Tuesday 15 March 2016

GESI YENYE UJAZO WA FUTI TIRIONI 2.17 YAGUNDULIKA BONDE LA RUVU MKOANI PWANI


Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhomgo (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam leo asubuhi, kuhusu kugundulika kwa futi za ujazo wa Gesi Tirioni 2.17 katika Bonde la Ruvu mkoani Pwani, katika eneo la Mamba Kofi One ikiwa ni moja ya ugunduzi ulifanywa na Kampuni ya Dodsal ikishirikiana na Shirika la Maendeleo ya Petroli na Tanzania (TPDC). Kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Justin Ntalikwa.

Makamu wa Rais Uendeshaji na Meneja Mkuu wa Kampuni ya Haydrocarbons and Power Limited (DODSAL), Tom Gray (kulia), akizungmza katika mkutano huo kuhusu kugundulika kwa gesi hiyo ambayo itachimbwa na kampuni yake hiyo.

Meneja Utafiti wa Shirika la Maendeleo ya Mafuta na Gesi Tanzania, Venosa Ngowi (wa pili kulia), akizungumza katika mkutano huo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justin Ntalikwa (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu, Dk.Juliana Pallangyo wakiwa katika mkutano huo.

Mkutano ukiendelea.

Na Dotto Mwaibale
SERIKARI imetangaza rasmi kugundulika kwa futi za ujazo wa Gesi Tirioni 2.17 katika Bonde la Ruvu mkoani Pwani, katika eneo lijulikanalo kama Mamba Kofi One ikiwa ni moja ugunduzi ulifanywa na Kampuni ya Dodsal ikishirikiana na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC).
Akitoa tamko hilo mbele ya vyombo vya habari ofisini kwake Dar es Salaam leo asubuhi, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alisema kuwa hadi kufikia Machi mwaka huu jumla ya gesi yote iliyogunduliwa nchini ni trioni 57.23.

"TPDC imerekebisha muundo wake tunataka iwe inajishughulisha na utafutaji wa gesi ya mafuta hivyo kufuatana na sheria ya petroli ya mwaka jana kazi zote zitasimamiwa na TPDC na haitaendelea kusimamia makampuni mengine badala yake tuameazisha wakala wakusimamia kazi ," alisema Muhongo.

Rais Dkt Magufuli awapa siku 15 Wakuu wa Mikoa kuwaondoa watumishi hewa walio katika orodha ya malipo ya mishahara ya watumishi wa umma katika Mikoa yao

Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza mbele ya Waku wa Mikoa mara baada ya kuwaapisha leo Ikulu jijini Dar.Rais Dkt Magufuli amewapa siku 15 Wakuu wa Mikoa kuwaondoa watumishi hewa walio katika orodha ya malipo ya mishahara ya watumishi wa umma katika Mikoa yao.Picha na Michuzi Jr-MMG
Na Jacquiline Mrisho- Dar es salaam.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewapa siku 15 Wakuu wa Mikoa kuwaondoa watumishi hewa walio katika orodha ya malipo ya mishahara ya watumishi wa umma katika Mikoa yao.

Rais Dkt. Magufuli amesema hayo leo Ikulu Jijini Dar es salaam baada ya kuwaapisha Wakuu wa Mikoa aliowateua Machi 13 mwaka huu ambapo amewaagiza washirikiane na Wakurugenzi wa Halmashauri kuwaondoa watumishi hewa.

“Nimewapa siku 15 kuanzia leo mkashirikiane na Wakurugenzi wa Halmashauri zenu kuwatoa wafanyakazi hewa, nikigundua kuwa bado kuna wafanyakazi hewa, Mkurugenzi husika atafukuzwa kazi na atapelekwa mahakamani”,
Na kusisitiza “Nimeamua kuwachagua nikiamini kwamba mtaniwakilisha vizuri katika Mikoa yenu, nawaomba mkatimize majukumu yenu bila kuogopa” alisema Dkt. Magufuli.
Aidha, Mhe. Dkt. Magufuli amesikitishwa na utafiti wa watumishi uliofanywa katika Mikoa ya Singida na Dodoma ambapo imegundulika watumishi 202 wanalipwa mishahara hewa.

Wakati wa utafiti huo, zaidi ya watumishi 26,900 walioko katika Halmashauri 14 za Mikoa hiyo, watumishi 3,320 hawakuwepo kazini kwa sababu mbalimbali.Kwa mantiki hiyo, ukichukua utafiti huo wa Mikoa miwili ni dhahiri Serikali inapoteza mapato mengi kwa kulipa mishahara ya watumishi hewa nchi nzima.

RAIS DKT MAGUFULI AMEWAAPISHA WAKUU WA MIKOA IKULU LEO JIJINI DAR


Wakuu Wateule wa Mikoa wakisubiri kuapishwa na Rais

Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan akizungumza jambo naMh Angellah Kairuki















Wakuu wa Mikoa wapya kabla ya kuapishwa wakifuatilia yaliyokuwa yakijiri Ikulu,mapema leo jijini Dar

Wageni waalikwa mbalimbali wakiwemo viongozi wa Ulinzi na Usalama

Wakuu wa Mikoa wakitia Saini hati kiapo cha Maadili ya viongozi wa Umma leo mara baada kuapishwa Ikulu jijini Dar






WAZIRI MKUU AMPA RAS KAGERA SIKU 5 AMLETEE TAARIFA

*Ni za matumizi ya sh. milioni 120 za Hospitali ya Mkoa

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekagua hospitali ya rufaa ya mkoa wa Kagera na kumpa siku tano Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa huo, Bw. Adam Swai amletee taarifa juu matumizi ya sh. Milioni 80 ambazo ni fedha za UKIMWI.
Pia amemtaka ifikapo Machi 20, nwaka huu awasilishe taarifa nyingine ya matumizi ya sh. Milioni 40 za ukarabati wa jengo la wagonjwa maalum (Grade A)
Ametoa agizo hilo leo asubuhi (Jumanne, Machi 15, 2016) wakati akizungumza na watumishi wa hospitali hiyo baada ya kutembelea maeneo kadhaa yakiwemo wodi ya watoto, wodi ya wazazi, chumba cha wagonjwa mahututi (ICU ) na chumba cha kuhifadhia maiti.
"Kulikuwa na frsha za ukimwi sh. Milioni 80 ambapo kila mtumishi alipaswa kupata sh. 200,000/- lakini ninyi mmewapa sh. 80,000 /-. RAS fedha hizi zimeenda wapi? Nataka uniletee taarifa ofisini kwangu Dar es Salaam ifikapo tarehe 20 mwezi huu," alisema huku akishangiliwa.

"Kwa mujibu wa taarifa ya CAG pale grade A kuna mgogoro wa sh. milioni 40. Wewe taarifa unayo lakini hujaifanyia kazi yoyote. Nataka tarehe 20 nayo hii pia niipate na nione umetoa mapendekezo gani."

Kuhusu tatizo la madaktari katika hospitali hiyo, Waziri Mkuu alisema atawasiliana na Waziri wa Afya ili madaktari watano ambao wanasubiri ajira rasmi lakini wameanza kazi kwa mkataba hospitali hapo wapewe ajira rasmi. Pia alisema amebaini upungufu wa madaktari bingwa uliopo katika hospitali hiyo.

Pia aliahidi kufuatilia maombi yao ya gari la wagonjwa hasa ikizingatiwa kuwa anayo maombi kama hayo kutoka hospitali za Mawenzi (Kilimanjaro), na Ligula (Mtwara).

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu aliwapongeza watumishi wa hospitali hiyo kwa huduma zao nzuri wanazotoa kwa wagonjwa. "Nineridhishwa na kauli walizotoa wagonjwa juu yenu. Tofauti na hospitali nyingine nilizopita, wao wamesema hawajatozwa fedha ili wapatiwe dawa. Nimefarijika sana."

RAIS DKT MAGUFULI AWAAPISHA WAKUU WA MIKOA LEO IKULU JIJINI DAR

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu kuwa mkuu wa mkoa wa Kagera,Hafla hiyo fupi ya kuwaapisha Wakuu hao wa Mikoa imefanyika leo Ikulu,jijini Dar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimuapisha Meja Jenerali Mstaafu Raphael Mugoya Muhuga kuwa mkuu wa mkoa wa Katavi,Hafla hiyo fupi ya kuwaapisha Wakuu hao wa Mikoa imefanyika leo Ikulu,jijini Dar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimwapisha Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Ikulu jijini Dar es salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimwapisha Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga kuwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimwapisha Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga kuwa Mkuu wa Mkoa wa Geita Ikulu jijini Dar es salaam leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimwapisha Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimwapisha Bw. Valentino Mlowola aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) leo Ikulu jijini Dar es salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimwapisha Bw. Alphayo Kidata kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Baadhi ya Wakuu wa Mikoa wakiimba wimbo wa Taifa kabala ya kuapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Ikulu jijini Dar es salaam.

Wakuu wa Mikoa wapya wa Tanzania Bara walioapishwa leo wakiwa katika picha ya pamoja Ikulu jijini Dar es salaam.

Wakuu wa Mikoa wapya walioapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakila kiapo cha kuzingatia maadili ya viongozi wa umma katika kutekeleza majukumu yao leo Ikulu jijini Dar es salaam.

Wakuu wa Mikoa wapya walioapishwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli wakisaini hati za viapo vya maadili ya viongozi wa umma mara baada ya kuapishwa leo Ikulu jijini Dar es salaam.Picha/Eleuteri Mangi na Aron Msigwa.

Na Jacquiline Mrisho- Dar es salaam.
Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewapa siku 15 Wakuu wa Mikoa kuwaondoa watumishi hewa walio katika orodha ya malipo ya mishahara ya watumishi wa umma katika Mikoa yao.

Rais Dkt. Magufuli amesema hayo leo Ikulu Jijini Dar es salaam baada ya kuwaapisha Wakuu wa Mikoa aliowateua Machi 13 mwaka huu ambapo amewaagiza washirikiane na Wakurugenzi wa Halmashauri kuwaondoa watumishi hewa.

“Nimewapa siku 15 kuanzia leo mkashirikiane na Wakurugenzi wa Halmashauri zenu kuwatoa wafanyakazi hewa, nikigundua kuwa bado kuna wafanyakazi hewa, Mkurugenzi husika atafukuzwa kazi na atapelekwa mahakamani”,
Na kusisitiza “Nimeamua kuwachagua nikiamini kwamba mtaniwakilisha vizuri katika Mikoa yenu, nawaomba mkatimize majukumu yenu bila kuogopa” alisema Dkt. Magufuli.

Aidha, Mhe. Dkt. Magufuli amesikitishwa na utafiti wa watumishi uliofanywa katika Mikoa ya Singida na Dodoma ambapo imegundulika watumishi 202 wanalipwa mishahara hewa.

Wakati wa utafiti huo, zaidi ya watumishi 26,900 walioko katika Halmashauri 14 za Mikoa hiyo, watumishi 3,320 hawakuwepo kazini kwa sababu mbalimbali.
Kwa mantiki hiyo, ukichukua utafiti huo wa Mikoa miwili ni dhahiri Serikali inapoteza mapato mengi kwa kulipa mishahara ya watumishi hewa nchi nzima.

Vivyo hivyo, Mhe. Dkt. Magufuli amewasisitiza Wakuu wote wa Mikoa wakasimamie ilani ya uchaguzi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kwakuwa waliahidi kutatua kero za wananchi na wahakikishe wanazitatua ili wananchi waishi vizuri kwa amani ndani ya nchi yao.

Naye Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amewataka Wakuu wa Mikoa na Wakurugenzi wa Majiji na Halmashauri zote nchini wajiandae kupokea na kuzipangia matumizi shilingi milioni 50 za kila Kijiji zilizoahidiwa wakati wa kampeni kwa lengo la kuboresha na kuimarisha shughuli za maendeleo.

KAMISHNA WA JESHI LA POLISI ZANZIBAR AZUNGUMZIA JUU YA MIRIPUKO INAYOTOKEA UNGUJA NA PEMBA.


Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame akizungumza na waandishi wa Habari kuhusu matokeo ya uripuaji wa mabomu na kuchoma moto nyumba na maskani za CCM Unguja na Pemba. Picha na Makame Mshenga/Maelezo Zanzibar.

Baadhi ya waandishi wa habari wakimsikiliza Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame leo Zanzibar.
Na Mwashungi Tahir na miza Kona - Maelezo Zanzibar 15/03/2016
NYUMBA ya Kamishna wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamdan Omar Makame imeripuliwa na kitu kinachosadikiwa kuwa ni bomu na watu wasiojulikana majira ya saa 5.00 usiku huko Kijichi nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari Ofisini kwake Makao Makuu ya Polisi Kilimani, Kamishna Hamdani amesema tukio hilo limeathiri sehemu ya paa la nyumba na dari na kujeruhi baadhi ya watu waliokuwa wamelala na kusababisha hasara kubwa.

Amesema tukio hilo linafanana lile lililotokea tarehe 03 mwezi huu katika Maskani ya CCM Kisonge Unguja hivyo polisi inaendelea kufanya uchunguzi ikiwa ni pamoja na kuwasaka wahalifu wanaofanya uhalifu huo.
Akizungumzia matukio mengine ya uhalifu na kuchoma moto nyumba, maskani na kituo cha Afya huko Pemba, alisema Jeshi la Polisi limeanza msako mkali na kuwatia mbaroni watu 31 ambao wanaendelea kuhojiwa na watakaohusika watafikishwa katika vyombo vya sheria.

WAZIRI MKUU MAJALIWA AMPA POLE PROFESA TIBAIJUKA-AWASILI NGARA.


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipewa kahawa iliyoyokaangwa maarufukwa jina la akamwani ikiwa ni mapokezi ya kimila ya Wahaya wakati alipokwenda nyumbani kwa Waziri wa Zamani wa Ardhi, Profesa Tibaijuka mjini Muleba kutoa pole kufuatia msiba wa mama yake mzazi, Aulelia Kajumulo Machi 15, 2016.


Waziri Mkuu, Kasim Majaliwa kiwasalimia wnanchi wa eneo la Benaco wilayani Ngara akiwa katika ziara ya mkoa wa Kagera Machi, 2016.

BILLIONI 12 ZAKUSANYWA KUTOKA KWA WAKWEPA KODI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akimwapisha Bw. Alphayo Kidata kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).


Na Raymond Mushumbusi- MAELEZO
15/3/2016. Dar es salaam.
Serikali kupitia Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imekusanya takribani Sh. billioni 12 kutoka kwa wafanyabiashara ambao walikwepa kodi na kupewa muda wa siku 14 na Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kulipa kodi hizo kwenye mamlaka hiyo.

Akitoa takwimu hizo mara baada ya kuapishwa kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Alphayo Kidata amesema, kila Mtanzania ana jukumu la kulipa kodi kwa mujibu wa sheria na sio kukwepa na amehaidi kulisimamia vizuri suala la ukusanyaji wa mapato katika sehemu mbalimbali ili kuongeza mapato ambayo yatasaidia kufanikisha maendeleo katika sekta mbalimbali.

“Tutajitahidi kwa kila namna kuwaelimisha wananchi wetu ili wafahamu wajibu wao na umuhimu katika kulipa kodi na sio kukwepa kulipa kodi na tunawaomba wananchi kila waendapo kupata huduma yoyote ile iwe katika sekta binafsi au Serikalini basi anatakiwa aombe stakabadhi za manunuzi au huduma ili tuweze kudhibiti upotevu wa kodi” alisema Kidata.

Kamishna aliongeza kwamba Kidata mamlaka hiyo ipo kwa ajili ya kuwahudumia wananchi na kama kuna suala lolote au tatizo kuhusu kodi kuna ofisi katika mikoa yote ikiwa ni hatua ya kutatua shida zao na kama kuna mtumishi yoyote wa mamlaka hiyo atashindwa kumuhudumia mwanachi inavyotakiwa basi taarifa zitolewa mara moja kupitia namba zao zilizoko kwenye tovuti ya mamlaka hiyo, ambayo ni www.tra.go.tz ili kuimarisha huduma zetu kwa wateja.

Aidha Kamishna Mkuu huyo amesema kuwa watawachukulia hatua wale wote ambao hawatalipa au hawajalipa kodi zao kwa kuwapeleka mahakamani kwa kukaidi kulipa kodi halali kwa mujibu wa Sheria.

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeanzishwa kwa mujibu wa Sheria na ina mamlaka ya usimamizi wa makusanyo ya Mapato Tanzania na kwa kipindi cha hivi karibuni kumekuwa na ukwepaji wa kodi uliotokana na sakata la upotevu wa makontena katika Bandari ya Dar es Salaam hivyo kuikosesha mapato Serikali lakini jitihada thabiti zimefanywa na mamlaka hiyo kukusanya madeni kutoka kwa wakwepa kodi na kuwafikisha mahakamani ambao wamekaidi kulipa.

WATAALAM WAJADILI MENEJIMENTI YA MAAFA KWA AJILI YA MAANDALIZI YA KIKAO CHA KAWAIDA CHA KAMATI YA TAIFA YA URATIBU WA MAAFA NCHINI (TANDREC)


Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brig.Jen, Mbazi Msuya akifuatilia hoja za wajumbe wa Kikao cha Wataalam kutoka Wizara, Idara na Taasisi za serikali (hawapo pichani), walipokutana kwa ajili ya maandalizi ya kikao cha Kamati ya Taifa ya Uratibu wa maafa nchini (TANDREC), tarehe 15 Machi, 2016, Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Idara ya Uratibu Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Brig.Jen, Mbazi Msuya akiwaongoza wajumbe kupitia makabrasha ya Kikao cha Wataalam kutoka Wizara, Idara na Taasisi za serikali walipokutana kwa ajili ya maandalizi ya kikao cha Kamati ya Taifa ya Uratibu wa maafa nchini (TANDREC), tarehe 15 Machi, 2016, Jijini Dar es Salaam.

Kaimu Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, ambaye pia niKamishna wa Operesheni, Rogatius Kipali akipitia makabrasha ya Kikao cha Wataalam kutoka Wizara, Idara na Taasisi za serikali walipokutana kwa ajili ya maandalizi ya kikao cha Kamati ya Taifa ya Uratibu wa maafa nchini (TANDREC), tarehe 15 Machi, 2016, Jijini Dar es Salaam..

Baadhi ya Wataalam kutoka Wizara, Idara na Taasisi za serikali wakipitia makabrasha ya kikao walipokutana kwa ajili ya maandalizi ya kikao cha Kamati ya Taifa ya Uratibu wa maafa nchini (TANDREC), Jijini Dar es Salaam, tarehe 15 Machi, 2016.