Saturday 8 February 2014

YANGA HATAREEEEE YAICHAPA KOMOROZINE MABAO 7-0 UWANJA WA TAIFA LEO


 Mshambuliaji wa Yanga, Mrisho Ngassa, akiruka kupiga mpira wa kichwa na kufunga bao la kwanza katika dakika ya 13 kipindi cha kwanza. Katika mchezo huo wa Klabu Bingwa Barani Afrika kati ya Yanga dhidi ya Komorozine ya Comorro, uliomalizika hivi punde kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Yanga imeibuka na ushindi wa mabao 7-0.  

Ngassa alipachika mabao matatu kati ya saba katika dakika za 13, 64 na 68. Bao la pili lilifungwa na Nadir Haroub, katika dakika ya 16, Didier Kavumbagu, dakika ya 57 na 80 na Hamis Kiiza, akifunga katika dakika ya 59.
 Goooo, bao la kwanza Ngassa akimgalagaza kipa wa Komorozine....
 Goooooo, bao la pili likifungwa na Canavaro.
 Wakishangilia moja kati ya mabao yao....
 David Luhende, akiwania mpira na kipa wa Komorozine....
 Mrisho Ngasa akishangilia bao lake la tatu....
 Sehemu ya mashabiki
 Ngasa akishangilia na Oscar Joshua.....
 Wakomorozine hoi baada ya kipigo hicho.....
 Ubao wa matangazo unavyosomeka hadi mwisho wa mchezo huo.
 Makocha wakipongezana baada ya mchezo huo....
 Mbuyu Twite akichezewa faulo.....
 Hamis Kiiza akiwania mpira na beki wa Komorozine....
 Haruna Niyonzima, akimfanya kitu mbaya beki wa Komorozine....

*YANGA INAONGOZA MABAO 2-0 UWANJA WA TAIFA DHIDI YA KOMOROZINE

 Nahodha wa timu ya Yanga, Nadir Haroub 'Canavaro', akijikunja kupiga mpira wa kichwa cha chini na kufunga bao la pili, baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na David Luhende baada ya Mbuyu Twite, kuchezewa Faulo na beki wa Komorozine, Ali Mohamed. Bao la kwanza lilifungwa na Mrisho Ngasa, akiunganisha mpira wa Krosi iliyopigwa na Simon Msuva.
 Mshambuliaji wa Yanga, Hamis Kiiza, akijaribu kuuwahi mpira mbele ya beki wa Komorozine, wakati wa mchezo huo kipindi cha kwanza.
Wachezaji wa Yanga, wakicheza kushangilia bao la kwanza lililofungwa na Mrisho Ngasa (katikati).

*WANAOANZA KUWAKIMBIZA WAKOMORO UWANJA WA TAIFA MUDA HUU

 Kocha wa Makipa Juma Pondamali, akiwafua makipa Deogratius Munishi na Juma Kaseja, wakati wa kupasha misuri moto. 

Timu zote hivi sasa zinaingia uwanjani tayari kabisa kwa kukaguliwa kuanza mtanange huo.

VIKOSI VINAVYOANZA
YANGA:- Juma Kaseja, Mbuyu Twite, Oscar Joshua, Nadir Haroub (c), Kelvin Yondani, Frank Domayo, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Hamis Kiiza, Mrisho Ngassa na David Luhende.

RIZEVU:- Deogratius Munishi, Rajab Zahir, Nizar Khalfan, Didier Kavumbagu, Juma Abdul, Hussein Javu, na Hassan Dilunga.

WACOMORO:- Attoumani Farid, Ali Mohamed, Nizar Amir, Abdou Moussoidikou, Ahamadi Houmadi Anli, Moidjie Ali, Mortadhoi Fayssoil, Attoumane Omar, Mohamed Erfeda (c), Mouayade Almansoor na Ahmed Waladi.
 Wachezaji wa Yanga wakiingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo baada ya kupasha misuri
 Wachezaji wa Comorro, wakiingia vyumbani....
Sehemu ya mashabiki.

No comments:

Post a Comment