Tuesday 8 April 2014

CHUO CHA UALIMU ERA KINACHOFUNGULIWA MWEZI WA SABA MWAKA HUU CHAANZA UANDIKISHAJI WANAFUNZI, KUWA NA URAFIKI NA GLOBAL CITIZENS NETWORK YA MAREKANI

 Hatimae uandikishaji wa wanafunzi katika chuo cha ualimu ERA kinachotarajia kuanza mwezi wa saba mwaka huu,Akiongea na mmiliki wa Blog hii ,Mwanzilishi wa chuo cha ERA kilichoko Bukoba Manispaa, kata ya Kitendaguro nje kidogo ya mji wa Bukoba Ndugu Paskazia Barongo amesema maandalizi yanaendelea vizuri na taratibu zote zinaendelea vizuri, ikiwa ni pamoja na kuandikisha wanafunzi wanaotarajia kuanza masomo mwezi wa saba mwaka huu.Amesema Ndugu Paskazia Barongo kuwa ni matarajio yao kuwa wamejipanga vizuri kutoa Elimu Bora ili waalimu watakaohitimu katika chuo cha ERA waweze kutoa elimu bora katika shule za msingi popote Tanzania kwa Weredi na ufasaha mkubwa,Pia ameeleza kuwa ile kuboresha mahusiano na  vyuo vingine ndani na nje ya nchi chuo chao kimeanzisha urafiki na  Global Citizens network walioko Minneapolis Marekani ili waweze kushirikiana katika maswala ya Elimu kwa wanafunzi wa ERA kwenda Marekani na wa Marekani kuja ERA. Ndugu Paskazia Barongo ameitaka jamii kwa ujumla kuleta watoto wao waliomaliza kidato cha nne  na hawakuweza kupata nafasi wajiunge na chuo cha ERA na watajikomboa wao binafsi na kuwa Walimu wa mfano katika kutoa elimu bora nchini Tanzania.
 Mama Ashura( Fundi cherehani) akimpima Unifomu mmoja wa wanafunzi anaetarajia kuanza masomo  chuoni mwezi wa saba mwaka huu
 Vipimo vya Unifomu
 Bi Paskazia Barongo akiongea na wanafunzi wanaotarajia kujiunga na chuo, wakisubiri kupima Unifomu chuoni hapo
 Bi Linda Stuart (kushoto) Mkurugenzi wa Global citizens network ya Marekani akiwa na Mkurugenzi wa Cosad Ndugu Smart Baitani anaeishi  Marekani
 Wanachuo watarajiwa wanaoanza masoma mwezi wa saba mwaka huu
 bI Paskazia Barongo akiwakaribisha wageni
 Mkuu wa  Chuo cha ERA  Bi Paulina Ngina Musau akieleza namna walivyojipanga kutoa Elimu katika chuo cha ERA
 Mmoja ya wanachuo wanaojiunga akitoa neno la shukrani kwa kuanzisha chuo
 Mwanachuo mtarajiwa akipongeza uongozi kwa wazo zuri la kuanzisha chuo cha ualimu
 Mzazi akinukuu vifungu vya Biblia na kusema chuo cha ERA ni mkombozi kwa watoto wao
 Wakipata kifungua kinywa
 Mtoto wa Bi Linda Stuart akipata chai
 Mkuu wa chuo akimtembeza kumuonyesha mazingira ya chuo na sehemu ya mabweni, katika chuo cha ERA Godoro na kitanda unavikuta chuoni ili kumpunguzia gharama mzazi
 Ni vitanda imara na salama
 Vyoo vizuri kwa afya ya wanachuo
 Mazingira ya kupendeza
 Bi Paskazia akitoa maelezo
 Picha ya pamoja
Mkuu wa chuo Bi Paulina akiwa na mmoja wa wakurugenzi wa chuo ambae pia ni mwalimu katika chuo cha ERA Bw Ocham Collins wakiwa na mtoto wao

No comments:

Post a Comment