Wednesday 9 April 2014

MWENYEKITI WA CHAMA CHA MPIRA WA MIGUU MKOA WA KAGERA KUWASILI KESHO 10-4-2014 ,AMBAE PIA NI RAIS WA TFF JAMAL MALINZI

 Mwenyekiti wa chama cha mpira wa miguu Mkoa wa Kagera(KRFA) Jamal Malinzi atawasili  siku ya Alhamis 10-4-2014 majira ya saa nne asubuhi katika uwanja wa ndege wa Bukoba.Kwa mujibu wa Katibu wa KRFA Salumu Umande Chama amewataka na kuwaomba wapenzi wa soka mkoa wa kagera kujitokeza kwa wingi uwanja wa ndege kumpokea mwenyekiti wao kwani tangu achaguliwe kuwa Rais wa TFF alikuwa hajabahatika kurudi nyumbani,Bw Jamal Malinzi atakapokuwa mkoani atahudhulia kikao cha kamati tendaji ya KRFA na siku inayofuata utakuwepo mkutano mkuu wa KRFA.
 Bw Salumu Chama Katibu wa KRFA
 Bw Pelegrinius .A. Rutayuga mjumbe wa kamati tendaji ya KRFA , Mjumbe wa mkutano mkuu wa TFF  na Mshauri Mkuu wa Kiufundi TFF makao makuu, nae yuko tayari Bukoba kuudhuria kikao cha kamati tendaji na mkutano mkuu wa KRFA
 Mmiliki wa Bukobasports.blog akiongea mawili matatu ya kimichezo na Bw Rutayuga
 Mmiliki wa jamcobukoba.blogspot.com akiwa na Bw Rutayuga ambae aliweza kuongelea mambo mengi ya kimechezo na kati ya mengi alisema ndoto yao kubwa ni kuweka mikakati popote Tanzania bila kujarieneo au mkoa mpira uchezwe,ukue na kupata vijana wenye uwezo wa kukuza soka la Tanzania ,kuachana na mazoea au ukariri wa fulani ndio anaweza wakati vipaji viko kila mahala Tanzania.


Kila rakheri katika mapambano ya kukuza soka Tanzania

No comments:

Post a Comment