Saturday 1 February 2014

MANGULA APEWA SOMO NA MUJATA MBEYA


Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula katika mkutano wake na Wanachama wa Mujata uliofanyika katika ukumbi wa CCM Mkoa wa Mbeya uliopo Sokomatola Jijini hapa.

Viongozi wa Mujata wakiwakilishwa na machifu wa mkoa wa Mbeya wakimvisha Shuka Makamu Mwenyekiti kama ishara ya kumkaribisha Mkoani Mbeya na kuwa Mlezi wa Mjata popote aendapo.



Mwenyekiti wa Mujata, Chifu Shayo Soja Masoko akimkabidhi Zawadi Makamu Mwenyekiti wa CCM

Wajumbe wa Mkutano kati ya Mujata na makamu Mwenyekiti wa CCM Philip Mangula wakifuatilia kwa makini Risala inayosomwa na Katibu wa Mujata Uswege



ASASI ya Muungano wa Jamii Tanzania(MUJATA) imekishauri Chama cha Mapinduzi (CCM) mambo yanayochangia kudhoofisha Chama na kutoa mwanya kwa vyama vya upinzani kupata nguvu na kukubalika katika jamii tofauti na ilivyokuwa mwanzo.
Ushauri huo ulitolewa na Asasi hiyo kwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara, Philip Mangula katika mkutano wake na Wanachama wa Mujata uliofanyika katika ukumbi wa CCM Mkoa wa Mbeya uliopo Sokomatola Jijini hapa.
Akizungumza katika mkutano huo Mwenyekiti wa Mujata, Chifu Shayo Soja Masoko, ambaye alimwambia Makamu Mwenyekiti kuwa Chama kikitaka kuendelea kutawala na kukubalika katika jamii jinatakiwa kufanya utafiti kabla ya kuteua wawakilishi wa wananchi katika maeneo mbali mbali.
Alisema Chama kikifanya utafiti wa mtu anayekubalika katika jamii bila kujali uwezo wake wa kifedha na  elimu na kumchagua kuwa mwakilishilishi wao itasaidia kuondoa makundi, Rushwa na vurugu katika jamii kutokana na makao makuu kuteua watu wasiokubalika na jamii.
Aidha katika Risala yao kwa Makamu Mwenyekiti, Mujata walitoa maoni mbali mbali ya namna ya kukijenga chama na kuendelea kuaminiwa na Watanzania ambayo ni pamoja na Chama kuwapa uongozi ndani ya chama baadhi ya watu wanaoshindwa kuhoji utendaji wa Serikali kwa ngazi za uenyekiti na katibu katika ngazi ya Shina.
Pia walishauri chama kudhibiti baadhi ya wagombea wanaotumia fedha ili kupata madaraka hata kama hawakubaliki katika jamii na uongozi kuendelea kuyafumbia macho bila kuwachukulia hatua zozote na kufanya nchi kukithiri kwa rushwa.
Akijibu baadhi ya mambo yaliyoko kwenye Risala hiyo, Makamu Mwenyekiti wa Tanzania Bara, Philip Mangula, alisema Chama kina utaratibu wake wa kushughulikia wanachama wanaokiuka kanuni za chama kwa maksudi kwa kuwaita na kuwaonya kwa misingi ya Katiba ya Chama.
Alisema katika Siasa hakukosekani Machangudoa kamawalivyo mitaani ambao kazi yao ni kujipisha pitisha bila kujali utaratibu na kuongeza kuwa jamii inatakiwa kuwadharau kabisa na kwamba hata chama hakikubaliani na hali hiyo.
Mangula alisema Wanasiasa duniani kote ndiyo waanzilishi wa migogoro katika jamii  kutokana na kukosa Sera za kuwaambia  wananchi wake hivyo kulazimisha kuonekana kwa kutumia njia zisizohalali ikiwemo kuwachonganisha wananchi.
Aliongeza kuwa wanaotafuta uongozi kwa kutumia fedha ni halali kwamba hawana uwezo na hawajiamini ndiyo maana huna mbinu mbadala ya kulamisha kukubalika ni kutumia fedha jambo ambalo linazalisha taswira mbaya katika Taifa.
Aidha Mangula ambaye katika Mkutano huo alivisha Shuka kama ishara ya kuwa Mlezi wa Chama cha Jamii popote nchini, alikipongeza chama hicho kwa jinsi walivyofanikiwa kuzima baadhi ya matukio ya uhalifu Mkoani Mbeya na kuondoa dhana mbaya iliyokuwa ikijulikana kuhusu Mkoa wa Mbeya.
Baadhi ya mambo waliofanikiwa kudhibiti na kuyakomesha kabisa ni pamoja na Uchunaji wa Ngozi, Mauaji ya Watoto, Upigaji wa nondo, wananchi kujichukulia Sheria mikononi, Maandamano yasiyokuwa na tija katika jamii, Vurugu zinazochochewa na vyama vya Siasa na viongozi wa dini likiowemo suala la Uchinjaji wa Nyama.

No comments:

Post a Comment