waziri wa kilimo Charles Tizeba akizungumza na viongozi wa Kagera sugar.
 Wafanyakazi wa kagera sugar.
 Bw Rwakabamba na mkewe, mmoja mwa mawaziri nchini Rwanda.


No comments:

Post a Comment