Saturday 23 December 2017

HONGERA SULEIMAN NA RUTH KWA KUUKIMBIA UKAPERA.

 Ilikuwa ni shangwe na sherehe ya aina yake katika viwanja vya Stella Hotel (Walkgard Hotel)pale Bw Suleiman na Bi Ruth walipoamua kuukimbia ukapera na kuanza maisha ya ndoa, maisha yanayompendeza Mungu. Hongereni.
 Katika viwanja vya Stella Hotel au Walgard Hotel.
 Kwa hisia kali sana.
Jamcoblog inawatakia maisha mema ya ndoa.

Tuesday 19 December 2017

TATU MZUKA WASHIRIKI AZIMIO LA KAGERA,USIKOSE KUCHEZA JUMAPILI 24-12-2017 MILIONI 100 KUTOLEWA .

 Ni vijana wenye nyuso za furaha wakiwa wamevaa T shirt za TATU MZUKA wakiwa katika kongamano la  Azimio la Kagera Mapinduzi ya fikra na uchumi, USIKOSE KUSHIRIKI KUANZIA SASA TATU MZUKA UTAJIPATIA MAMILIONI YA FEDHA,JUMAPILI HII 24-12-2017 MILIONI 100 KUTOLEWA, CHEZA KWA WINGI TATU MZUKA.
 HAPA NI TATU MZUKA TU.

KONGAMANO LA AZIMIO LA KAGERA LAFANA,WAZIRI AWATAKA WATENDAJI WA SERIKALI KUACHA UMANGI MEZA.

 Waziri wa Tamisem Suleiman Jaffo amewataka watendaji mbalimbali katika wizara yake kuacha tabia ya kunyanyasa wananchi na kujiona miungu Watu , pale wananchi wanapokwenda katika ofisi zao kwa ajili ya kuhitaji huduma mbalimbali kwa ajili ya kuendeleza maisha yao,Waziri Jaffo aliyasema hayo katika Kongamano la Azimio la Kagera lililoandaliwa na kituo cha tv cha Clouds Tv, wakiwa wanatekeleza agizo la rais Dkt John Magufuli wakati wa ziara yake Mkoani Kagera alimtaka Mkurugenzi wa vipindi  Clouds Tv Bw Ruge Mutahaba kuandaa kongamona kwa ajili ya kuibua na kujadili Fursa mbalimbali katika nyanja za kibiashara , kilimo, ujasilimari na mambo mengine kwa ajili ya maendeleo ya wananchi, kongamano hili lilifanyika Bukoba katika ukumbi wa Bukoba hotel na washiriki kutoka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania walishiriki.(katika picha kulia ni Waziri wa biashara, viwanda na uwekezaji Charles Mwijage, Bw Ruge Muta
haba, Waziri wa Tamisem Suleiman Jaffo na mkuu wa Mkoa Kagera Meja Jenerali mstaafu Salum Kijuu.)