Friday 20 September 2013

SEMINA YA FURSA KWA VIJANA YAPOKELEWA KWA SHANGWE BUKOBA MJINI HII LEO.

Mdau wa michezo na mwanamichezo wa sports extra wa Clouds Fm (kushoto) Bw. Shaffih Dauda akiteta jambo na Mrisho Mpoto na (katikati) ni Ruge Mtahaba Mkurugenzi wa Vipindi,Uzalishaji na Mipango wa Clouds Group mapema na kabla ya semina kuanza kwenye ukumbi wa Lina's Club Bukoba mjini.
Mghani mahiri wa mashairi hapa nchini Mrisho Mpoto akizungumza kwa msisitizo,masuala ya fursa mbalimbali zinazopatikana katika suala la Ujasiliamali mapema mchana wa leo kwenye Ukumbi wa Lina's Night Club Bukoba Mjini.Semina hiyo iliyoandaliwa na Clouds Media Group,imefadhiriwa na shirika la NSSF;Zantel,MaxMalipo, Lake Oil.
Ruge Mtahaba Mkurugenzi wa Vipindi,Uzalishaji na Mipango wa Clouds Group akizungumza na Vijana waliojitokeza kwa wingi kwenye Ukumbi wa Lina's Club kuhusu swala zima la Fursa mbalimbali.Semina hiyo iliyoandaliwa na Clouds Media Group,imefadhiriwa na shirika la NSSF;Zantel,MaxMalipo, Lake Oil.

Bw. Willy O.Ruta wa Kiroyera Tours kushoto alikuwa mmoja wa wageni maalum waliokuwa kwenye meza kuu.

Baadhi ya wakazi wa Bukoba wakiwa kwenye semina ya Fursa ndani ya ukumbi Lina's  mapema leo, ambapo mada mbalimbali zimezungumzwa, ikiwemo mambo ya ujasiliamali kwa vijana, mikopo, akiba sambamba na namna ya kujiongezea thamani ya fursa unayoipata.Semina hiyo iliyoandaliwa na Clouds Media Group,imefadhiriwa na shirika la NSSF;Zantel,MaxMalipo, Lake Oil.

Baadhi ya wakazi wa Bukoba wakiwa kwenye semina ya Fursa ndani ya ukumbi Lina's  mapema leo, ambapo mada mbalimbali zimezungumzwa, ikiwemo mambo ya ujasiliamali kwa vijana, mikopo, akiba sambamba na namna ya kujiongezea thamani ya fursa unayoipata.



Baadhi ya wakazi wa Bukoba wakiwa kwenye semina ya Fursa ndani ya ukumbi Lina's  mapema leo, ambapo mada mbalimbali zimezungumzwa, ikiwemo mambo ya ujasiliamali kwa vijana, mikopo, akiba sambamba na namna ya kujiongezea thamani ya fursa unayoipata.

Baadhi ya wakazi wa Bukoba wakiwa kwenye semina ya Fursa ndani ya ukumbi Lina's  mapema leo, ambapo mada mbalimbali zimezungumzwa, ikiwemo mambo ya ujasiliamali kwa vijana, mikopo, akiba sambamba na namna ya kujiongezea thamani ya fursa unayoipata.kulia ni Bw. Mbonde nae alikuwepo mjini hapa Bukoba akizungumza kwa msisitizo,masuala ya fursa mbalimbali zinazopatikana katika suala la Ujasiliamali mapema mchana wa leo kwenye Ukumbi wa Lina's Night Club Bukoba Mjini.
Ruge Mtahaba Mkurugenzi wa Vipindi,Uzalishaji na Mipango wa Clouds Group kwenye meza kuu akisikiliza kwa makini hoja za mchangiaji
Bw. Mbonde kushoto akimpa mic mmoja wa vijana kuuliza swali kwa viongozi kuhusu swala zima la Semina ya Fursa kwa Vijana kwenye ukumbi wa Lina's mjini Bukoba.

Maswali yakiendelea kuulizwa

Shaffih Dauda ,akizungumza mbele ya washiriki wa Semina ya Fursa ndani ya ukumbi


Wadau mbalimbali walijitokeza kwa wingi kwenye Ukumbi wa lina's Night Club leo hii.





Baadhi ya wakazi wa Bukoba wakiwa kwenye semina ya Fursa ndani ya ukumbi Lina's  mapema leo, ambapo mada mbalimbali zimezungumzwa, ikiwemo mambo ya ujasiliamali kwa vijana, mikopo, akiba sambamba na namna ya kujiongezea thamani ya fursa unayoipata.
Mrisho Mpoto alikubalika zaidi baada ya kutoa hoja zake kuhusu swala zima la Fursa kwa vijana.

Mghani mahiri wa mashairi hapa nchini Mrisho Mpoto akipongezwa na Ruge Mtahaba Mkurugenzi wa Vipindi,Uzalishaji na Mipango wa Clouds Group baada ya kumaliza ungwe yake swala zima la Fursa kwa vijana.


Mghani mahiri wa mashairi hapa nchini Mrisho Mpoto na kulia ni Bw.Faustine Ruta  mwandishi wa mtandao wa www.bukobasports.com kwenye picha ya pamoja
Kushoto ni Mghani mahiri wa mashairi hapa nchini Mrisho Mpoto katikati ni Bw. Jamco Jamal Kalumuna wa blog ya Jamcobk na kulia ni Bw.Faustine Ruta  mwandishi wa mtandao wa www.bukobasports.com kwenye picha ya pamoja
Mdau wa michezo na mwanamichezo wa sports extra wa Clouds Fm (kushoto) Bw. Shaffih Dauda na kulia ni Bw.Faustine Ruta mwandishi wa mtandao wa www.bukobasports.com

Wednesday 18 September 2013

TFDA yakamata kilo 7,500 za samaki wabovu kutoka nje


Ofisa Uhusiano wa Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), Gaudensia Simwanza akizungumza na mmiliki wa Kampuni ya Sais Boutique iliyopo Tabata Bima, Dar es Salaam, Sadick Mapolo wakati maofisa wa TDFA walipofanya ukaguzi wa kushtukiza katika maghala ya kampuni hiyo na kubaini samaki wabovu kilo 7,500 aina ya vibua kutoka nje ya nchi waliokutwa wameharibika. 

  • Alisema walipofika katika eneo hilo walikuta makontena mawili, moja lilikuwa limejaa samaki ambao walionekana kuwa wazima huku lile lililokuwa nusu lilikuwa na samaki walioharibika kutokana na kutoa harufu na kuzingirwa na inzi.



Dar es Salaam. Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), imekamata kilo 7,500 za samaki aina ya vibua walioharibika ambao waliagizwa na Kampuni ya Sais Boutique kutoka China, Julai mwaka huu.
Taarifa ya kuwapo kwa samaki hao sokoni iliripotiwa na Gazeti la Mwananchi Jumapili, Jumapili iliyopita ikieleza kuwa walikuwa wakiuzwa kwa bei ya chini na wafanyabiashara wa Soko Kuu la Kimataifa la Feri, Dar es Salaam.
Akizungumza jana Tabata Bima, Dar es Salaam ambako samaki hao wamehifadhiwa, Ofisa Uhusiano wa TFDA, Gaudensia Simwanza alisema mamlaka hiyo ilianza kufanya uchunguzi baada ya kuona taarifa kwenye gazeti hili ikiwa ni pamoja na kwenda katika Soko la Feri ili kujua namna wanavyoingizwa nchini.
“Samaki hawa ni wabovu lakini walikuwa wanauzwa mitaani kwa bei ndogo na tulimkuta mmoja wa wasambazaji akiwa na maboksi 10 ya samaki walioharibika baada ya kumbana ndipo alituelekeza anapowanunua ikabidi tuje kwa ajili ya kuhakikisha na ndipo tukawakamata wahusika,” alisema Simwanza.
Alisema bei ya kawaida ya samaki aina ya vibua ni Sh30,000 mpaka Sh35,000 kwa boksi moja la kilo 10 lakini mfanyabiashara huyo alikuwa anawauza kwa Sh23,000.
Alisema walipofika katika eneo hilo walikuta makontena mawili, moja lilikuwa limejaa samaki ambao walionekana kuwa wazima huku lile lililokuwa nusu lilikuwa na samaki walioharibika kutokana na kutoa harufu na kuzingirwa na inzi.
Simwanza alisema Kampuni ya Sais Boutique ilipewa kibali cha kuingiza samaki Julai 8, mwaka huu na kwa mujibu wa taratibu za TFDA, kila mfanyabiashara mwenye kibali anapoingiza bidhaa anapaswa aipeleke ikaguliwe kabla ya kuiingiza sokoni ili kujiridhisha kama inafaa kwa matumizi ya binadamu.
Alisema kampuni hiyo ilikiuka taratibu hizo na kuanza kuuza samaki hao kabla hawajakaguliwa na kusema kwamba kufanya hivyo ni kosa kubwa.
Alisema kutokana na kosa hilo, mmiliki wa kampuni hiyo, Sadick Mapolo yuko chini ya ulinzi akisubiri kuchukuliwa hatua za kisheria kulingana na kosa alilofanya huku taratibu za kuteketeza bidhaa hiyo zikifanyika.
Alisema eneo ambalo linatumika kuhifadhia na kuuza samaki hao siyo rasmi kwani halikusajiliwa na TFDA.
“Hapo alipo ana kosa jingine kwani amehifadhi chakula hiki katika sehemu isiyo salama. Angalia kontena zilizowekwa samaki hawa zimezungukwa na gereji. Tulivyofika tulihisi kumehifadhiwa mizigo tu ya kawaida, hatukudhani kama kuna chakula,” alisema Simwanza.
Maofisa wa TFDA walichukua sampuli ya samaki aina ya Kolekole ambao wametokea Yemen waliopo katika kontena ambalo lilikuwa halijaanza kuuzwa lenye kilo 27,500 ili kuwapima.

BW AMOS RWEYEMAMU AWATAKA WAZAZI KUSAIDIANA NA SERIKALI KUWEKA MAZINGIRA MAZURI YA WATOTO KUSOMA,KATIKA MAHAFARI YA DARASA LA SABA SHULE YA MSINGI IGOMA IZIMBYA

 Bw Amos Rweyemamu ambae alikuwa ni mgeni rasmi katika mahafari ya darasa la saba shule ya msingi Igoma akiongea na wazazi na wageni waalikwa,amewataka wazazi kushirikiana na serikali kusaidia kuweka mazingira mazuri kwa wanafunzi waweze kusoma vizuri,bw amos baada ya kutembelea majengo ya shule na kujionea hali mbaya ya baadhi ya madarasa yakiwa yameharibika sakafu na watoto kusomea katika vumbi ,ameahadi kuvifanyia ukarabati vyumba hivyo haraka iwezekanavyo ili wanafunzi waweze kusoma katika mazingira mazuri,pia ameahidi kununua ngoma za bendi ambazo zimeharibika.bw Amos anaeishi nchini spain amesema wanao umoja wao huko spain wenye watu kama 200 unajinyima kidogo wanachokpata na kusaidia watoto wenye mahitaji,yatima na walioadhilika na virusi vya ukimwi,amewasihi watanzania kuwa na moyo wa kizalendo wa kusaidia wahitaji.

 hili ni mojawapo ya darasa ambalo limeharibika sakafu,ambalo wanafunzi wanalitumia na ni hatari kwa afya zao,bw amos amejitolea kukarabati,lakini jitokezeni na wengine kusaidia mahitaji ni makubwa sana shule imejengwa miaka zaidi ya 50 iliyopita.
                                      mgeni rasmi akionyeshwa hali halisi ya madarasa               
                         wanafunzi wakiingia katika ukumbi wa mahafari ya darasa lasaba
                                                                wazazi katika mapozz tofauti
                                           mgeni rasmi akisaini kitabu cha wageni
                                                                    waalimu katika pozzz
                                                       ni wahitimu 47 wakifurahia
                                                  chezeeaa darasa la tatu weweee
                                  watoto mahiri katika burudani ya taarabu wakiwaaga wenzao
                                          risara ya wahitimu ikakabidhiwa kwa mgeni rasm ili ijibiwe
                                         mgeni rasmi akapewa zawadi ya jogoo alienona
                                                   wahitimu katika miondoko ya kwaito...
 mwalimu mkuu wa shule ya igoma akiwasihi wahitimu kuwa watulivu na kuendelea na masomo ya pre form one wakisubiri matokeo yao
                                                            burudani kama kawaida
                    mmoja wapo ya wazazi wakiwa na mtoto wao aliehitimu darasa la saba