Monday 13 May 2013

BANDARI YA BUKOBA YAZIDI KUBORESHWA ILI KUTOA HUDUMA BORA KWA MTEJA

      Leo camera yetu ilitembelea bandari ya Bukoba na kukuta shughuli zikiendelea vizuri, na hali ya mazingira ikionekana katika hali ya usafi na kuvutia,viwanja vya bandari hiyo kwa sasa vimeboreshwa kwa kuwekewa sakafu ambayo imeondoa kabisa ile hali ya tope kipindi cha mvua na vumbi kipindi cha kiangazi,Lakini pia upo ujenzi wa mzani unaendelea 'mzani huu utakao kuwa ukipitisha gari iliyobeba mzigo na kuwezesha kutambua uzito wa mzigo kwa haraka zaidi.  Pia camera yetu ilienda eneo la meli ya victoria ilipotia nanga,shughuli za upakiaji mzigo ulikuwa ukiendelea vizuri,.


 Shughuli za upakiaji mizigo  zikiendelea katika bandari ya bukoba mjini

 Meli ya mv victoria ikiwa imetia nanga bandari ya bukoba,na shughuli za upakiaji mizigo zikiendelea
 Wafanyabiashara wa ndizi wakishusha ndizi bandari ya bukoba kwa ajili ya kupelekwa Mwanza


 Upakiaji mizigo melini hutumia craine ili kurahisisha upakiji kwa haraka na usalama zaidi wa mizigo na wabebaji mzigo

 baharia shomari akiwa kazini
 trector hutumika kuvuta tela  la mizigo kusogeza eneo la kupakia


 kapteni mwasa  wa victoria (kushoto) akiwa katika mazingira ya bandari ya bukoba akiangalia shughuli zinavyoendelea 

 Kijana Bunduki akiwa na  ndugu akida kwenye dirisha la tiketi


 Dada Akida akiendelea na kazi zake

 Ndizi mbivu zinazopelekwa mwanza kibiashara
 Mama mjasiriamali akisubiri kupakia ndizi zake mbivu kupeleka Mwanza
 Abiria wanaokwenda kwenda Mwanza wakikata tiketi dirishani

 ndugu Methew Mathias(passenger Argent) bandari ya bukoba

 Upimaji wa mizigo ukiendelea,mzani mkubwa unaojengwa kwa sasa utakapokamilika upimaji wa mizigo utakuwa rahisi zaidi


 Eneo la bandari ya bukoba linavyoonekana,tope na vumbi kwa sasa ni historia.

 Eneo la abiria kukaa na kusubiri kuingia melini limeboreshwa bandari ya bukoba
 abiria wakisubiri muda wa kuingia melini kuelekea mwanza
 Hapa ndio unajengwa mzani mkubwa bandari ya bukoba
 MZANI HUU UKIKAMILIKA UTARAHISISHA UPAKIAJI WA MIZIGO KIRAHISI
 ENEO LA GETI LA KUINGIA BANDARINI
TUNAIPONGEZA SERIKALI,WIZARA NA MAMLAKA YA BANDARI KWA KUBORESHA BANDARI YA BUKOBA ILI KUMUWEZESHA ABIRIA.MTEJA KUTUMIA HUDUMA ZA BANDARI YA BUKOBA. KWA HABARI ZA UHAKIKA ANGALIA jamcobk.blogspot.com

No comments:

Post a Comment