Tuesday 2 August 2016

MUFTI WA TANZANIA ATEMBELEA KABURI LA ALHAJI JAFFARI SAKIBU BWANIKA NA KUSHIRIKI DUA MAALUMU KAMACHUMU BUKOBA.

Mufti wa Tanzania Abubakari Zuberi ameshiriki dua maalumu ya kumkumbuka marehemu Alhaj Jaffari Sakibu Bwanika iliyofanyika nyumbani kwa marehemu Kamachumu kijiji cha Bushagara ,wilaya ya muleba. Pia kilifanyika kisomo maalumu kwa ajili ya kuombea  Taifa kwa ujumla,wageni mbalimbali kutoka ndani ya nchi na nje ya nchi walishiriki, Ni utaratibu wa kila mwaka ambao umeandaliwa na wanafamilia, ukutunisha ndugu, jamaa na marafiki kutoka maeneo tofauti, hii ni mara ya nne sasa tangu familia ya marehemu Jaffari Sakibu Bwanika kuanzisha utaratibu huu, mbali na mufti kuudhuria ,pia uongozi wa juu wa Bakwata,mashehe mbalimbali walishiriki.

 Shekhe kutoka Uganda,kilemba chake kilikuwa kivutio kikubwa.
 Bw Kandanda akiwa na pilika za hapa na pale
  Mufti akipokelewa na kiongozi wa familia Abdulfifuu  Jaffar Bwanika.
 Wakiwa makaburini.
 Waziri wa viwanda na biashara Charles Mwijage(kushoto) akiwa na balozi Ngemera.
 Kushoto shekhe wa mkoa kagera Haruna kichwabuta akiwana Mufti i Zuberi.
 Waziri Mwijage akiwa na diwani Kamala.
 Shekhe Mustafa.
Shehe mustafa akiomba dua.