Saturday 28 February 2015

KARAMAGI AENDELEA NA ZIARA YA KUIMARISHA CHAMA BUKOBA VIJIJINI,AZIDI KUWAMWAGIA VIFAA VYA MICHEZO VIJANA

Mnec wa Bukoba vijijini Mh Nazir Mustafa Karamagi ameendelea kwa kasi kubwa   kupita katika vijiji na kata za Jimbo la Bukoba vijijini kukutana na vijana kuzungumza nao na kugawa vifaa vya michezo na vizibao maalumu kwa ajiri ya waendesha pikipiki maarufu bodaboda.Akiongea na vijana katika nyakati tofauti maeneo ya Rukoma, Kibirizi,Kyaitoke, Izimbya na Mugajwale amewataka vijana wote washiriki katika michezo,na mtazamo wao usihishie tu kwa ajiri ya burudani, bali mtazamo wao uwe katika kutambua kuwa mchezo wa mpira wa miguu ni ajira, na kuipitia michezo unaweza kujiajiri na kuendesha maisha,kwa upande wa bodaboda am,ewagawia vizibao maalum ili waweze kutambulika na nyakati za usiku  waweze kutambuliwa kirahi na waendesha magari barabarani kuepukana na ajari zisizo za lazima,Mh Mnec  anaendel;ea na ziara yake na anatarajia kuhitimisha ziara yake leo 28-2-2015 kwa kutembelea  kata 29 zenye vijiji 94 katika jimbo la Bukoba vijijini.
Vijana wakimsikiliza Mneck kwa makini.
Katika picha Mh Mnec akiwa na vijana ambao tayari wamekabidhiwa vifaa vya michezo.
Waendesha pikipiki wakiwa wameshakabidhiwa vizibao maalum.
Katibu wa wilaya Bukoba Vijijini ccm akiongea na vijana.
Mh Mnec akizungumza na wananchi.

Maneo mengi wananchi walijitokeza kwa wingi kumsikiliza Mnec na wengine walimpokea kwa nyimbo  na nderemo.
Waitu wakola ta Karamagi
Hii ndio hali halisi alikopita mh Karamangi, watu walifurika.
Tutaendelea kuwaletea matukio ya siku ya mwisho wa ziara yake, endelea kutembelea jamcobukoba.blogspot.com

KAPTEN JOHN KOMBA HATUNAE TENA.

Mbunge wa Mbinga Magharibi Mh Kapten John Komba  amefariki dunia leo saa 10 jioni katika hospital ya TMJ Mikocheni Dar es salaam. Kwa mujibu wa maelezo ya mwanae Jerry Komba amesema kifo cha marehemu baba yake kimetokana na ugonjwa wa kisukari, Ambapo akiwa nyumbani kwake  mbezi beach sukari ilishuka na kukimbizwa hospital na mauti kumkuta.

Friday 27 February 2015

MNEC WA BUKOBA VIJIJINI NAZIR KARAMAGI ATOA VIFAA VYA MICHEZO NA VIZIBAO KWA WAENDESHA PIKIPIKI KUIMARISHA CHAMA.

 Mjumbe wa halmashauri kuu ya chama cha mapinduzi anaewakilisha wilaya ya Bukoba vijijini Naziri Karamagi anaendelea na ziara ya kuimarisha chama na hasa kuwawezesha vijana na kuwapa moyo katika shughuli zao na kuwawezesha kupata vifaa vya michezo  Jezi , Mipira na vizibao kwa vijana wanaofanya biashara ya kuendesha pikipiki,Mnec Karamagi akiongelea kuhusu michezo amesema vijana wanayohaki ya kupata vifaa vya michezo na kuonekana katika muonekano nadhifu kama wachezaji wa timu kubwa nchini na nje ya nchi,kwa upande wa waendesha pikipiki amesema  wanapokuwa katika sare maalumu wataweza kutambuana vizuri na  kuonekana na kutambulika kwa  wateja au abiria wanaotumia  pikipiki zao. Mnec Karamangi yupo kwenye ziara ya jimbo zima la Bukoba vijijini,katika  habari hii ametembelea maeneo ya Kaibanja, Katoro, Kyamulaile, Ruhunga na Butelankunzi.
 Katibu wa ccm Bukoba vijijini Mwishehe Maurid Acheni akiongea na wananchi katika  kijiji cha Kaibanja, kueleza na kumshukuru Mnec kwa jitihada za kusaidia vijana.
 Mh Karamagi akiwa na mwenyekiti wa halmashauri ya Bukoba vijijini Mh Kapteni Mstaafu Kateme.
 Mnec  akiongea na vijana.
 Mh Mnec akikabidhi vifaa vya michezo kwa timu za vijana Bukoba vijijini.
 Mh Mnec Karamagi akiwa na Katibu wa uvccm Bukoba vijijini.
 Vijana waendesha pikipiki wakiwa wameshakabidhiwa vizibao vyao.
 Waendesha pikipiki wakimsikiliza Mnec.
 Msaidizi wa Mnec Bi Georgia Kalikawe akitabasamu kwa maana ya kufurahia zoezi  linavyoendelea.
 Mnec akikabidhi vifaa.
 Pande za Katoro.

 Waitu kasinge,ogendelele kubaooo,ta karamagi. Ni maneno ya wananchi yalisikika.
Mh Karamagi anaendelea na ziara katika maeneo mbalimbali Bukoba vijijini.