Friday 18 April 2014

Rais Kikwete akerwa na kitendo cha wanasiasa kumtukana Mwalimu Nyerere....Asema ni utovu wa nidhamu kuwatukana waasisi wa Tanzania

 
Rais Jakaya Kikwete amesema ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa adabu unaoonyeshwa na baadhi ya Watanzania kuwatukana, kuwadhihaki na kuwakejeli waanzilishi wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere na Sheikh Abeid Amani Karume.
Rais Kikwete alitoa kauli hiyo juzi alipokuwa kwenye mahojiano maalumu na wahariri wa baadhi ya vyombo vya habari (wa Mwananchi hawakuwapo) ya kuadhimisha miaka 50 ya Muungano.
Kauli hiyo ilikuwa ni jibu la moja ya maswali alilokuwa ameulizwa na wahariri hao kuhusu matusi, kejeli na dhihaka ambazo zimekuwa zinaonyeshwa na wajumbe wachache wa Bunge Maalumu la Katiba juu ya waasisi hao wa Tanzania na wabunifu wakuu wa Muungano wa Tanzania.
“Ni kukosa adabu na ni utovu mkubwa wa nidhamu kwa Mtanzania yeyote kuwatukana, kuwadhihaki au kuwakejeli waasisi wa Taifa letu. Hawa ni watu ambao waliifanyia nchi yetu mambo makubwa,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:

No comments:

Post a Comment