Saturday 10 August 2013

TETESI: SHEIKH PONDA KUPIGWA RISASI ZA BEGA MJINI MOROGORO LEO

Saturday, August 10, 2013


MUDA MCHACHE uliopita mjini Morogoro sheikh Ponda Issa Ponda amepigwa risasi na polisi .
Inasemekana pengine umauti umemkuta .

Dhahama hiyo imempata baada ya kushuka kwenye tax ambako kulikuwa leo

akiendesha mhadhala baada ya mhadhala huo kukawa kama kuna maandamano
kueleke barabarani, gafla polisi walitokea na kuanzanza kutawanya wakati huo yeye
alikuwa hayupo .

Ndipo mda mdogo akawasili akashuka na ndipo akapigwa risasi za kutosha.


Haijulikani hali yake. RPC, Faustine Shilogile, anasema hali ni shwari ila Ponda hajui hali yake Maana polisi walizuia gari la Ponda wamkamate, lakini wananchi wakaanza kushambulia polisi ndipo wakarusha risasi hewani kutawanya watu, lakini wananchi wakamtorosha. Anasema taarifa ni nyingi za uongo, hakuna watu polisi wala hospitali waliozingira na anaomba anayejua alipo atoe taarifa.

RAIS KIKWETE AKUTANA NA WAZIRI WA UCHUMI BIASHARA NA VIWANDA WA JAPAN

Saturday, August 10, 2013

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na  Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa Japan, Mheshimiwa Toshimistu Motegi alipokutana na kufanya mazungumzo naye  Ikulu, Dar Es Salaam
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na  Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa Japan, Mheshimiwa Toshimistu Motegi alipokutana na kufanya mazungumzo naye  Ikulu, Dar Es Salaam
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete akimsindikiza   Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa Japan, Mheshimiwa Toshimistu Motegi baada ya kukutana na kufanya mazungumzo naye  Ikulu, Dar Es Salaam, leo Agosti 10, 2013
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete katika picha ya pamoja na Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa Japan, Mheshimiwa Toshimistu Motegi (wa tatu kushoto, mbele)  na ujumbe wake pamoja na Waziri wa Uchukuzi  Dkt.  Harrison Mwakyembe (wa kwanza kulia),  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwezeshaji na Uwekezaji Dr Mary Nagu (wa pili kulia), Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt Abdallah Kigoda (wa pili kushoto), Balozi wa Tanzania nchini Japan Mhe Salome  Sijaona  (wa kwanza kushoto) alipokutana na kufanya mazungumzo naye  Ikulu, Dar Es Salaam,





TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
.                                  Japan yatangaza sera mpya kwa Tanzania
·         Sasa Tanzania kuwa nchi lengwa ya Japan
·         Japan itasaidia Tanzania kuwa kitovu cha uwekezaji katika Afrika
·         Kushiriki maboresho Reli ya Kati
·         Kusaidia kupanua na kuboresha Bandari ya Dar Es Salaam
·         Viwanda vya Japan kujengwa nchini kikiwemo cha kutengeneza pikipiki za Honda 
·         Ni matokeo ya Ziara ya Rais Kikwete Japan
JAPAN imeamua kuanzisha ushirikiano mkubwa zaidi na Tanzania ambako nchi hiyo itaifanya Tanzania kuwa nchi lengwa ya Japan na kuiwezesha kuwa kitovu cha biashara na uwekezaji katika Afrika kwa nia ya kuiwezesha kuwa na uchumi ulioimarika na wenye kuzalisha ajira nyingi kwa wananchi.
Uamuzi huo wa Japan ni matunda ya mazungumzo kati ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na Waziri Mkuu wa Japan, Mheshimiwa Shinzo Abe yaliyofanyika Tokyo, Japan wakati Rais Kikwete alipotembelea nchi hiyo Juni, mwaka huu, 2013.
Uamuzi na msimamo mpya wa Japan umetangazwa rasmi leo, Jumamosi, Agosti 10, 2013 na Waziri wa Uchumi, Biashara na Viwanda wa nchi hiyo, Mheshimiwa Toshimistu Motegi alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Kikwete, Ikulu, Dar Es Salaam.
Kwa upande wa Tanzania, mazungumzo hayo yamehudhuriwa pia na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anashughulika na Uwekezaji na Uwezeshaji  Mheshimiwa Mary Nagu, Waziri wa Viwanda na Biashara Mheshimiwa Dkt. Abdallah Kigoda na Waziri wa Uchukuzi Mheshimiwa Dkt. Harrison Mwakyembe.
Waziri Motegi amemwambia Rais Kikwete kuwa ametumwa na Waziri Mkuu Abe kufuatilia mazungumzo kati yao na kutangaza rasmi kuwa Japan imeiteua Tanzania kuwa nchi lengwa na kitovu cha uwekezaji wa Japan katika Afrika Mashariki na katika Afrika kwa jumla.
Waziri Motegi pia amemwambia Rais Kikwete kuwa pia amekuja Tanzania kutoa taarifa kuwa Japan iko tayari kushiriki katika kuboresha na kuifanya ya kisasa zaidi Reli ya Kati kwa kujenga njia ya kimataifa badala ya njia nyembamba ya sasa. Amesema kuwa Japan itatuma wataalam wake kuangalia jinsi gani ya kuanza kazi hiyo ya uboreshaji wa Reli hiyo.
Aidha, Mheshimiwa Motegi ametangaza kuwa Japan itashiriki katika upanuzi na uboreshaji wa Bandari ya Dar Es Salaam kwa kuifanya ya kisasa zaidi.
Waziri Motegi amesema kuwa katika azma ya Japan ya kuifanya Tanzania nchi ya mfano katika Afrika katika uwekezaji na uchumi ulioimarisha, amekuja na kundi la wafanya biashara wa Japan ambao wanaendelea kufanya mazungumzo na wafanyabiashara wa Tanzania kuona jinsi gani wanavyoweza kusaidiana katika kuwekeza katika uchumi wa Tanzania.
                        Waziri pia amesema kuwa moja ya malengo ya uamuzi huo wa Japan ni kuhakikisha kuwa bidhaa ambazo kwa sasa zinanunuliwa moja kwa moja kutoka Japan zitazalishwa hapa nchini katika viwanda ambavyo vitajengwa na makampuni ya Japan.
Kwa kuanzia amesema kuwa makampuni mawili ya Honda na Panasonic yamekubali kujenga viwanda nchini kimoja kwa ajili ya kutengeneza pikipiki za Honda hapa hapa nchini na kingine kwa ajili ya kutengeneza vifaa vya umeme.
“Huu ni mwanzo tu Mheshimiwa Rais kwa sababu kama nilivyosema kuwa tunataka Tanzania kuwa nchi mfano ya uwekezaji wa Japan  katika eneo hili la dunia na namna hiyo kwa pamoja tutakuwa tumeshirikiana katika kuongeza ajira kwa wananchi wa Tanzania,” Mheshimiwa Motegi amemwambia Rais Kikwete.
Waziri huyo pia amesema kuwa baadhi ya makampuni ya Japan yana mipango ya kuwekeza katika kilimo, na hasa kilimo cha pamba, na kuanzisha viwanda vya nguo hapa hapa nchini.
Wakati wa mazungumzo yao mjini Tokyo, Rais Kikwete alimtaka Waziri Mkuu Abe kuwekeza zaidi katika Afrika akisisitiza kuwa Japan ni moja ya mataifa makubwa duniani ambayo yamefanikiwa kupata soko kubwa katika Afrika na hasa soko la magari.
Uamuzi huo wa Japan na ziara ya Mheshimiwa Motegi inakuja wiki na miezi michache baada ya Tanzania kuwa imepokea viongozi wa mataifa mengi yakiwemo mataifa makubwa ya Marekani na China na inathibitisha ni kiasi gani siasa na sera za Tanzania zinavyokubalika duniani.
Ends 
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
10 Agosti, 2013

BINGWA MTETEZI KAGASHEKI CUP BAKOBA YATOLEWA HATUA YA ROBO FAINALI NA RWAMISHENYE KWA MATUTA BAADA YA DAKIKA 90 KWISHA

 Mwenyekiti wa bakoba Ernest nyambo akiwa aamini macho yake kilichotokea katika uwanja wa kaitaba baada ya timu ya bakoba mwanzo mwisho kuondolewa leo kwa mikwaju ya penati 5kwa 6
 kabla ya mechi kuanza ulizuka mtafaruku wa mashabiki wa bakoba na rwamishenye kuweka bendera za timu zao sehemu moja,kitu kilichosababisha ngumi kupinwa na shabiki mmoja wa rwamishenye kujeruiwa
                                      wachezaji wa rwamishenye wakipasha kabla ya mpambano
                                                                   waamuzi wa leo
                                       mshabiki wa rwamishenye akiwa amejeruiwa
                          bwana haridi akiwa hajui nani  kampa kipigo,akimtafuta alimjerui na polisi
                                                         mechi ilikuwa ngumu kwa pande zote
                                      kocha wa rwamishenye akiwa anafuatilia mtanange
                                                                    wakati wa penati ukafika

                                                       penati iliyomuondoa bakoba
                            kipa wa rwamishenye akiwa kabebwa baada ya kudaka penati ya sita ya bakoba

                                                                    rwamishenye oyeeeee
                                      mwenzako akinyolewa ,unatia maji,kesho kashai na kagondo

                                                      viongozi wa miembeni wakitathimini mchezo
               mkurugenzi wa manispaa shabiki nguri wa simba akimtania jamco kuwa jezi walizovaa bakoba ndio zimewaponza kuwa ni za yanga

                                     umati mkubwa wa watu wakitoka katika uwanja wa kaitaba

SIKUKUU YA EID ILIVYOSHEREKEWA MAENEO TOFAUTI BUKOBA MJINI,FUKWE ZOTE ZAJAA WATU

 khadija jamal,jamiru jamal na Ashira jamal muda mfupi wakiwa nyumbani kabla ya mtoko wa eid
                                           watu wazima, watoto kila mmoja kivyake
  nitoke vipi,mtoto ABDARAH Nuwah akivinjari maeneo ya ufukwe na baiskeli yake
                                 kila mmoja alivyojisikia kutoka,pande za ufukwe wa bukoba club darajani
                                                               pande za ufukwe wa kiroyera
                     watoto wakibembea ufukwe wa kiroyera, wanapouza samaki palikuwa hapatoshi
                                                 watoto wakiogerea ufukwe wa kiroyera
                                                           ufukwe wa space na yasira
                               walinzi wa amani muda wote walikuwa makini
                                                              watoto wakinunua maeple
                                                         ni full shangwe kila mahala
                                                                            kifamilia zaidi
                                            na sie tupige jamco..., nikawapiga wananijua siwajui, wakafurahi
                                              barabara ya bukoba club ilikuwa busy muda wote
                          pande za walkgard hotel kashura,na mh diwani nilikuta anachomoka na familia
                                                   watoto wakiwa walkgard hotel wanabembea
                                                 nikakutana na ndugu chama na familia walkgard hotel
                                                          watoto wakiogerea walkgard hotel
                                                                wanaweza watoto
                                               watu wanasherekea eid walkgard hotel

                                                   dada rose kajilita na wanae wakiwa walkgard hotel wakisherekea eid
                                                                 mama na mwana usipime, full shangwe