Saturday 16 May 2015

BALOZI KAGASHEKI ATIMIZA OMBI LA MWENYEKITI WA MTAA WA CHADEMA.

 Mbunge wa jimbo la Bukoba Mjini Balozi Khamis Sued Kagasheki ametimiza ombi la mwenyekiti wa mtaa wa chadema kata ya kitendaguro Bwana Mweyunge Paulo Erasto,Katika nkutano wa hadhara wa Mbunge katika kata ya kitendagoro ,Bw Mweyunge alisimama akamuomba mbunge asaidie kuwapatia tochi,filimbi na betri kwa ajili ya kusaidia katika zoezi la ulinzi shirikishi katika kata hiyo kutokana matukio ya uharifu yaliyokuwa wamejitokeza kwa kasi kubwa katika kata ya Kitendaguro na Kibeta,Bw Mweyunge alimueleza mh Kagasheki kuwa pamoja na jeshi la polisi kujitahidi kupambana na waharifu, lakini pia wao katika mitaa saba ya kata Kitendaguro wananchi wameweka utaratibu wa kuzunguka usiku kucha kuhakikisha usalama wa wananchi unakuwepo.(Katika picha msaidizi wa Mbunge Bw Jumanne Bingwa akikabidhi vifaa kwa niaba ya Mbunge Kagasheki)
 Viongozi wa Kata Kitendaguro wakipokea vifaa.

 Mtendaji wa Kata ya Kitendaguro Bi Mary (gauni la njano) akipokea vifaa.
 Ofisi ya Kata .
Endelea kuangalia jamcobukoba.blogspot.com

Thursday 14 May 2015

MKAPA AWATAKA WAKANDARASI NCHINI KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA WELEDI.


RAis mstaafu wa awamu ya tatu Mhe. Benjamin Mkapa akifungua Mkutano wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wakandarasi leo jijini Dar es salaam

Rais mstaafu wa awamu ya Pili Mhe.Benjamin Mkapa akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Usajili wa Wakandarasi (CRB).

Rais mstaafu,Benjamin Mkapa akiwa katika picha ya pamoja na wawakilishi/wakandarasi waliofanya vizuri na kupewa zawadi mbalimbali na vyeti na Bodi ya Wasajili wa Wakandarasi (CRB).

Baadhi ya Wahandisi waliohudhuria mkutano huo wakiapishwa leo jijini Dar es Salaam.

Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia masuala mbalimbali. Picha/Aron Msigwa -MAELEZO.

Na.Aron Msigwa -MAELEZO.
14/5/2015.Dare es salaam.
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Mhe.Benjamin Mkapa amewataka Wakandarasi kote nchini kufanya kazi zao kwa weledi na kuzingatia sheria, kanuni na taratibu zinazosimamia Sekta ujenzi ili miradi wanayoisimamia na kuitekeleza iweze kuwa na manufaa kwa taifa.

WAZIRI WA AFYA AIPONGEZA MUHIMBILI KUFANIKISHA MATIBABU YA MOYO KWA WATANZANIA

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Mh. Dkt. Seif Rashid ameipongeza Hospitali ya Taifa Muhimbili kupitia Idara yake ya Tiba na Upasuaji Moyo kwa kufanikisha matibabu ya moyo kwa wagonjwa 24 katika kipindi cha siku nne.
Hayo ameyasema alipotembelea Hospitali hiyo kuona namna ambavyo wataalam wetu kwa kushirikiana na madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Prince Sultan Cardiac Centre iliyoko Riyadhi nchini Saudi Arabia ambao wamekuwepo Muhimbili toka tarehe 9 Mei na wanatarajiwa kuondoka tarehe16 Mei, mwaka huu.
Dkt. Rashid amesema ni mfanikio makubwa sana ambayo tumefikiwa hadi hivi sasa katika upasuaji moyo na tunatarajia kasi hii ya ushirikiano ikiendelea tutapunguza kwa kasi sana wagonjwa wanaopelekwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu.

“Kama ndani ya siku nne tu mmeweza kuziba matundu ya moyo kwa watoto 12 bila kufungua kifua na mkaweza kufungua vifua vya watoto wengine 12 ambao kutokana na hali zao walihitaji kufunguliwa vifua, mmenipa moyo sana kwamba mmejidhatiti kuhakikisha Watanzania wanapata huduma hii kwa haraka na kwa ufanisi wa hali ya juu, nawapongezeni sana” amesema Dkt. Rashid.


Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid akiwa na mtoto ambaye anasubiri kufanyiwa uchunguzi wa kina kama anahitaji upasuaji wa moyo au la.

mtoto Catherine Gwabala (6) alikuwa wodini jumamosi iliyopita akisubiri kufanyiwa upasuaji.

Mh. Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid akimjulia hali leo baada ya kufanyiwa upasuaji. Kushoto kwake ni mama Catherine akifurahia baada ya mtoto wake kufanyiwa upasuaji.

Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dkt. Seif Rashid ambapo kulia kwake ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Dkt. Hussein Kidanto wakiwa ndani ya Chumba chenye mtambo wa Cath Lab ambao unatumika kuzibua mishipa ya damu inayopeleka damu kwenye moyo iliyoziba na pia mtambo huu pamoja na mambo mengine umetumika kwa mara ya kwanza kuziba matundu ya moyo bila kufungua kifua. Mtoto huyu ambaye jina lake limehifadhiwa anasubiri kuzibwa tundu kwenye moyo wake kwa kutumia mtambo wa Cath Lab. Ndani ya siku tatu ataruhusiwa kwenda nyumbani.

Hapa ni ndani ya chumba chenye vifaa vya kisasa kabisa kwa ajili ya wagonjwa wenye kuhitaji uangalizi maalumu (ICU) ambapo mtoto aliyefanyiwa upasuaji anaangaliwa.

Jopo la wataalam wakiwa ndani ya chumba cha kisasa cha upasuaji moyo wakiendelea na upasuaji moyo.

Jopo la Watalaam wakifurahi baada ya kumaliza upasuaji kwa ufanisi na mgonjwa kupelekwa chumba maalumu (ICU).

Mtoto Cherish Chatama akifurahi baada kusalimiwa na Mh. Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid ambapo pembeni yake ni mama Cherish

Mtoto Michelle Colila (5) akifurahi baada kusalimiwa na Mh. Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Seif Rashid ambapo pembeni yake ni mama Michelle.

MTOTO WA BABA WA TAIFA JOHN GUIDO NYERERE AZIKWA LEO BUTIAMA


Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma Mhashamu Michael Msonganzila akisali mbele ya jeneza la marehemu John Guido Nyerere kabla halijaingia kanisani kwa ajili ya ibada maalum iliyofanyika kwenye Kanisa Katoliki la Bikira Maria wa Damu Azizi ya Yesu Jimbo la Musoma Parokia ya Butiama.

Viongozi na wananchi wakishiriki ibada ya kumuombea marehemu John Gaudo Nyerere katika Kanisa Katoliki la Bikira Maria wa Damu Azizi ya Yesu Jimbo la Musoma Parokia ya Butiama

Askofu wa Kanisa Katoliki Jimbo la Musoma Mhashamu Michael Msonganzila akitoa heshima za mwisho kwa marehemu John Guido Nyerere baada ya kukamilika kwa ibada maalum iliyofanyika kwenye Kanisa Katoliki la Bikira Maria wa Damu Azizi ya Yesu Jimbo la Musoma Parokia ya Butiama.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi CCM Taifa Nape Nnauye akizungumza na Mbunge wa Jimbo la Monduli na Waziri Mkuu Mstaafu Ndugu Edward Lowassa wakati wa mazishi ya John Guido Nyerere yaliyofanyika nyumbani kwa Baba wa Taifa ,Butiama.

Jeneza lenye mwili wa marehemu John Guido Nyerere likiteremshwa kaburini na Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Mama Maria Nyerere akiweka udongo kwenye kaburi la mtoto wake John Guido Nyerere.

Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Asha-Rose Migiro akiweka udongo kwenye kaburi la John Guido Nyerere.

Mtoto wa mwisho wa marehemu John Guido Nyerere anayefahamika kwa jina la Wanzagi akilia kwa uchungu huku akifarijiwa na shangazi yake Anna Nyerere.

Ni huzuni kwa kila mtu.

Mama Maria Nyerere akiweka shada la mau kwenye kaburi la mtoto wake John Guido Nyerere.

Mtoto wa Marehemu anayeishi Lusaka Zambia, Sofia Nyerere Mwape akiweka shada la maua kwenye kaburi la Baba yake marehemu John Nyerere.

Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akitoa heshima mbele ya kaburi la marehemu John Gaudo Nyerere mara baada ya kuweka taji la maua.

Mbunge wa Bunge la Jumuiya ya Afrika Mashariki Shyrose Bhanji akiweka shada la maua kwenye kaburi la marehemu John Nyerere kwenye mazishi yaliofanyika nyumbani kwa marehemu Baba wa Taifa Butiama.

Askari wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wakishiriki kuweka mashada ya maua kwenye kaburi la John Guido Nyerere.

Baadhi ya Watoto wa marehemu pamoja na ndugu wengine.

Mheshimiwa Waziri wa Katiba na Sheria Dk. Asha-Rose Migiro akisoma salaam za rambi rambi kwa niaba ya Serikali ya Jamhuri wa Muungano wakati wa mazishi ya John Nyerere.
Emily Magige Nyerere akifafanua jambo wakati wa mazishi ya John Guido Nyerere. (Picha zote na Adam H. Mzee)

Wednesday 13 May 2015

MANISPAA YA BUKOBA YAZINDUA MFUKO WA BIMA YA AFYA(CHF) MATIBABU KWA KUTUMIA KADI (TIKA)

Manispaa ya Bukoba imezindua rasmi mfuko wa jamii wa Bima ya Afya CHF  ambapo wananchi watapatiwa matibabu kwa kutumia kadi kwa kuchangia shilingi elfu kumi kwa mwaka,Uzinduzi huo umefanywa na Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Jackson Msome kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera John Mongella katika kikao kilichojumuisha wadau wa Afya na waratibu wa mfuko huo kutoka makao makuu.Bwana Msome amesema kuwa mfuko huo utawawezesha wakazi wa Manispaa kupatiwa matibabu kwa kutumia kadi (TIKA) kwa mwaka mzima na hivyo kuwaepusha na usumbufu wakati wa kutafuta pesa za matibabu,Mapema akisoma hotuba Mkurugenzi wa sera, Mipango ya Afya katika ofisi ya Katibu mkuu wizara ya afya, Mariam Ally amewataka wadau wa afya kuhamasisha wananchi katika Manispaa ya Bukoba kujiunga katika mfuko wa jamii wa Bima ya Afya kwa manufaa yao ya badae.
Washiriki wakijiandikisha kwenye ukumbi wa St Francis Bukoba.
Bwana Muchuruza(kushoto) Mkurugenzi wa shirika lisilo la serikali KADETFU akiwa na Mzee Joansen Rutabingwa.
Mwanahabari wa CHF akiwa mambo sawa.
Mgeni rasmi akiwasili.
Washiriki .
Wafanyakazi wa Manispaa ya Bukoba.
Kaimu Mkurugenzi Manispaa ya Bukoba.
Mkurugenzi Mtendaji wa CHF akisoma rhotuba kwa washiriki.
Mkurugenzi wa sera, wizara ya afya Mariam Ally akitoa hotuba.
Wanahabari wakiwa kazini.
Naibu  Meya Alexandar Ngalinda akiwakaribisha washiriki.
Mgeni rasni Mkuu wa wilaya ya Bukoba Jackson Msome akitoa hotuba.
Diwani Robert Katunzi akitoa neno la shukrani kwa niaba ya washiriki.
Mkuu wa wilaya akipokea mashuka 150 yaliyotolewa na  CHF kwa ajili ya wagonjwa wa hospital ya rufaa ya Kagera.
muwezeshaji akiendelea na mada.
Wananchi changamkieni fursa.