Saturday 12 April 2014

CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU MKOA WA KAGERA CHAFANYA MKUTANO MKUU WA KAWAIDA, JAMAL MALINZI ASEMA ATAENDELEA KUWA MWENYEKITI WA KRFA

 Chama cha mpira wa miguu Mkoa wa Kagera (KRFA) kimefanya mkutano mkuu wa kawaida kwenye ukumbi wa mkuu wa mkoa wa Kagera na mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa wilaya ya Missenye Kanal Issa Njiku. Awali akisoma taarifa yake mwenyekiti wa KRFA ambae pia ni Rais wa TFF Jamal Emil Malinzi aliwashukuru wajumbe wote wa mkutano mkuu kwa namna walivyoshiriki kwa namna tofauti katika kuendeleza michezo katika wilaya zote za Mkoa wa Kagera,Hotuba iliyosheheni mipango kedekede ya kuinua soka kwa ujumla  nchini Tanzania na Kagera ikiwemo.Katika mambo mengi aliyoeleza  ameweza kueleza changamoto nyingi zinazoikabiri KRFA na kuwataka viongozi kuhakikisha wanawasiliana na Halimashauri za wilaya zao kutenga maeneo ya viwanja vya michezo,akiongelea uwanja wa Kaitaba amesema anayofuraha kuwajulisha wajumbe kuwa sasa uwanja huo unawekewa nyasi bandia kwa ufadhili wa FIFA kwa asilimia mia moja,lakini pia amehaidi kuitisha harambee ya wadau mbalimbali jijini Dar es salam kwa ajili ya kupata pesa ya kujenga jukwaa moja  katika uwanja wa Kaitaba Bukoba.Pia aliweza kuelezea kuhusiana na nafasi ya uenyekiti wa KRFA, Amesema tangu amepata nafasi ya Rais TFF amekuwa akikutana na maswali mengi ya waandishi wa habari na wadau kuhusiana na kujiuzuru nafasi hiyo,( Wakati nakuja Bukoba nilikuwa na wazo ili la kujiuzuru ,lakini  kila mjumbe aliesimama hapa ameniomba nisijiuzuru mpaka wengine kutamka kuwa iwapo nitajiuzuru basi nao watajiuzuru nafasi hii,lakini kuna mjumbe kasema wapo watu wakati wa kampeni walikuwa wakisema natafuta nafasi hii ili niweze kugombea urais, kwahiyo basi naomba nitamke kuwa sitojiuzuru nitaendelea kuwa mwenyekiti wa KRFA.)
 Katibu wa KRFA Salumu  Chama akiongea na wajumbe
 Bw Pelegrius Rutayuga akisoma agenda za mkutano
 Mweka Hazina wa KRFA
 Mgeni rasmi Kanal Mstaaf Issa Njiku Mkuu wa Wilaya ya Missenye akifungua mkutano
 Wajumbe
 Bw Didas Zimbile mjumbe
 Bw Kazinja Mjumbe
 Mabrogger

 Makamu mwenyekiti wa KRFA
 Mkurugenzi wa sheria TFF Evodius Mtawala akifafanua vipengere mbalimbali katika marekebisho ya Katiba ya KRFA
Ukafika wakati wa


Katibu wa KRFA Salumu Chama akiwa na Mwenyekiti wa BUFA Marick Tibabimare

Thursday 10 April 2014

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MPIRA KAGERA AWASILI BUKOBA ,TAYARI KWA VIKAO VYA KIKATIBA

 Rais wa TFF ambae pia ni Mwenyekiti  wa chama cha soka Mkoa wa Kagera KRFA Jamal Emil Malinzi amewasili leo Bukoba katika uwanja wa ndege majira ya saa nne asubuhi na kupokelewa na viongozi mbalimbali wa soka Mkoa, wadau na wapenzi. Atakapokuwa hapa mkoani atahudhulia kikao cha kamati tendaji ya KRFA kitakachofanyika leo na badae ataendesha na kusimamia mkutano mkuu wa kawaida wa KRFA, Lakini pia atapata fursa ya kukutana na viongozi wa serikali  ngazi ya Mkoa na Manispaa kuzungumza nao kuhusiana na maswala ya kimichezo.Rais wa TFF Jamal Malinzi akisaini kitabu cha wageni chumba cha mapokezi VIP Bukoba
 Akipokelewa na viongozi wa soka
 Mwandishi wa habari Audax Mtiganzi akiongea na  Bw Jamal Malinzi
 Rais wa TFF Jamal Malinzi akiwa na mshauri wa ufundi TFF bw Pelegrinius Rutayuga
 Al amin A bdul akimsalimia kwa bashasha Rais wa TFF
 Karibu sana mkuu,nitafurahi ukinikabidhi mikoba, ni maneno aliyoyatamka tukiwa hapo, sasa sijui ni mikoba ipi, mimi na wewe hatujui...

 Akaomba picha ya kumbukumbu
 Wakateta.....
 Akawasili Wily Kiroyera  wakasalimiana, angalia picha vizuri, kila mtu mawazo yakiwa tofauti
 Wily Kiroyera akisalimiana na Rais wa TFF
 akisalimiana na Katibu wa KRFA Salumu Chama
 Yakapita maneno ya utani......
 Mmiliki wa jamcobukoba.blogspot.com Jamal Kalumuna akiwa na Rais wa TFF, Hutaniana wajina
 Mdau Ruge Masabara,
 Mmiliki wa Bukobasports.blog Faustini Ruta akiwa na Rais TFF
 Msafara ulielekea Vctorius peach Hotel
 Didas Ziimbile akisalimiana na Rais wa TFF
 Al amin akiwa na Evodiua Mtawala alieambatana na Rais
 Hii ni picha itaingia kwenye Historia ya soka Kagera hivi karibuni




 Wadau mbalimbali wakiwa uwanja wa ndege Bukoba

Wapenzi wa soka wakiwa uwanja wa ndege