Saturday 1 November 2014

MWEKEZAJI NAFTARI FELIX TIBENDELANA AJENGA JENGO LA KITEGA UCHUMI MULEBA,LENYE HOTEL, VYUMBA VYA BIASHARA, UKUMBI MKUBWA NA NIGHT CLUB YA KISASA,KUFUNGULIWA RASMI 5-12-2014.

Ni mmiliki wa Jengo la kitega uchumi la kisasa lililo  katika hatua za mwisho kufunguliwa Bw Naftari Felix ana kwea ana na camera yetu, Bw Nafu amesema ameamua kuweka kitega uchumi katika wilaya ya Muleba kwa sababu ya kusogeza huduma bora kwa wakazi wa Muleba na kutambua kwamba  ni lazima sasa wazawa watambue kuleta m,aendeleo nyumbani. Jengo hilo lenye eneo la hotel, ukumbi mkubwa wa mikutano na shughuri mbalimbali,vyumba vya biashara mbalimbali,na Night club ya kisasa ambayo katika kanda ya ziwa itakuwa Muleba.Amesema huduma zote hizo zitazinduliwa rasmi tarehe 5-12-2014.Bw Nafu amesema siku ya ufunguzi anategemea kuzindua kwa stail ya aina yake kwani marafiki zake wapendwa wamemchangia kiasi cha shilingi milioni  therasini kwa ajiri ya kumuunga mkono ,hivyo anatarajia kwenye ufunguzi kuwepo kiongozi  mzito ambae hakumtaja jina ,ila amesema itakuwepo band kubwa ya hapa nchini itakayotoa burudani kwa wageni waalikwa, pia wasanii wa kubwa hapa nchini akiwemo  Mrisho mpoto watatoa Burudani.Amesema baada ya shughuri za Ibada wakati wa asubuhi,jioni sherehe zitaendelea ikiwa ni pamoja na ufunguzi wa Night Club.
Ni muonekano kwa mbali baadhi ya majengo.
Kitega uchumi hiki kipo mkabala na jengo la NMB Muleba.
Sehemu ya maduka ya biashara.
Sehemu ya nje ya kuingia kwenye ukumbi wa mikutano.
Ni jengo la aina yake kwa Muleba.
Sehemu ya ukumbi wa mikutano wakiendelea na matengenezo, utakuwa na uwezo  wa watu  2000.
Matengenezo yakiendelea.
Sehemu ya Night club.
Matengenezo yakiendelea sehemu ya Night club.
Itakuwa ni Night club ya pekee kanda ya ziwa.
Eneo la hotel matengenezo yakiendelea.
Bw Nafu akifuatilia mafundi wanavyoendelea na kazi.
Ufunguzi rasmi ni tarehe 5-12-2014 Muleba .

Monday 27 October 2014

MSANII LULU AITAMBULISHA FILAMU YAKE MPYA IITWAYO MAPENZI YA MUNGU LEO.FILAMU YAINGIA SOKONI LEO


 Msanii wa Sanaa ya Maigizo Nchini, Elizabeth Michael almaarufu kama Lulu akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa Alipokuwa akiitambulisha filamu yake Mpya iitwayo MAPENZI YA MUNGU ambayo amewashirikisha Flora Mtegoha au Mama Kanumba na Msanii wa Muziki wa Kizazi Kipya Linah Sanga.
 Msanii Wa Maigizo Nchini, Elizabeth Michael almaarufu kama Lulu akiitambulisha filamu yake Mpya iitwayo MAPENZI YA MUNGU leo mbele ya wanahabari (hawapo pichani).,Kulia ni Mmoja kati wa wasanii walioshiriki katika filamu hiyo ajulikanae kama Flora Mtegoha almaarufu kama Mama Kanumba
Meneja Masoko wa Kampuni ya Proin Promotions Ltd, Evance Stephen akiongea na wanahabari leo katika Ofisi za Proin Promotions Ltd zilizopo Mikocheni mtaa wa Ursino wakati wa Utambulisho wa Filamu mpya ya Lulu Iitwayo MAPENZI YA MUNGU.

Msanii Elizabeth Michael aka Lulu leo ametambulisha Filamu yake Mpya ambayo imeingia sokoni leo iitwayo MAPENZI YA MUNGU, huku akiwa amemshirikisha Msanii wa Bongo Fleva Linah Sanga na Mama Kanumba.

Wakati akiilezea filamu hiyo leo mbele ya wanahabari Lulu amesema Kuwa Ni Filamu inayofundisha na Kutoa somo kwa mtu yoyote yule ambae yupo hapa duniani kwa kuendelea kuonyesha kuwa MUNGU YUPO. Akiongezea kuwa..."Sisi kama binadamu tumekuwa tukifanya mambo mengi sana hapa Duniani na kupelekea kumsahau Mungu na pengine kuendelea kufikiria kuwa yote tuyafanyayo ni kwa uwezo wetu kumbe Sio uwezo wetu na Ni Mapenzi ya Mungu tu ndio yanayofanya sisi kufikia hapa tulipo leo"

Filamu ya MAPENZI YA MUNGU imekuwa gumzo kabla ya kutoka kutokana na watanzania wengi kuwa na shauku ya Kutaka kumuona Lulu tena mara baada ya Kuonekana  katika Filamu Zake Mbili zilizotangulia za FOOLISH AGE na FAMILY CURSE. Sasa Lulu kuonekana tena katika kiwango cha Juu katika Filamu hii Mpya ambayo imeingia Sokoni Leo.


Sunday 26 October 2014

MAADHIMISHO YA MWAKA MPYA WA KIISLAM 1436 KITAIFA WASHEREKEWA MKOANI KAGERA MANISPAA YA BUKOBA

 Waislamu kote duniani wamesherekea mwaka mpya wa kiislamu wa 1436,Kitaifa nchini Tanzania madhimisho ya mwaka mpya wa kiislamu yamefanyika Mkoani Kagera katika Manispaa ya Bukoba na mgeni rasmi alikuwa Mufti wa Tanzania.
 Waumini wakiislamu wakiwa katika matembezi ya amani kusherekea mwaka mpya wa kiislamu mitaa mbalimbali ya Bukoba mjini.
 Matembezi ya amani kuelekea uwanja wa Uhuru Platform uswahilini Bukoba.
 Mufti wa Tanzania  ndio aliepokea matembezi ya amani.
 Shekhe Mustafa akiwasili viwanja vya Uhuru.
 Baba Askof Buberwa wa Kanisa la Kilutheri nae alishiriki sherehe za mwaka mpya wa kiislamu.
 Quruani tukufu ya ufunguzi wa sherehe ikisomwa.
 Mkuu wa Mkoa wa Kagera kanal mstaafu Fabian Massawe akisalimiana na waislamu na kuwatakia heri ya mwaka wa kiislamu.
 Alhaj Ayub Kagera mwenyekiti wa Bakwata Bukoba Mjini.
 Mashekhe kutoka mikoa mbalimbali nchini na viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini.
 Mkurugenzi wa Kasibante redio Richard Leo (kulia)akiwa na Yusuf Abed mtangazaji wakiwa Live Kasibante redio 88.5
 Channel 4 Tv wakichukua matukio.
 Ustadhi Chakindo.
 Kaswida wakitoa burudani.
 Dufu la Kansenene.
 Bi Sakina akifurahia dufu.
Ni dua ya kufunga sherehe mida ya saa saba usiku katika viwanja vya Uhuru platy form Bukoba.