Tuesday 10 September 2013


*BODA BODA SI KWA ABIRIA TU BALI HATA MZIGO WA NYANYA

 Dereva wa bodaboda akisafirisha nyanya
Wafanyabiashara wa nyanya wakisubiri wateja. Huu ni msimu wa nyanya ambapo zao hilo limepungua bei huku kisado kikiuza hadi Sh. 1500.

*MATUKIO YA BARABARANI DAR ES SALAAM - ARUSHA

 Fuso lenye namba za usajili T 509 AGD, likiwa limeanguka na kumwaga mzigo wote wa Nyanya uliokuwa umebebwa na fuso hilo. Haikuweza kufahamika kwa haraka chanzo cha ajali hiyo.
 Mmoja wa wahusika akijaribu kuomba msaada kwa magari yaliyokuwa yakipita eneo hilo.
 Mafunzo wa Kampuni ya Strabag, wakiendelea na kazi ya upanuzi wa barabara ya Arusha inayoendelea kupanuliwa ambapo kwa sasa magari yamekuwa yakitumia muda mrefu kumaliza eneo hilo kwa kupita katika barabara vumbi iliyowekwa kwa dharula.
 Upanuzi wenyewe ni kama hivi
 Gari ndogo inayoelezwa kuwa iligongwa na basi la Happy Nations eneo la Mto Wami, likiwa limeegeshwa nje ya Kituo cha Polisi cha Wami.
 Mafundi wakiendelea na ujenzi wa mitaro katika barabara mpya ya mabasi ya Kaskazini, inayotokea Bagamoyo.
 Jamaa wakilinda mzigo wao nyuma ua Canter, kutoka Soko la Kariakoo kuelekea Tegeta.
 haikuweza kufahamika jamaa hawa walikuwa wakisafiri kwa staili hii kuwa walikuwa na matatizo ya kijamii au ndo tatizo la usafiri, hapa wakitokea bagamoyo kuelekea Chalinze katika barabara mpya....
 Ni baadhi ya wachezaji wa Taswa Fc, waliposhuka kupata chakula cha mchana maeneo ya Korogwe wakati wakielekea Mkoani Arusha kushiriki Bonanza linaloandaliwa na Taswa Arusha kila mwaka.
 Safari hiyo ilijumuisha timu zote mbili ya Taswa Fc na Taswa Queens....
 Wachezaji wakishuka garini kuelekea kupata msosi....
 Maeneo ya mbali na mijini hivi ndivyo vituo vya mafuta ambapo huuzwa kwa lita moja moja kama hivi...
Mafuta aina ya Petroli, yakiuzwa kwa staili hii jambo ambalo ni hatari....

*AJALI HAINA KINGA

 Baadhi ya abiria waliokuwa katika gari lililogongana na gari ndogo (pichani chini) wakilia baada ya kutokea ajali karubu kabisa na maeneo ya njia panda ya Kunduchi, wakati mabinti hao na wenzao wakiwa safarini kuelekea Bagamoyo kama kundi kuhudhuria Bonanza la familia, mwishoni mwa wiki iliyopita. 
Baadhi ya abiria waliokuwa katika Coaster hilo, na mashuhuda wakijadili alaji hiyo. Katika ajali hiyo hakuna aliyejeruhiwa zaidi ya magari kuumia.

*ANGALIA AKILI YA DEREVA HUYU v/s MNYAMA HUYU

 Hapa ilikuwa ni barabara mpya inayotokea Bagamoyo kuelekea mikoa ya Kaskazini inayochomokea njia panda ya Chalinze, ambapo Mnyama huyu alikuwa akikatiza barabara kuelekea upande wa pili wa barabara hiyo, huku (kushoto) ni Lori lililokuwa katika mwendo na (kulia) mwa Lori hilo ilikuwa ni Coaster iliyokuwa ikijaribu kulipita Lori hilo.

Wakati Coaster ikikaribia kumaliza bodi ya Lori ndipo Mnyama huyu akatokea upande wa pili akivuka huku akikimbia kwa mbwembwe akiruka ruka jambo lililowafanya abiria waliokuwa katika Coaster kumfurahia huku wakimsikitikia  kuwa huenda asingewahi kuvuka kabla ya kulambwa tairi na Lori.

Lakini wakati abiria hao wakifurahishwa na Mnyama huyu ambaye alikuwa mithili ya Nyani, ghafla Dereva wa Lori aliwashangaza watu baada ya kutumia bodi kubwa ya Lori lake lililokuwa na tera 'Eti' kumkatia denge mnyama huyo ili amkanyage na ndipo Lori hilo liliyumba na kutaka kuanguka huku likitoka nje ya Barabara huku mnyama huyo akikatiza kiulaini na kuondoka zake.

Sasa sijui kama Dereva huyu angeangusha gari angejieleza alikuwa akifanya nini, au angeelezeaje sababu za kuangusha gari. MADEREVA, UTULIVU, AKILI NA BUSARA MUWAPO BARABARANI NDIYO KITU CHA KWANZA.
Hapa Lori hilo likitoka nje ya Barabara kumkatia denege mnyama huyo, ambapo lilimkosa na kuyumba wakati likijitahidi kurudi barabarani na kutaka kusababisha ajali kwa kuigonga Coaster iliyokuwa pembeni yake.

*SALAAM ZA PONGEZI KUTOKA MMK MEDIA GROUP

MMK MEDIA GROUP SWAHILI TV, SWAHILI RADIO na DMK411
Tunatoa pongezi zetu za dhati kwa mwana habari mwenzetu ndugu Issa Michuzi na Blog yake ya www.issamichuzi.blogspot.com kwa kazi kubwa walioifanya na wanayoendelea kuifanya ya kuhabarisha jamii yetu kwa muda wa Miaka tisa (9) mfululizo bila kupumzika.

Blog ya Issa Michuzi imetimiza miaka 9 tangu kuanzishwa  tarehe 8 Septemba 2005 jijini Helsinki, Finland.  Kwanza kabisa; tunampa hongera Ndugu  Michuzi kwa kuandika historia kwa kuleta mapinduzi ya habari ndani nchini na nje ya Tanzania.

Pili; tumefurahishwa sana kwa kitendo cha Ndugu Michuzi kurudisha shukrani na fadhila kwa Baba wa Ma-blog Bwana Ndesanjo Macha kwa kumtambulisha, kumuingiza na kumfungulia blog ya jamii ya  www.issamichuzi.blogspot.com mnamo tarehe 8 Septemba 2005 jijini Helsinki, Finland. 
Tatu; Pongezi za kipekee zimuendee Ndugu Issa Michuzi kwa kazi kubwa ya kutuhabarisha usiku na mchana pamoja na majukumu yake ya  kikazi akilitumikia vyema Taifa letu la Tanzania katika Ofisi Kuu kuliko zote akiwa kama  Mwanahabari Mpiga Picha (Photo Journalist) mwajiriwa wa Serikali akifanya kazi chini ya  Kurugenzi ya Mawasiliano, Ofisi ya Rais Ikulu ya Tanzania.

Nne; Ni ukweli usiopingika kwamba Issa Michuzi ni mtu wa watu, anapenda watu na ucheshi wake umemletea mafanikio makubwa katika tasnia ya habari. Kwa upande mwingine Michuzi ameitumia vyema nafasi ya kipekee aliyopata kutuhabarisha kwa kutujuza mambo mbalimbali yanayoendelea ndani na nje ya nchi. Hakuna ubishi tukijiuliza swali ni wafanyakazi wangapi waliopo sasa hivi Serikalini katika nafasi kama ya  Michuzi, ama waliopita ambao wamefanya mapinduzi ya habari kama Michuzi? 
Ndugu msomaji, ukweli unabaki palepale Michuzi anastahili pongezi za kipekee kwa kuthubutu.

Mwisho kwa kumalizia napenda kuufahamisha Umma kwamba  Bwana Issa Michuzi amekuwa mfano wa kuigwa na jitihada zake na mazingira yake kikazi yamekuwa chanzo cha mafanikio na umaarufu mkubwa aliojizolea na kujijengea jina nchini na nje ya nchi. Hongera kwa jitihada na harakati zako.

Tunatambua pia kwa nafasi uliyonayo kikazi inakupa mlango wa kupata habari kabla ya vyombo vingine vya habari kupata,  na vilevile kwa kuwa mwajiriwa wa Serikali umejijengea heshima kwa taasisi, wizara na vyombo vingine vya Kiserikali kukuleletea habari zao moja kwa moja wewe kwanza kabla ya vyombo vingine, kitu ambacho kimefanya watu wengi tuwe tunasoma blog yako na kuipenda kitu ambacho ni kuzuri na cha kuigwa.

Mwisho tunakuomba ukaze mwendo na uendelee kutuhabarisha

No comments:

Post a Comment