Thursday 17 July 2014

MABASI YENYE TV [TELEVISHENI] KILA SITI YATUA TANZANIA


Katika ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia tunaweza shangaa mengi ama kufurahia mambo mengi yakizidi kurahisishwa katika vitu vingi tuvitumiavyo. Zamani haikuwa rahisi hata kuipata gari yenye hata Televisheni moja lakini hivi sasa mambo si kama enzi za zama za kale.

Hivi sasa tunapata kujionea kewenye magari ya kampuni ya RATCO ya mabasi yaendayo Tanga wameleta mabasi yenye Televisheni katika kila kiti cha abiria. Raha ilioje hii..? Na zaidi sasa magari yaliyo mengi yana soketi za umeme katika kila kiti ambapo utaweza kuchaji simu yako huku ukisafiri.

No comments:

Post a Comment