Saturday 2 May 2015

BALOZI KAGASHEKI AISHUKURU DENMARK KWA MSAADA WA GARI LA KUZIMA MOTO MANISPAA YA BUKOBA.

 Mbunge wa Bukoba mjini balozi Khamis Sued Kagasheki ameishukuru serikali ya Denmark kupitia kwa ujumbe wa watu sita unaongozwa na Meya wa mji wa  Nykobing Mors kwa kutoa gari la zima moto katika Manispaa ya Bukoba,Mh Kagasheki akiongea kwa niaba ya wananchi wa jimbo la Bukoba katika hafla fupi ya chakula cha jioni alichokiandaa kwa ajili wageni nyumbani kwake, amesema gari hili la zima moto limekuja wakati muafaka maana gari lililokuwepo lilipata ajari na bado halijafanyiwa matengenezo, amewataka waliokabidhiwa gari hilo kutambua kuwa gari hilo ni la gharama kubwa na wanao wajibu wa kutambua na kuhakikisha wanalitunza vizuri.Akiongea kwa niaba ya ujumbe aliofuatana nao Mstahiki meya wa mji wa Nykobing Mors amesema gali hili la zima moto ni  ombi maalumu lilitolewa na Mh Samwel Ntambala Rwangisa kipindi akiwa Meya wa Manispaa ya Bukoba, Hivyo mahusiano yake mazuri aliyoyatengeneza kati  ya Manispaa ya Bukoba na  Mji wa  Nykobing Mors kwa urafiki wa muda mrefu  ndio umezaa matunda ya kutoa msaada wa gari la zima moto.( katika picha mh Kagasheki akimtambulisha mkurugenzi wa Cosad nchini Tanzania Bw Smart Baitan.)
 Gari la zima moto liliokabidhiwa katika Manispaa ya Bukoba, ikiwa ni maombi ya Mh Samweli Rwangisa kipindi akiwa meya wa Manispaa ya Bukoba.
 Ni Bango linalothibitisha urafiki wa muda mrefu wa miji hii miwili tangu mwaka 1983.
 Wa pili kulia ni Bw Benard Matungwa, akiwa na Bw Abdul Kagasheki wakipokea wageni.
 Mzee Rutabingwa akiongoza ujumbe kutoka Denmark akipokelewa na mh Kagasheki nyumbani  kwake .
 Mh Kagasheki akimkaribisha makamu meya wa mji wa Nykobing Mors.
 Mh Kagasheki akiongea na ugeni.
 Mwenyeji wa ujumbe huu Mzee Rutabingwa akitambulisha wageni.
 Mstahiki Meya wa Mji wa Nykobing Mors akitoa neno la shukrani na kuhaidi kuendeleza mahusiano mazuri na Manispaa ya  Bukoba.
 Bw Smart Baitan.
 Mh Kagasheki akiongea na Bw Malingumu.
 Bw Jum,anne Bingwa akikaribisha wageni vinywaji.
 Mama Annamary kutoka Dernmark akimpa zawadi mh Kagasheki na moja ya kipeperushi kumuonyesha shughuli mbalimbali wanazosaidia na hasa wakina mama katika kuondokana na wimbi la umasikini.
 Bw Smart Baitan akiteta na Meya wa Nykobing Mors.
 Picha ya pamoja.
 Mzee Rutabingwa  akiongea na mtangazaji wa redio kasibante, bw Richard Kalumuna.
Jamco bukoba.blogspot inawatakia usomaji mwema wa habari  na matukio.kama una tangazo  au habari yako tupigie 0754 757157 au 0788 707027.

Monday 27 April 2015

YANGA BINGWA 2015,YAINYUKA POLISI MORO 4-1



Simon Msuva (kushoto) akishangilia na Amis Tambwe baada ya Tabwe kuipatia timu yake bao la katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Yanga imeshida 4-1. (Picha na Francis Dande)

Mashabiki wa Yanga wakishangilia bao lililofungwa na Amis Tambwe.

Mshambuliaji Wa Yanga, Simon Msuva akimtoka beki wa Polisi Moro, Hassan Mganga katika mchezo wa Ligi Kuu ya Soka Tanzania Bara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Shabiki wa Yanga akifurahia bao la pili la timu yake.
Wachezaji wa Yanga wakishangilia baada ya kumalizika kwa mchezona Yanga kuibuka na ushindi wa mabao 4-1.
Amis Tambwe akipokea mpira baada ya kufunga"Hat Trick"

WAZIRI MKUU PINDA ASISITIZA UWAZI KATIKA MATUMIZI YA TAKWIMU SAHIHI


Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda akionyesha kitabu kinachoeleza Maendeleo na historia ya Takwimu katika Bara la Afrika alichokizindua leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Rais wa Taasisi ya Kimataifa ya Takwimu (ISI) Bw. Vijay Nair na kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS).

Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda akizindua kitabu kinachoeleza Maendeleo na historia ya Takwimu katika Bara la Afrika alichokizindua leo jijini Dar es salaam. Kushoto ni Rais wa Taasisi ya Kimataifa ya Takwimu (ISI) Bw. Vijay Nair na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) kushoto kwa Waziri Mkuu na Prof. Ben Kiregyeza (kulia) ambaye ndiye mwandishi wa kitabu hicho.

Waziri Mkuu Mhe. Mizengo Pinda akifungua Kongamano la Kimataifa la Siku 3 la Wakuu wa Taasisi za Takwimu wa nchi 38 za Afrika na 18 kutoka nje ya Bara la Afrika leo jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu Dkt. Albina Chuwa awali akizungumza na Wakuu wa Taasisi za Takwimu wa nchi 38 za Afrika na 18 kutoka nje ya Bara la Afrika waliohudhuria Kongamano la Siku 3 la Kimataifa kujadili Matumizi ya Takwimu leo jijini Dar es salaam.



Rais wa Taasisi ya Kimataifa ya Takwimu (ISI) Bw. Vijay Nair akizungumza kabla ya uzinduzi wa Kongamano la Kimataifa la masuala ya Takwimu la Wakuu wa Taasisi za Takwimu wa kutoka Afrika na nje ya Afrika.

Waziri Mkuu akizungumza jambo na Makamu wa Rais wa Taasisi ya Kimataifa ya Takwimu (ISI) Bi. Irena Krizman leo jijini Dar es salaam mara baada ya kufungua kongamano la Wakuu wa Taasisi za Takwimu wa nchi 38 za Afrika na 18 kutoka nje ya Bara la Afrika. Katikati ni mjumbe kutoka ya Kusini Bw. Pali Lihohla.

Waziri Mkuu akizungumza akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam mara baada ya kufungua kongamano la Wakuu wa Taasisi za Takwimu wa nchi 32 za Afrika na 18 kutoka nje ya Bara la Afrika.

Waziri Mkuu akizungumza akizungumza akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu mara baada ya kufungua kongamano la Kimataifa la Wakuu wa Taasisi za Takwimu kutoka nchi 32 za Afrika na 18 za nje ya Bara la Afrika.

Waziri Mkuu akizungumza akiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Taasisi za Takwimu kutoka nchi 32 za Afrika na 18 za nje ya Bara la Afrika waliohudhuria Mkutano wa siku 3 wa Takwimu jijini Dar es salaam.

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, LAZARO NYALANDU ATEMBELEA CHUO CHA USIMAMIZI WANYAMAPORI PASIANSI-MWANZA

Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akiangalia moja ya kompyuta maalum zinazotumiwa wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi Wanyamapori Pasiansi mjini Mwanza alipokwenda kukagua vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa na Taasisi ya Buffet Foundation kwa jili ya mafunzo ikiwemo vitabu, kompyuta, magari na darubini.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akijaribu akikagua moja ya vitanda na hema linazotumiwa na wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi Wanyamapori Pasiansi mjini Mwanza alipokwenda kukagua vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa na Taasisi ya Buffet Foundation kwa ajili ya mafunzo ikiwemo vitabu, kompyuta, magari na darubini.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akishuka kutoka basi linalotumiwa na wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi Wanyamapori Pasiansi mjini Mwanza alipokwenda kukagua vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa na Taasisi ya Buffet Foundation kwa ajili ya mafunzo ikiwemo vitabu, kompyuta, magari na darubini

Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akicheza na mwanafunzi wa Chuo cha Usimamizi Wanyamapori Pasiansi mjini Mwanza alipokwenda kukagua vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa na Taasisi ya Buffet Foundation kwa ajili ya mafunzo ikiwemo vitabu, kompyuta, magari na darubini.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akizungumza na wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi Wanyamapori Pasiansi mjini Mwanza alipokwenda kukagua vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa na Taasisi ya Buffet Foundation kwa ajili ya mafunzo ikiwemo vitabu, kompyuta, magari na darubini.

Wanafunzi wa Chuo cha Usimamizi Wanyamapori Pasiansi mjini Mwanza wakinyanyua juu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu jana,alipokwenda kukagua vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa na Taasisi ya Buffet Foundation kwa ajili ya mafunzo ikiwemo vitabu, kompyuta, magari na darubini.

Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu akikwagua gwaride la heshima jana alipowasili Chuo cha Usimamizi Wanyamapori Pasiansi mjini Mwanza alipokwenda kukagua vifaa mbalimbali vilivyonunuliwa na Taasisi ya Buffet Foundation kwa jili ya mafunzo ikiwemo vitabu, kompyuta, magari na darubini.