Friday 14 April 2017

WATANZANIA WAISHIO ALGERIA WAUPOKEA MSAFARA WA YANGA KWA SHANGWE


 Kikosi cha wawakilishi watanzania katika michuano ya kimataifa ya kombe la Shirikisho barani Afrika Yanga wamewasili salama nchini Algerai kwa ajili ya mchezo wao marudiano dhidi ya MC Alger utakaochezwa kesho majira ya saa 2 usiku kwa saa za Afrika Mashariki.

Katika msafara huo uliiongozwa na Katibu Mkuu wa Yanga Charles Boniface Mkwasa umefika salama na ukipokelewa na watanzania wanaoishi nchi Algeria na kufurahishwa na mapokezi hayo na kuahidi ushindi kwa watanzania.

Msafara wa wachezaji hao uliingia kwa mafungu mawili ambapo kundi la kwanza liliwasili likiongozwa na benchi la ufundi la timu hiyo likiwa na kocha Mkuu George Lwandamina huku kundi la pili likiwasili  na Katibu Mkuu.

Mtanzania Hamis Mwampese anayeishi nchini Algeria amesema kuwa timu ya Algers wameingia uoga hasa baada ya kuona Yanga wamechelewa kuingia nchini humo na zaidi kwa kufanya hivyo wameepusha sana kufanyiwa hujuma na wenyeji wa nchi hiyo.

Yanga wamefikia katika Hotel ya nyota tano inayojulikana kwa jina la Sultan ambapo si mbali sana na Uwanja ulipo utakaochezewa kesho katika mechi hiyo ya marudiano ambapo Yanga wanatakiwa kupata ushindi wa aina yoyote au sare.

Mtanzania Hamis Mwampese akisalimiana na Katibu Mkuu wa Yanga Charles Mkwasa baada ya kuwasili Jijini Algeria  kwa ajili ya mechi ya marudiano ya hatua ya mtaoano wa Kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Mc Alger ambapo katika mechi ya awali Yanga walitoka na ushindi wa goli 1-0..
 
Mtanzania Hamis Mwampese  akiwa katika picha mbalimbali na wachezaji wa timu hiyo baada ya kuwasili nchini Algeria kwa ajili ya mechi ya marudiano ya hatua ya mtaoano wa Kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Mc Alger ambapo katika mechi ya awali Yanga walitoka na ushindi wa goli 1-0.

JESHI LA POLISI LATANGAZA VITA NA MSAKO KALI DHIDI YA WAHALIFU WAUAJI WA ASKARI WANANE


Kamishina wa Operesheni na Mafunzo ya Polisi, Nsato Marijani, akizungumza na waandishi wa habari kwenye Ofisi za Wizara ya Mambo ya Ndani, wakati akitoa tamko kuhusu operesheni itakayoendeshwa na jeshi hilo ya kuwasaka wahalifu waliohusika na mauaji ya Askari nane katika msitu wa Jaribu Mpakani Mkoa wa Pwani juzi. Kushoto ni Msemaji wa Jeshi la Polisi, Advera Bulimba 

''Tunaomba wananchi watusamehe kwa poeresheni hii tunayokwenda kuianza, kwani askari wanane ni wengi sana na hatutakuwa na msalie mtume kwa hili, wameanza sisi tunamaliza, na jana ilikuwa ni 8 - 4, lakini tukianza nawaambia mabao yetu yatakuwa ni zaidi yao'';. alisema Marijani

Aidha Marijani ametangaza kuwa eneo hilo ni marufuku waendesha pikipiki kupita zaidi ya saa kumi na moja jioni.

Monday 10 April 2017

MEYA MANISPAA YA BUKOBA ATOA WITO KWA SERIKALI KUUNGA MKONO JITIHADA ZA KUENDELEZA ELIMU

Meya wa Manispaa ya Bukoba Chief Kalumuna ametoa wito kwa serikali ya awamu ya tano kuwaunga mkonona kuwawezesha watanzania wanaowekeza katika elimu kwa kujenga mashule kwa kutowawekea  vikwazo na urasimu wanapoamua kuwekeza katika elimu,Mstahiki meya aliyasema hayo alipokuwa akiongea na wazazi wa wanafunzi wa  shule ya Henry English medium primary and pre primary school iliyoko katika kata ya Rwamishenye Manispaa ya Bukoba wakati wa hafla ya kufunga muhula wa kwanza.(katika picha wa tatu kushoto ni Meya Chief Kalumuna akiwa na viongozi mbalimbali.)
Muonekano wa kazi.
Kushoto, mstahiki meya, mkurugenzi mkuu wa shule Bw Simeo,mwana na mkewe, wa mwisho ni afisa Elimu Msaidizi Manispaa ya Bukoba.


Wakurugenzi wa Henry English Medium primary and pre primary school.