Saturday 30 August 2014

MTEMVU: CCM ITAUPUKUTISHA UPINZANI TEMEKE UCHAGUZI WA MITAA, SIYO KWA KUTUMIA NGUVU ILA MATUNDA YA UTEKELEZAJI ILANI



Na Bashir Nkoromo
Mbunge wa Temeke, Abbas Mtemvu ametamba kuwa, CCM itapukutisha kwa kishindo upinzani wote katika jimbo hilo kwa kushinda mitaa yote katika uchaguzi unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.

"Wala hatutatumia nguvu bali tutaichukua mitaa yote hata hiyo michache iliyopo sasa chini ya upinzani, kwa kutumia mtaji wa mafanikio makubwa tuliyoonyesha katika utekelezaji wa ilani ya CCM katika kipindi hiki", alisema Mtemvu.

Mtemvu alitoa tambo hizo wakati akihutubia mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Jumuia ya Wanawake Tanzania, Kata ya Azimio, kwenye Viwanja vya Shule ya Msingi Sokoine, katika Kata hiyo, Temeke jijini Dar es Salaam.

Alisema, CCM inao uhakika wa kutwaa viti vyote hadi kurejesha vichache vilivyopo sasa chini ya upinzani kwa kuwa mengi ambayo CCM iliahidi kupitia yeye wakati akiomba kuwa mbunge wa jimbo hilo katika uchaguzi mkuu uliopita yamefanyika.

Mtemvu alitaja baadhi ya yaliyotekelezwa kuwa ni pamoja na ujenzi wa barabara katika maeneo mbalimbali ambazo karibu zote zimeboreshwa kwa kujengwa kwa kiwngo cha lami tofauti na awali ambapo ilikuwa kero kubwa kwa kuwa zilikuwa hazipitiki kutokana na ubovu tena za vumbi.

"Zamani nilikuwa kila nikisimama jukwaani mnaniolea matatizo na kero lukuki hasa kuhusu hizi barabara, sasa leo hatuzungumzii matatizo ya barabara, tunazungumzia tu sasa kuboresha taa kwenye mitaa na barabara hizi", alisema Mtemvu.

Alisema, kuanzia mwezi huu Septemba, taa zote katika barabara na mitaa kwenye jimbo hilo zitawaka ambapo sasa zinafanyiwa maboresho ili zitumie nishati ya jua (solar) ili kupunguza changamoto ya gharama za malipo ya umeme wa taa hizo.

Mtemvu alisema, kukamilika kwa taa hizo itakuwa janga kwa vibaka ambao wamekuwa wakitumia fursa ya giza kujificha wakati wakivizia kuiba kwenye nyumba za watu na pia kukwapua wapitanjia nyakati za usiku.

Alisema mbali na kuboresha barabara CCM pia kupitia uongozi wake imeweza kuboresha hali za wananchi hasa kina mama na vijana kwa kuviwezesha vikundi vyao vya ujasiriamali kwa kuwakopesha fedha kwa ajili ya miradi mbalimbali ambapo sasa zaidi ya vikundi 100 vimenufaika.

Mtemvu aliahidi kuendelea kushirikiana na wabunge wengine wa Temeke na mkoa wa Dar es Salaam kwa jumla kuhakikisha watendaji wabovu serikalini wanakabwa koo ili wawajibike ipasavyo kutumikia wananchi.

Pia aliahidi kuhakikisha anaedelea kupigania kupatikana kwa mazingira bora ya kufanya kazi zao mamalishe na bodaboda kwa kuwa wana mchango mkubwa katika maendeleao ya jamii.

"Najua haiwezekani bodaboda zote zikaingia mjini, lakini tunachofanya ni kupigania kuhakikisha unakuwepo utaratibu mzuri utakaowezesha baadhi kufika mjini bila kuharibu taratibu na sheria zilizopo. Pia Mamalishe kwa kuwa lazima waendelee na shughuli zao tunawatafutia utaratibu bora kufanya shughuli zao kwa amani badala ya kukimzwa kimbizwa na mgambo kila mara", alisema Mtemvu.

Katika mkutano huo, uliosheheni burudani mbalimbali ikiwemo msanii Omari Tego kuimba wimbo maalum wa CCM ambao ulikonga nyoyo za waliohudhuria, Mtemvu aligawa kadi kwa wanachama wapya 45 wa UWT.

HABARI KATIKA PICHA KUHUSU MKUTANO HUO
Mbunge wa Temeke, Abbas  Mtemvu akihutubia mkutano wa hadhara uliofabyika kwenye Uwanja wa shule ya Sokoine, Temeke jijini Dar es Salaam, jana, Agosti 30, 2014.
Mtemvu akishangiliwa wakati akihutubia mkutano huo wa hadhara
Mbunge wa Temeke Abbas Mtemvu akimpa kadi ya Uanachama wa UWT Maridha Rajabu wakati wa mkutano huo, wanachama wapya 45 wa jumuia hiyo walipewa kadi
Mbunge wa temeke,  Mtemvu akimtuza msanii Omari Tego baada ya kukunwa na msanii huo kwa kuimba wimbo maalum wa CCM wakati wa mkutano huo
Mbunge wa temeke,  Mtemvu akimpongeza baada ya kumtuza msanii Omari Tego baada ya kukunwa na msanii huo kwa kuimba wimbo maalum wa CCM wakati wa mkutano huo
Umati wa wananchi ukiwa umefurika wakati wa mkutano huo
Mwenyekiti wa UWT Kata ya Azimio, Tatu Hassan akifungua mkutano huo, kwenye Uwanja wa Sokoine Temeke kabla ya kuhutubiwa na Mtemvu
Diwani wa Kata ya Azimio, Hamisi Mzuzuri akieleza utekelezaji wa ilani ya CCM katika kata hiyo wakati wa mkutano huo
Ofisa Kutoka Makao Makuu ya CCM, Idara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Gifti Isaya akipata picha kupitia simu yake kwenye mkutano huo
Waalikwa wakiwa kwenye mkutano huo. Wapili walioketi kulia ni Ofisa katika Idara ya Mambo ya Nje Makao Makuu ya CCM,  Gift Isaya akifuatilia kwa makini pamoja na wenzake
Msanii Yusuf Peter wa Kikundi cha hamasa Temeke, akionyesha vimbwanga vyake mbele ya mke wa Mbunge wa Temeke  Mama Mtemvu (kulia)
Msanii Ahmadi Juma wa kikundi cha hamasa Temeke, akionyesha uhodari wa 'kula' moto wakati kikundi hicho kikitoa burudani wakati wa mkutano huo
Mtemvu akiwatuza wasanii waliotia fora uwanjani wakati wa mkutano huo.

Friday 29 August 2014

VICTOR ALCARD MWOMBEKI AFANYIWA SHEREHE BABU KUBWA NYUMBANI KWAO(BAG PARTY) NA WANA KASTAMU NA BAKOBA KABLA YA NDOA YAKE ITAKAYOFUNGWA 13-9-2014

 Ni bwana harusi mtarajiwa Victor akiwa na mama yake mzazi Ma Vediana Fredrick anatarajia kufunga pingu za maisha 13-9-2014,Wana Kastamu wakishirikiana na mama mzazi wa victor ndugu na jamaa waliandaa sherehe ya kumkaribisha na kumpongeza Victor kabla ya ndoa yake takatifu na Bi Lyidia Kashubi Protas.
 Mambo yalikuwa mazito walidondoka ng'ombe wawili kwa ajili ya Vctor na waalikwa wote
 Mandalizi yakiendelea
 Uwezi amini kama hapo ni migombani ni kampuni ya Walkgard hotel chini ya mkurugenzi Mama Matungwa ndio alipamba eneo  na kubadilika
 Kulia ni Mh Diwani Bigambo ni miongoni mwa wageni waliokuwepo
 Bw Bushira nae alikuwepo
 Eneo la migombani lilibadilishwa na kuonekana hivi ,pande za Kastamu Bukoba mjini
 Wamama wa Kastamu walitokelezea
 Mapema Victor akiwasili kutoka uwanja wa ndege  wa Bukoba akitokea Dar kuja kwenye shughuli yake ,na Coster imeleta marafiki wa victor kutoka Dar
 Wageni kutoka Dar wakishuka kwenye gari
 Shangwe zikatawala
 Mama Matungwa mpambaji akimpokea victor alipowasiri Kastamu
 Ndugu na jamaa wakimpokea
 Kulia Mama mzazi wa victor akija kumpokea mwanae
 Karibu nyumbani mwanangu
 Watu wakajitoa fahamu
 Marafiki walioambatana na victor
 Eneo rasmi aliloandaliwa Victor
 Victor akiwa na rafiki yake kipenzi
 Mkurugenzi wa jamco video production na Blog hii akiteta jambo na Victor
 Watu wakacheza ngoma
 Mama mlezi wa victor wa Dar mama Kafanabo akitambulisha watu waliotoka Dar
 Kundi la Ngoma la Rugoloire likamfurahisha Vctor
 Hapana chezea victor katika ngoma
 Kwaya YABUNENA NAO WAKATUMBUIZA
Wakati wa chakula
 Mh Diwani Bigambo akitoa neno
 Umati mkubwa wa wageni waalikwa
 Wamama wa uwaka wakicheza ngoma
 Toina kumubona Victor
 Wamama wa uwaka wakimpa zawadi victor
 Nani kama mama
 Akaingia diamond wa Bukoba Nshomile Family watu wakapagawa
 Mistari ya nshomile ikamwamsha victor na kumwagia noti za kutosha
 Hapana chezee Nshomile
 Ashiraf rafiki wa victor akiteta jambo
 Mambo ya samaki wa foil
 Nyama choma
 Ni migombani huwezi aminiiiii
 Cheza ngoma
 Maisha yakiendelea
Hakika wahaya wanamsemo(Oburanura bubanza ne nan'ga) kama mabo yamekuwa hivi sherehe ya nyumbani,  siku ya ndoa 13-9-2014 itakuaje, mimi na wewe hatujui tusubiri.jamcobukoba.blogspot.com tunawatakia maandalizi mema.