Friday 16 August 2013

AKAMATWA NA MENO YA TEMBO YENYE THAMANI YA MILIONI 23.2 JIJINI MWANZA


 MKAZI wa Kijiji cha Buhemba Wilaya ya Butiama Mkoani Mara Yohana Jackison (27) amekamatwa na Askari Polisi wa dolia akiwa na vipande 10 vya meno ya Tembo vyenye thamani ya zaidi shilingi milioni 23.2 Jijini Mwanza.
Gunia lililokamatwa na nyaraka hizo za serikali (meno ya Tembo).
 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza Evarist Mangu jana alieleza kuwa mtuhumiwa huyo aliyekuwa akisafirisha meno ya tembo kutoka kijiji cha Buhemba kuja Jijini Mwanza alikamatwa na askari wa dolia katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Buzuruga majira ya saa 3:15 asubuhi kwenye kilichopo eneo la Nyakato baada ya kushitukiwa na askari hao.
Kamanda Mangu alisema kwamba baada ya kushuka kwenye basi dogo mali ya Kampuni ya JOHANVIA Express linalofanya safari zake kati ya Butiama na Mwanza akiwa ameficha vipande vya meno hayo ya Tembo kwenye gunia la mkaa ambapo baada ya kutelemka na kuonyesha wasiwasi ndipo askari hao waliamua kumsimamisha.
Vipande vya meno ya Tembo vikikaguliwa mara baada ya kutolewa kwenye gunia.
Yohana Jackison (27)

No comments:

Post a Comment