Friday 18 April 2014

EXCLUSIVE,MH:MWIGULU NCHEMBA AFUTA POSHO ZA WAJUMBE WALIOSUSIA BUNGE LA KATIBA,AAGIZA BENKI KUSITISHA CHEQUE ZOTE.E

MWIGULU NCHEMBA1 
Wizara ya Fedha kupitia Naibu wake Waziri wa fedha Mh. Mwigulu Nchemba wametangaza uamuzi wa kufuta malipo ya Wabunge waliosusia vikao vya mchakato wa Katiba vinavyoendelea Dodoma.
Uamuzi huu umetangazwa ikiwa ni siku ya pili tangu Wajumbe wa Bunge la Katiba Kutoka UKAWA wasusie Shughuli za Bunge la Katiba kwa Madai wamechoka matusi na Kuburuzwa kwenye Bunge hilo.
Hii leo Naibu waziri wa Fedha Mh.Mwigulu Nchemba ambaye kwa Sasa anakaimu Kuwa Waziri wa Fedha tangu April 10  20014 baada ya  Waziri wa Fedha kupata safari ya kikazi nchini Marekani,amefuta Malipo ya wabunge waliosusia Mchakato huo wa Katiba.
Mheshimiwa Mwigulu Nchemba ameagiza Benki zote kurudisha Cheque za Malipo ya Posho na seating allowance ambazo zilipelekwa Bungeni April 16 ili ziwekwe kwenye akaunti binafsi za Wabunge ikiwa ni Malipo ya Mpaka April 30. 
Bonyeza play kumsikiliza Mh.Mwigulu Nchemba akielezea hili

Mwigulu Insert 18April2014


No comments:

Post a Comment