Wednesday 7 August 2013

Hatua iliyofikiwa katika kuanzisha moja wa Fedha wa Jumuiya ya Afrika Mashariki




Mchumi Mwandamizi wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Emmanuel Mbwambo akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu hatua iliyofikiwa na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika majadiliano ya kuanzisha umoja wa fedha wakati wa mkutano na Waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Habari Bi. zamaradi Kawawa. (Picha: Frank Mvungi)

TAARIFA YA HATUA ILIYOFIKIWA NA NCHI WANACHAMA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI KATIKA MAJADILIANO YA KUANZISHA UMOJA WA FEDHA


1.0       UTANGULIZI

Ibara ya 5(2) ya Mkataba wa Uanzishwaji wa Jumuiya ya Afrika Mashariki inabainisha kuwa Umoja wa Fedha ni hatua ya tatu ya Mtangamano wa Afrika Mashariki. Madhumuni ya Umoja wa Fedha ni kujenga ukanda tulivu wa kifedha (monetary and financial stability zone) utakaoharakisha kusaidia ukuaji wa biashara na shughuli za kiuchumi ndani ya Jumuiya. Katika kufikia malengo haya ya Umoja wa Fedha Nchi Wanachama, ikiwemo Jumuiya ya Afrika Mashariki, hukubaliana yafuatayo:-

i. Kuongeza kiwango na kasi ya mtangamano wa masoko ya fedha na mitaji (deepen financial market integration);
ii. Kuhuisha sera za kibajeti za nchi Wanachama (harmonisation of national fiscal policies);
iii. Kuwa na utaratibu wa kuendesha shughuli za uchumi bila kukinzana na malengo ya Umoja wa Fedha;
iv. Kuunda Benki Kuu moja ya Jumuiya (EACB) itakayosimamia Sera moja ya fedha(single monetary policy) na sera moja ya viwango vya ubadilishanaji fedha (exchange rate policy); na
v. Kuanzisha sarafu moja ya Jumuiya;

2.0    HATUA ILIYOFIKIWA

Mchakato wa uundaji Umoja wa Fedha wa Afrika Mashariki ulianzishwa na Kikao cha 15 cha Baraza la 

t
 
 
Picture
Mwanasheria Mshauri wa Baraza la Ushindani (FCT) Bi. Hafsa Said(kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari sheria mbalimbali na kesi ambazo zimeshawahi kuendeshwa na baraza hilo, kwenye mkutano uliofanyika ukumbi wa Idara ya Habari, kulia ni Mchumi Mshauri wa Baraza hilo Bw. Nzinyangwa Mchany.
BARAZA LA USHINDANI (FAIR COMPETITION TRIBUNAL – FCT)

MADA KUHUSU BARAZA LA USHINDANI ILIYOWASILISHWA KWA WAANDISHI WA HABARI TAREHE 6 AGOSTI 2013, KATIKA UKUMBI WA HABARI MAELEZO, DAR ES SALAAM

Utangulizi

Ndugu Waandishi wa Habari, mada yetu inahusu Baraza la Ushindani. Katika mada hii tunatarajia kuliezea Baraza la Ushindani kuwa ni chombo cha namna gani, majukumu yake na uwezo wake kisheria. Hivyo, ili kuweza kuwapa maelezo yatakayoweza kuwasidia kuandika makala zenu vizuri mada hii imejengwa katika sehemu tatu kuu kama ifuatavyo:
  1. Chimbuko la Baraza la Ushindani;
  2.  Baraza la Ushindani ni nini
  3. Majukumu na Uwezo wa Baraza.

Chimbuko la Baraza la Ushindani

Bila shaka mtakumbuka kwamba katika jitihada za kuboresha na kuimarisha uchumi mwaka 1986, Serikali ya Tanzania iliamua kubadilisha mfumo wa uendeshaji wa uchumi kutoka kwenye mfumo wa uchumi hodhi (planned economy) na kufuata mfumo wa uchumi wa soko (Market Economy). Kwa kifupi katika Mfumo wa uendeshaji wa uchumi hodhi maamuzi yote makubwa yanayohusisha uendeshaji wa uchumi hufanywa na Serikali, wakati katika mfumo wa uchumi wa soko, maamuzi yote makubwa hufanywa kwa kutegemea mwelekeo na nguvu ya soko.   Aidha, mfumo wa uchumi wa soko unashirikisha kwa kiasi kikubwa sekta binafsi. Katika mfumo huu huduma na bidhaa sokoni hutolewa na kuuzwa kwa ushindani. Uzoefu duniani umeonesha kuwa bila kuwa na usimamizi mzuri wa ushindani sokoni migongano na mivutano ya kimasilahi 


No comments:

Post a Comment