Thursday 15 August 2013

CCM MKOA KAGERA NI MAJANGA.... MWENYEKITI WA CCM MKOA CONSITANCIA BUHIYE ATUNISHA MSULI ASEMA HAJASIKIA TAMKO LA NAPE NA HALIHUSIANI NA MAAMUZI YA HALMASHAURI KUU YA MKOA YA KUWAFUKUZA MADIWANI WANANE

 Muda mfupi uliopita mwenyekiti wa mkoa wa kagera ccm constansia buhiye ameita waandishi wa habari na kuongea nao katika ukumbi wa mkutano wa ccm mkoa na  kusisitiza kuwa maamuzi yaliyotolewa na halmashauri kuu ya mkoa ya kuwafukuza na kuwaondolea nyadhifa za udiwani madiwani wanane wa chama mapinduzi manispaa ya bukoba,maamuzi yako palepale,akijibu baadhi ya maswali yaliyoulizwa na waandishi wa habari kuhusiana na tamko la katibu mwenezi taifa ndugu Nape kutengua maamuzi ya halmashauri kuu ya mkoa wa kagera,mwenyekiti amesema hata taarifa ya Nape hajaisikia, anacoeleza ni maamuzi waliyoyafanya kwa mujibu wa katiba ya chama, kauli  ya mwenyekiti ilizua maswali mengi kwa waandishi na kusababisha kuleta picha ya kauli za viongozi kupingana na kuchanganya wananchi kushindwa kuelewa kauli ya nani na yupi ni sahihi.
mwenyekiti wa ccm mkoa akiongea na waandishi wa habari leo kususitiza kuwa  maamuzi ya halmashauri kuu ya mkoa dhidi ya madiwani  wanane wa ccm bukoba mjini ndio sahihi
                              waandishi wa habari wakisikiliza maelezo ya mwekiti ccm mkoa wa kagera
                                       waandishi wakiwa makini kuandika anachoeleza mwenyekiti
kauli ya mwenyekiti imeonyesha alichozungumza Nape ni maswala binafsi,maamuzi waliyoamua halimashauri kuu mkoa ndio sahihi,na mkweli,nani msemaji  wa chama,yote hayo ni maswali  yanasubiri majibu
                                                                Endelea kufutilia jamcoblogspot.blogspot.com

No comments:

Post a Comment