Friday 15 December 2017

SERIKALI YA KUWEIT YAAHIDI KUENDELEZA USHIRIKIANO NA SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Kulia akipokea zawadi na Vifaa kwa ajili ya Watu wenye Ulemavu Zanzibar kutoka kwa Balozi wa Kuweit Nchini Tanzania Bwana Jasem Al – Najem.
Balozi wa Kuweit Nchini Tanzania Bwana Jasem Al – Najem akisisitiza umuhimu wa Nchi yake kuendelea kusaidia huduma za Kijamii Nchini Tanzania hasa kwa Watu wenye mahitaji Maalum.
Balozi Seif Kulia akiushukuru Ubalozi wa Kuweit Nchini Tanzania kwa mchango wake mkubwa wa kusaidia huduma za Kijamii Nchini Tanzania.
Balozi wa Kuweit Nchini Tanzania Bwana Jasem Al – Najem Kushoto akibadilishana mawazo na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif katika hafla maalum ya makabidhiwano ya zawadi ya Vifaa kwa ajili ya Watu wenye ulemavu.
Baadhi ya Watu wenye mahitaji maalum pamoja na Wafanyakazi wa Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar wakifuatilia matukio yaliyjiri kwenye hafla maalum ya makabidhiwano ya zawadi ya Vifaa kwa ajili ya Watu wenye ulemavu.

WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA AAGIZA BENKI ZISIZOKIDHI VIGEZO ZIFUTIWE LESENI

 Benny Mwaipaja, WFM, Dodoma
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa, ameiagiza Benki Kuu ya Tanzania BOT kuzifutia leseni benki zote za biashara pamoja na benki za wananchi zitakazoshindwa kukidhi vigezo vya kuendesha shughuli za kibenki nchini.

Ametoa agizo hilo mjini Dodoma katika hotuba iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, wakati akifungua Mkutano Maalum wa Wadau wa Jumuiya ya Benki za Wananchi Tanzania (COBAT).

“kwa taarifa niliyonayo hadi sasa baadhi ya benki hazijatimiza matakwa ya kisheria ya kuwa na mtaji wa kutosha, hali ambayo haiwezi kuachwa iendelea hata kidogo, kwani haiimarishi sekta ya fedha na haiwasaidii wananchi kuendelea kiuchumi” alisema Waziri Kassim Majaliwa katika hotuba hiyo

Alisema Benki Kuu ilitoa muda hadi mwishoni mwa Desemba 2017, benki za wananchi ziweze kuongeza mtaji na kwamba muda huo hautaongezwa na wala Serikali haitatoa mtaji kwa benki hizo.

“Serikali kupitia Benki Kuu ya Tanzania haitasita kuifungia benki yoyote na kufuta leseni yake ya biashara pindi itakapobaini inavunja sheria, ikiwa ni pamoja na kuwa na upungufu mkubwa wa mtaji na ukwasi ambao unahatarisha usalama wa sekta ya fedha na amana za wateja kama tulivyofanya kwa Mbinga Community Bank PLC kuanzia tarehe 12/5/2017” alisema Dkt. Mpango kwa niaba ya Waziri Mkuu.

Maagizo hayo yamekuja siku moja baada ya Mhe. Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, kuiagiza Wizara ya Fedha na Mipango wakati akifungua tawi kuu la Benki ya CRDB mjini Dodoma, kuhakikisha kuwa Benki Kuu ya Tanzania-BOT, inazifuta benki zote zinazoshindwa kujiendesha kibiashara hata kama zinamilikiwa na Serikali kwa asilimia 100.


Alisema Serikali inafanya jitihada mbalimbali ili kuhakikisha benki za wananchi zinaimarika zikiwemo kuruhusiwa kuanzisha mifumo ya ushirikiano katika Nyanja ya Mfumo wa Mawasiliano na Habari (ICT), Idara za Ukaguzi wa Ndani (Internal Audit Services), kupunguza wingi wa idara na kuwa na idara tatu (3) tu muhimu, kuruhusiwa kuungana (Federation), ambazo zitapunguza gharama za uendeshaji wa benki za wananchi na kuleta ufanisi katika kutoa huduma.

“Napenda kusisitiza kuwa sekta ya benki ni muhimu sana kwa uhai na ukuaji wa uchumi kama ilivyo damu kwa mwili wa binadamu na kutokana na umuhimu wake huo, sekta hii ni kati ya sekta chache zinazosimamiwa kwa karibu sana ili kulinda amana za wateja pamoja na kuhakikisha uhimilivu wa mfumo mzima wa sekta ya fedha na mwenendo wa uchumi wa Taifa” aliongeza Dkt. Mpango

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya Benki za Wananchi Tanzania (COBAT) Bw. Rukwaro Senkoro, alisema hadi kufikia Juni, 2017, Benki za Wananchi nchini zilikuwa na wateja zaidi ya milioni 1.4, wateja wa vikundi zaidi ya 10,000, Matawi 12, Vituo 59, na wanahisa 66,492.

“Benki hizo zina amana zenye thamani ya shs bilioni 74.2, zimetoa mikopo ya sh. bilioni 56.8, na jumla ya mali zenye thamani ya shs. bilioni 92.3” Alisema Bw. Senkoro

Hata hivyo, kutokana na Utafiti wa Matumizi ya Huduma za Kifedha uliofanyika mwaka 2017 umebaini kuwa asilimia 28 ya wananchi bado hawapati huduma za kifedha hapa nchini hususan vijijini na kutaja changamoto ya ukosefu wa mitaji ya benki hizo kukwaza sekta hiyo.

Dhana kuu ya mkutano huo wa COBAT uliowashirikisha wadau mbalimbali kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ni “Mitaji na Mpango wa Kuziunganisha Benki za Wananchi Tanzania”, ambayo ni dhana mpya.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akihutubia katika mkutano maalum wa wadau wa Jumuiya ya Benki za Wananchi-COBAT, uliofanyika mjini Dodoma ili kujadili masuala ya Mitaji na Mpango wa Kuziunganisha Benki za Wananchi Tanzania.
Washiriki wa mkutano maalum wa wadau wa Jumuiya ya Benki za Wananchi wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa mkutano huo uliofunguliwa na Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (hayupo pichani), kwa niaba ya Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Mjini Dodoma.
Naibu Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dkt. Benard Kibesse (kushoto) na Afisa Mtendaji Mkuu wa Jumuiya ya Benki za Wananchi –COBAT, Bw. Rukwaro Senkoro, wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mhe. Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, iliyosomwa kwa niaba yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), mijini Dodoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia), akifurahia jambo na Mbunge wa Mtwara Vijijini ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Mhe. Hawa Ghasia baada ya kufungua mkutano wa wadau wa Jumuiya ya Benki za Wananchi-COBAT, uliofanyika kwenye ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango mjini Dodoma.

VILIO VYATAWALA WAKATI MIILI YA ASKARI WA JWTZ WALIOUAWA DRC IKIWASILI ZANZIBAR

Miili ya Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania {JWTZ} ikiteremshwa kwenye ndege ya JW 8029 katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Aman Karume ikitokea Mjini Dar es salaam.
Balozi Seif pamoja na Mkuu wa Jeshi la Nchi Kavu Meja General Sharif Sheikh Othman wakitoa heshima wakati Miili ya mwashujaa ikiteremshwa kwenye ndege.
Balozi wa Kuweit Nchini Tanzania Bwana Jassem Alnajem wa kwanza kutoka kushoto akijumuika pamoja na Viongozi wa Kiserikali katika kuipokea Miili ya askari wa Tanzania waliouawa Nchini DRC Wiki iliyopita.
Mawaziri mbali mbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar wakishuhudia kuwasili kwa Miili yaWanajeshi wa Tanzania waliouawa na waasi wa ADF Nchini DRC.
Balozi Seif akiongoza Viongozi na Wananchi wa Zanzibar katika kuipokea miili ya Makeshi ya Tanzania yaliyouawa Nchini Jamuhuri ya Kisemokrasi ya Congo.
Majeshi ya Wananchi wa Tanzania wakiichukuwa Miili ya Askari wenzao wakiwasili katika Viwanja vya Makao Makuu ya Brigedia Nyuki Migombani kwa ajili ya kuagwa rasmi Kiserikali.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akitoa salamu za pole kwenye shughuli Maalum ya Kuiaga Miili ya Wanajeshi wa JWTZ hapo Migombani Mjini Zanzibar.

RAIS DKT. MAGUFULI AFUNGUA MKUTANO MKUU WA CHAMA CHA WALIMU TANZANIA (CWT) MKOANI DODOMA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na mamia ya wanachama wa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) kabla ya kufungua mkutano huo Mkuu wa (CWT )katika ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma. Wanachama hao wa CWT walisimama na kushangilia mara baada ya ahadi ya Rais Dkt. Magufuli kuwaahidi kuendelea kutatua kero zao mbalimbali.
Mamia ya Wajumbe wa Chama cha Walimu(CWT) wakishangilia ndani ya ukumbi wa Chimwaga wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipokuwa akijibu kero zao mbalimbali walizoziwasilisha.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na baadhi ya wajumbe wa Chama cha Walimu CWT mara baada ya kuwahutubia katika ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshikana mikono na viongozi wa muda wa CWT, Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako, Spika wa Bunge Job Ndugai, pamoja na mke wa Rais Mama Janeth Magufuli wakiimba wimbo wa mshikamano pamoja na Wajumbe wote wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) katika ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wakiwa wameshikana mikono wakati wakiimba wimbo wa mshikamano kabla ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kuhutubia na kufungua mkutano huo wa CWT katika ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.

MAJALIWA AMWAKILISHA JPM KUAGA MIILI YA ASKARI 14 WA JWTZ WALIOUAWA WAKIWA KWENYE OPERESHENI YA ULINZI WA AMANI CHINI YA UMOJA WA MATAIFA NCHINI DRC

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Nchini, Jenerali Venance Mabeyo baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Upanga jijini Dar es salaam Desemba 14, 2017, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli katika kuaga miili ya askari 14 wa JWTZ waliouawa wakiwa katika operesheni ya ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa nchini Congo - DRC. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu,. Kassim Majaliwa akisalimiana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dkt. Hussein Mwinyi baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Upanga jijini Dar es salaam Desemba 14, 2017, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli katika kuaga miili ya askari 14 wa JWTZ waliouawa wakiwa katika operesheni ya ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa nchini Congo - DRC. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitia saini kitabu cha maombolezo baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Upanga jijini Dar es salaam Desemba 14, 2017, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli katika kuaga miili ya askari 14 wa JWTZ waliouawa wakiwa katika operesheni ya ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa nchini Congo - DRC. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Jakaya Mrisho Kikwete baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Upanga jijini Dar es salaam Desemba 14, 2017, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli katika kuaga miili ya askari 14 wa JWTZ waliouawa wakiwa katika operesheni ya ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa nchini Congo - DRC. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika ya Mashariki, Dkt. Susan Kolimba baada ya kuwasili kwenye viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Upanga jijini Dar es salaam Desemba 14, 2017, kumwakilisha Rais John Pombe Magufuli katika kuaga miili ya askari 14 wa JWTZ waliouawa wakiwa katika operesheni ya ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa nchini Congo - DRC. Katikati ni Rais Mstaafu wa Awamu wa Nne, Jakaya Mrisho Kikwete na kushoto Katibu Mtendaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika - SADC. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Askari wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakiwa wamebeba miili ya askari 14 wa JWTZ waliouwa wakiwa kwenye operesheni ya ulinzi wa amani chini ya Umoja wa Mataifa nchini Congo - DRC,`kwenye viwanja vya Makao Makuu ya JWTZ Upanga jijini Dar es salaam Desemba 14, 2017. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa alimwakilisha Rais John Pombe Magufuli katika kuaga miili ya askari hao. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Tuesday 12 December 2017

TASWIRA KUTOKA JOSIAH GIRL'S SEC SCHOOL ILIYOPO BUKOBA





TASWIRA KUTOKA UWANJA WA NDEGE, JAMCO BLOG TWATETA JAMBO KWA KINA!




KIWANDA CHA SARUJI TANGA (SIMBA CEMENT) YATOA MIFUKO 760 KUCHANGIA UJENZI WA VYUMBA VYA MADARASA SHULE YA MSINGI PONGWE JIJINI TANGA


Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akipanga tofali kwenye msingi wa ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya msingi ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) na wasioona ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo

Mkurugenzi Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart kulia akijenga tofati katika vyumba vipya vitatu vya madarasa kwenye shule ya Msingi ya
ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) na wasioona ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa

Mkurugenzi Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart kulia akiweka tofati katika vyumba vipya vitatu vya madarasa kwenye shule ya Msingi ya
ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) na wasioona ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa



Mkurugenzi Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart kulia akiweka sawa tofati katika msingi wa moja ya vyumba vipya vitatu vya madarasa kwenye shule ya Msingi ya ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) na wasioona ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo

Mkurugenzi Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart kulia akimuelekeza jambo mmoja wa wakandarasi watakaojenga vyumba vitatu vya madarasa katika shule ya wanafunzi wenye maahitaji maalumu ikiwemo wasiona na wenye ulemavu wa ngozi (Albino) ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo



Mkurugenzi Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart kulia akiweka sawa tofati katika msingi wa moja ya vyumba vipya vitatu vya madarasa kwenye shule ya Msingi ya ya wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi (Albino) ya Pongwe Jijini Tanga ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo

Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa akizungumza katika halfa hiyo iliyofanyika leo kwenye shule ya Msingi Pongwe Jijini Tanga



Mkurugenzi Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya uzinduzi huo leo



Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Pongwe Yahaya Mafita mara baada ya kutoa hotuba fupi katika uzinduzi huo leo ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo ambapo aliishukuru kampuni hiyo kwa kuthamini juhudi za kuinua elimu

Diwani wa Kata ya Pongwe(CCM),Mbaraka Sadi akizungumza katika uzinduzi huo ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo



Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga akizungumza katika uzinduzi huo leo kwenye shule ya Msingi Pongwe ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo


Mkurugenzi Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart kushoto akipongezwa na Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Pongwe Yahaya Mafita mara baada ya kutoa hotuba fupi katika uzinduzi huo leo ambapo Kampuni ya Simba Cement imetoa mifuko 760 kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa vyumba hivyo
Mkurugenzi Kiwanda cha Saruji cha Simba Cement cha Tanga (TTCL), Reinhardt Swart katikati akifuatilia uzinduzi wa ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye shule hiyo uliofanywa leo na Mkuu wa wilaya ya Tanga,Thobias Mwilapwa kushoto ni Afisa Uhusiano wa Simba Cement Noor Mtanga