Wednesday 12 July 2017

Waziri Prof. Mbarawa akagua mradi wa barabara za juu TAZARA jijini Dar es salaam


Na Joachim Mushi wa TBN
WAZIRI wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa leo ametembelea mradi wa ujenzi wa barabara za juu unaoendelea eneo la Tazara jijini Dar es Salaam na kuridhishwa na kasi ya ujenzi inayoendelea chini ya Kampuni ya Sumitomo Mitsui Construction Co. Ltd ya nchini Japan. 
Akizungumza katika ziara hiyo alisema lengo ni kuangalia maendeleo ya ujenzi wa mradi huo ili kuhakikisha unakamilika mapema kama ulivyopangwa. Prof. Mbarawa alisema ameridhishwa na maendeleo ya mradi huo ambao mara baada ya kukamilika utarahisisha shughuli za usafiri kwa wananchi watumiao barabara hizo mbili za Nyerere na Mandela jijini Dar es Salaam. 
Mradi huo wa ujenzi unatarajiwa kukamilika ifikapo Oktoba 2018 huku ukitarajiwa kugharimu takribani shilingi bilioni 100, ambapo kati ya fedha hizo shilingi bilioni 93.44 zitatolewa na Japan kupitia Shirika la Ushirikiano wa Kimataifa (JICA), na Serikali ya Tanzania itatoa shilingi Bilioni 8.3.   
Mhandisi Mkazi wa Kampuni ya Sumitomo Mitsui Construction Co. Ltd inayojenga barabara za juu eneo la Tazara, Kiyokazu Tsuji (kulia) akitoa maelekezo kewa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (katikati) maendeleo ya daraja hilo wakati alipotembelea kuangalia maendeleo ya mradi huo. Kushoto ni Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharu Yoshida akishuhudia. Mhandisi Mkazi wa Kampuni ya Sumitomo Mitsui Construction Co. Ltd inayojenga barabara za juu eneo la Tazara, Kiyokazu Tsuji (kulia) akimuonesha Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (katikati) muonekano wa ramani ya daraja hilo na ujenzi unavyoendelea wakati alipotembelea kuangalia maendeleo ya mradi huo. Kushoto ni Balozi wa Japan nchini Tanzania, Masaharu Yoshida akishuhudia.  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Prof. Makame Mbarawa (wa pili kushoto) akipata maelezo juu ya maendeleo ya mradi huo Muonekano wa ujenzi wa barabara za juu unaoendelea eneo la Tazara jijini Dar es Salaam. Muonekano wa ujenzi wa barabara za juu unaoendelea eneo la Tazara jijini Dar es Salaam.

MAKAMU WA RAIS MHE. SAMI SULUHU HASSAN AMRITHI MAMA SALMA KIKWETE ULEZI WA TANZANIA GIRL GUIDES


 
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewataka wasichana ambo ni wanachama wa chama cha Tanzania Girl Guides Association (TGGA) kuzingatia mafunzo wanayopatiwa kwa ajili ya maisha yao ya baadaye. 
 Kauli hiyo aliitoa leo jijini Dar es Salaam wakati akikabidhiwa kijiti cha kuwa mlezi wa chama hicho kutoka kwa Mama Salma Kikwete anayesitaafu nafasi hiyo aliyoihudumu kwa zaidi ya miaka 12.
 “Niwatake tu watoto wangu kutochukulia kwa mzaha mafunzo mnayopatiwa kwani ni tija kwa maendeleo ya Taifa,” alisema Makamu wa Rais. 
Aidha aliwaahidi wanachama kutowaangusha katika kutekeleza majukumu ya kukilea chama hicho ambapo alimpongeza Mama Salma Kikwete kwa kuweza kukiongoza vizuri kwa mafanikio makubwa licha ya kuwa na majukumu mengine. 
Aliahidi kuifanyia kazi changamoto iliyotajwa ya matumizi ya mitandao ya kijamii ambapo alisema atalisimamia hilo kwani ni vizuri kutumia mitandao hiyo kwa kuzingatia maadili kutokana na hivi sasa watu kuitumia vibaya. 
Pia alitoa pendekezo la chama hicho kubuni miradi mingine ambayo inaweza kuwaingizia fedha ili kuacha kutegemea wahisani. Mama Salma Kikwete wakati akimuachia jukumu hilo la kukilea chama hicho alimkabidhi vitu vitatu ambavyo ni Bendera ya Taifa ya chama, Katiba na mpango mkakati wa chama na kumvalisha Skafu ya chama kama ishara ya kukabidhiwa rasmi kijiti hicho. 
 Aidha alisema kuwa chama kimekuwa na mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kuweza kuongeza wanachama kutoka 97,143 hadi kufikia wanachama 100,008 mwaka huu. 
Aliongeza kwamba wanatarajia mwezi Septemba kuapisha wanachama 300 katika mkoa huku akieleza kwamba tayari wamekwisha sajili zaidi ya wanachama 2000 katika mkoa wa lindi.
Aliyekuwa Mlezi wa Chama cha Tanzania Girl Guides (TGGA), Mama Salma Kikwete (kushoto) akimkabidhi  Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan bendera ikiwa ni ishara ya kumpatia ulezi wa chama hicho katika hafla iliyofanyika, kwenye viwanja vya Jumba la Makumbusho Dar es Salaam leo
Mama salma akimkabidhi Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan mpango mkakati wa TGGA
Samia Suluhu Hasan akimkabidhi Mlezi mstaafu wa TGGA zawadi ya saa aliyopewa zawadi na uongozi wa TGGA kwa ajili ya kumbukumbu. PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA - KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Kikundi cha sanaa cha Ilala kikitumbuiza 
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, ambaye pia ni Kamishna wa TGGA, Sophia Mjema akimlaki aliyekuwa Mlezi wa TGGA Mama Salma Kikwete
Mama Salma Kikwete akisalimiana na Kamishna Mkuu wa TGGA, Symphorosa Hangi
Salma Kikwete akisalimiana na Katibu Mkuu wa TGGA, Grace Shaba
Mama Salma Kikwete akisalimiana na Kamishna wa TGGA

Samia akiangalia kazi mbalimbali zinazofanywa na Girl Guides

Samia akipata maelezo  kutoka kwa Mkufunzi wa Girl Guides Ruth kuhusu kazi mbalimbali za TGGA
Samia na Salma Kikwete wakilakiwa na Girl Guides
Brass Band ya Polisi ikiongoza wimbo wa Taifa
Viongozi mbalimbali wakiwa katika sherehe hiyo
Baadhi ya makamishna wa TGGA wakiwa katika sherehe hiyo
Mwenyekiti wa TGGA Profesa Martha Qorro akitambulisha baadhi ya wageni waalikwa
Kamishna Mkuu wa TGGA Symphorosa Hangi akisema neno la utangulizi pamoja na kutambulisha  wageni waalikwa 
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya TGGA, Anna Abdalah akihutubia wakati wa sherehe hiyo
Aliyekuwa Mlezi wa TGGA, Mama Salma Kikwete akihutubia kabla ya kumkabidhi ulezi Makamu wa Rais Samia
Ni furaha iliyoje
Salma Kikwete akimvisha skavu Mlezi mpya wa TGGA, Samia Suluhu Hassan
Wasanii wa Shule ya Msingi Umoja wakitumbuiza wakati wa sherehe hiyo
Ni wakati wa furaha
Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Mjema na Mwenyekiti wa Bodi ya TGGA, Anna Abdalah wakichenza ngoma

Mama Samia akimtunza fedha kiongozi wa kikundi cha Umoja kwa kucheza vizuri
Kamishna Mkuu wa TGGA akimkabidhi zawadi ya saa  Mlezi mstaafu wa TGGA, Mama Salma Kikwete
Mama Salma akionesha Saa hiyo

Girl Guides wakighani shairi maalumu
Baadhi ya makamishna wakiimba wimbo maalumu
NI FURAHA TELE
Viongozi na makamishna wakiwa katika picha ya pamoja na Mlezi mpya wa TGGA, Samia
Mlezi mpya, Mama Samia akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na makamishna wa mikoa
Mama Samia na Salma Kikwete wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa TGGA
Girl Guides wakiwa na Mama Salma Kikwete pamoja na Mlezi mpya, Samia

EVERTON IKIJINOA UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM TAYARI KUIVAA GOR MAHIA

EVERTON IKIJINOA UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR ES SALAAM TAYARI KUIVAA GOR MAHIA

 Basi lililobeba wachezaji wa Timu ya Everton ya nchini Uingereza likiwasili katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mazoezi leo.
 Baadhi ya viongozi wa wa Timu ya Everton ya nchini Uingereza wakishuka katika basi la timu hiyo mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam kwa ajili ya mazoezi leo.
  Mchezaji Wayne Rooney wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza akielekea kufanya mazoezi na wenzie katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salam leo.
 Wachezaji wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza wakiingia katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Wachezaji wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza wakifanya mazoezi katika dinba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Wachezaji wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza wakifanya mazoezi katika dinba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Wachezaji wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza wakifanya mazoezi katika dinba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Wachezaji wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza wakifanya mazoezi katika dinba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Wachezaji wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza wakifanya mazoezi katika dinba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Makipa wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza wakifanya mazoezi katika dinba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Mchezaji Wayne Rooney wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza akifanya mazoezi na wenzie katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salam leo.
  Mchezaji Wayne Rooney wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza akifanya mazoezi na wenzie katika dimba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salam leo.
 Wachezaji wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya mashabiki wa timu hiyo mara baada ya kumaliza mazoezi katika dinba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Wachezaji wa Timu ya Everton FC ya nchini Uingereza wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya mashabiki wa timu hiyo mara baada ya kumaliza mazoezi katika dinba la uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza jambo na Meneja wa Habari wa Timu ya Everton FC  wakati wa mazoezi ya timu hiyo katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Yusuf Omar Singo.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo Prof. Elisante Ole Gabriel akizungumza jambo na Meneja wa Habari wa Timu ya Everton FC  wakati wa mazoezi ya timu hiyo katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo. Katikati ni Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Bw. Yusuf Omar Singo.