Wednesday 7 August 2013

KAGASHEKI CUP 2013: TIMU YA BILELE WAFANYA KWELI WAIFUNGA TIMU YA HAMUGEMBE BAO 2-1, MCHEZAJI KHALFAN RASHID NDIYE MUUAJI!!

Kikosi Cha timu ya Hamugembe kilichoanza pamoja na Kocha wao (kushoto)

Dakika ya kwanza(1) Mchezaji Jingo Suleiman anaipatia bao timu ya Bilele baada ya kuachia shuti kali lililomuacha kipa wa Hamugembe na hapa ni wachezaji wa Bilele wakimpongeza.
Wachezaji wa Bilele wakishangilia na mashabiki wao baada ya kufunga bao dakika ya kwanza.
 ***********************
Na Faustine Ruta, Bukoba
Timu ya Bilele FC wenye maskani yao Bukoba Mjini ( Uswahili) leo imejikatia tiketi ya kucheza Nusu Fainali na kusonga mbele kwa kuifunga timu Hamugembe bao 2-1 kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.

Timu ya Bilele ndio walianza kuandika bao lao dakika ya 1 bao lililofungwa na mchezaji mshambuliaji Jingo Suleiman na kuwafanya Hamugembe wasiamini macho yao kwa goli hilo la haraka. Timu ya Hamugembe pia ilikosa mkwaju wa penati uliodakwa na kipa Erick Nkwenkwe, penati iliyoleta utata kwa baadhi ya wachezaji wa Bilele na Mashabiki wao.

Dakika ya mwishoni mwa kipindi cha kwanza dakika ya 45 timu ya Hamugembe nao wakafanikiwa kusawazisha bao baada ya beki wa Bilele kujichanganya na kugawa pasi isiyo na macho kwa kipa wake na hatimaye mchezaji wa Hamugembe kutumia nafasi hiyo kusawazisha na kufanya 1-1.

Kipindi cha pili kilianza kila timu ikiwa makini ili kutafuta bao la ushindi na hatimaye timu ya Bilele kufanya mashambulizi ya uhakika katika dakika za majeruhi dakika ya 90 mchezaji Khalfan Rashid Kitenge wa Bilele akachomoka na kuwaacha mabeki na kutupia nyavuni, Kwa ushindi huu Bilele wanajikatia tiketi ya kucheza Nusu fainali na timu iliyoshinda jana Makhirikhiri (Kitendaguro) kwenye Nusu Fainali wiki ijayo siku ya Jumanne tarehe 13.08.2013.

Wadau wakifuatoia mtanange Kidogo Bilele wafungwe bao hapa..Mchezaji wa Bilele akiendesha huku mchezaji wa Hamugembe akimkinga hapa hupiti!!
Kipa wa Bilele akiondoa mkwaju wa penati hapa.....Patashika uwanjani hapa wachezaji wa Bilele wakiwenka ngumu kwa wachezaji wa HamugembeMchezaji wa Bilele akiondosha mpira kwa kichwa hapa
Mashabiki
You might also like:

No comments:

Post a Comment