Tuesday 3 February 2015

MAYATIMA WA KITUO CHA NUSURU YATIMA KASHAI WASHIRIKI DUA YA SHUKRANI NYUMBANI KWA FAMILIA YA JAMAL KALUMUNA

 Nusura Yatima ni kituo cha kulea  Watoto wadogo mayatima kilichopo kata ya Kashai Manispaa ya Bukoba,Familia ya Jamali Kalumuna ilifika kituoni hapo na kuwachukua watoto wote kushiriki nao Dua ya kumshukuru mwenyezi mungu kuwanusuru katika tukio la kuvamiwa na watu wanaosadikiwa ni majambazi nyumbani mapema mwezi jana.Pamoja na kusoma dua ya shukrani pia familia ilipata chakula cha usiku na watoto hao yatima na kutoa zawadi kidogo kwa watoto hao,Kupitia mtandao huu tunawaomba watu mbalimbali wafike kuwaona mayatima hawa na wanahitaji msaada mkubwa kwani  wanatunzwa na Mama Nuru alijitolea kufanya hii kazi ngumu na kubwa kwa kujitolea na bila kuwa na chanzo chochote cha kumuwezesha kusaidia watoto hawa yatima.
 Ni Bango la kutambulisha kituo hicho ambalo linaendelea kufutika,lakini pia watoto hawa wanahitaji msaada  kutoka kwa wadau mbalimbali,Yawezekana nawe msomaji ni yatima, lakini uyatima unatofautiana,yawezekana wewe ni yatima mwenye uwezo a kujimudu na ni mtu mzima, hawa ni yatima na watoto wadogo sana wanaohitaji msaada wako.
 Wakipanda gari kuelekea kwenye dua nyumbani kwa Familia ya Jamal.
 Dua ikiendelea, na dua ya mtoto  yatima  ni makubur, yaani ni bora kuliko ya mtu mzima.
 Kulia ni shekhe Idrisa akiwa na mwalimu wa watoto yatima wakiendelea na dua.
 Hawa ni yatima jamani tuwasaidie.
 Kulia ni Bw Ben Kataruga , rafiki wa familia  akishiriki dua.
AMINA YARABI AMINA..
 Mwenyezi mungu wahepushe na wabaya viumbe wako.
 Badae wakapata maakur.
 Pacha akihudumia watoto.
 Pacha mkubwa nae akihudumia watoto.
 Jamco, baba Right,na Bw Ben Kataruga wakipata supu..
 Bw Adamu MUBAGO akipata msosi.
 Mama mwenyeji , Mama Jamco akiwa na mwanae Jabir Jamal.
 Ukafika wakati wa kueleza nia na madhumuni ya uwepo wa wageni,Jamal Kalumuna akasimama kuzungumza na kuwashukuru wote walioiombea familia na kuwa nao kwa karibu wakati wa matatizo hayo.
 Ni Zawadi za nguo , viatu na vitu vingine vilivyotolewa na familia kwa ajili ya matumizi ya watoto yatima wakirejea kituoni.
 Bw Ben Kataruga baada ya maelezo akaguswa  na akasimama kuongea, kikubwa aliona upo wajibu mkubwa sana wa kusaidia watoto yatima, na akahaidi kufika kituoni na kupeleka msaada wake, na kuwasihi wadau mbalimbali kuwasaidia mayatima.
 Jamco family.
Jamcobukoba.blogspot.com kwa habari za uhakika. piga simu 0788-707027 au 0754-757157.

No comments:

Post a Comment