Tuesday 11 February 2014

MAZISHI YA MCHUNGAJI KABUGA YAFANYIKA BUKOBA ,SIMANZI ZATAWALA

 Amefariki usiku wa kuamkia ijumaa iliyopita jijini Dar es salaam alipopelekwa baada ya kutokea hospitali ya Bugando Mwanza akisumbuliwa na ugonjwa wa moyo.
 Mazishi yake yamefanyika nyumbani kwake Kagondo Kaifo manispaa ya Bukoba, ambapo picha juu ni Askofu wa kanisa hilo mkoani Kagera, aliyechukua nafasi yake alioachia kabla ya kuugua na chini walioudhuria mazishi wakiendelea kusalia mwili ulioko kwenye jeneza.

 Picha juu ni Kanisa la TAG Hamgembe alipokuwa akiongoza kanisa hilo, na chini ni gari iliyobeba mwili wa marehemu ukisindikizwa na magari na pikipiki kutokea mjini kati kwenda Kagondo.

Mchungaji JACKSON KABUGA, alizaliwa mwaka 1954 huko Kigoma Tanzania,ameishi mkoani Kagera kikazi na ameacha mjane na watoto 7.

No comments:

Post a Comment