Sunday 14 September 2014

MAMBO YALIKUWA HIVI YA VICTOR NA LYDIA MLIMANI CITY ANGALI PICHA 190,CHOPA YATUA SAA 12.15 JONI.

 Ni ngweee ya mwisho katika mlolongo wote wa mpangilio wa harusi ya Victor Alcard Mwombeki na Lydia Protas unaishia Mlimani City kwa chopa kupaa mara 2 na kutua 2 katika maeneo yaliyokuwa yamepangwa.Victor akiwa kavishwa na kampuni ya mitindo ya Sheria Ngowi na Lydia alievishwa na kampuni kubwa nchini Tanzania Eva collection wakiingia katika ukumbi uliopambwa na kupambika Mlimani City.
 Hii ndio hali halisi katika ukumbi
 Mmoja ya wapambaji maarufu Mama Matungwa akiwa na Mume  Mr Robert Matungwa akifuatilia kwa makini kinachoendelea ukumbini,kwanza ulikuwa unakutana na Menu ikieleza upande wa vinywaji vilivyopo,na vyakula vitakavyokuwepo,lakini mpangilio mzima wa meza ulipendeza.
 Ni sehemu ya lango la kuingilia ukumbini unakutana na kitu cha namna hii unapata picha kabla ya kuingia ndani
 Katika swala zima la vinywaji kampuni ya Mabibo beer & wine ilijipanga ni mwendo wa  windhock,juice za box,vikali tofauti ilikuwa ni uwezo  wako na speed yako katika kutumia,namaanisha kama kasi yako ungeanza kwa kasi basi wewe mapema sana mchezoni ungetoka.
 Watu walitoka pande tofauti tofauti kushoto ni mmoja wa wakutubi kutoka chuo kikuu cha Josiah Kibira(JOKUKO) kilichopo Bukoba maeneo ya Nyakato  Bukoba.
 Akudo band kama kawaida walikuwepo
 Ni moja ya kaunta ya vinywaji vikali ndani ya ukumbi
 Kaka mkubwa Ernest Nyambo uso kwa uso na camera yetu
 Ni kwamba kabla ujamaliza au zimebaki mbili unapewa nyingine bila kuomba kama unavyoona jamaa akabaki kushangaa na kuhoji jamani mnampango gani leo na hizi windhoeck zenu?
 Sehemu ya marusi kukaa, hakuna mambo mengi , ni machache lakini kiwango.
 Keki
 Ulikuwa kila meza unakutana na kibox cha hivi kwa ndani ni chokulate
 Mmoja ya boss wa Bw Harusi katika Biashara
 Bosi mwingine
 Bosi mwingine
 Kundi la ngoma kutoka Bukoba
 Mzee Rugemarila akiwa na mkewe
 Kushoto Pro Anna Tibaijuka Waziri wa Ardhi ,Nyumba na makazi nae ndani ya nyumba
 Kushoto Mama mzazi wa Bi harusi akiwa na mama mzazi wa Bw harusi
 Angalia vizuri na kwa umakini mpangilio wa meza na vilivyopo.
 Ni nguo ya tatu, na badae ilivaliwa ya nne,hapana chezea EVA COLLECTION
 Hii ni history kwetu mke wangu
 Wakiingia ukumbini
 Wapambe nao walitishaaaa mbayaa
 Gauni hili ilikuwa ni moja ya kivutio kikubwa ukumbini, maana alipotembea nalo lilionekana kuvimba na kuchezacheza
 Ninomaaa
 Akudo bendi wakiimba wimbo wa mama vanesa, wimbo maalumu uliotunwa siku kitambo kwa ajili ya bi Lydia mama vanesa na kuingia katika moja ya nyimbo zinazopendwa sana na mashabiki. mama vanesa ndio huyu Bi harusi .
 Kwa mbele unaona stand za camera zikitafuta matukio
 Abashagazi
 Mama Saverina akiwa na mwanae
 Baadhi ya waimbaji wa Akudo bendi
 Akudo
 Wanenguaji wa Akudo
 Akicheka na camera yetu
 Sheria Ngowi ndio walimvisha Bw harusi cheki kitu kwa karibu
 Ni vitu tofauti vilivyokuwa vinasambazwa kila meza
 Ni madikodiko kibao yalikuwepo,ilikuwa ni kula unaingia mpaka unatoka ni kula tu
 Mzinga mkubwa wa shampein
 Nshomile kama kawaida yake akawapagawisha wahaya na watu tofauti
 Ukiishiwa unaletewa
 Mzee Rugemarila baba mdogo wa bw harusi akitoa neno
 Wasanii kutoka Nigeria nao wakatumbuiza
 Bi Harusi katika pozzzz
 Mwanamke kujikubari
 Tishaaa mbaya
 Queen katikati akishare love na wenzake
 safi sanaaa
 Nilishe nikulishe
 Karibuni wazazi wangu
 Taji Liundi mc wa viwango akiwakilisha na kuongea chochote kinachoendelea ukumbini
 Marafiki wote wanaofanya kazi na Bw Harusi Kariakoo wakafungua Bonge la shampein kuonyesha upendo
 Wakati wa msosi
 Hebu angalia mwenyewe
 Eneo la matunda
 Dah ilikuwa poa sana
 obu buki chonkaa(mama anauliza kitu gani hiki)
 Sasa nichukue nini hapa
 Kwaitooo
 Mke wangu hivi hawa watu tutawalipa nini?
 Mmiliki wa kampuni ya ubunifu mavazi Eva Rugemarila (EVA COLLECTION) akiwa na baba mzazi na mama yake mzazi .Eva ndio alihusika katika swala la mipango yote ya maharusi mavazi, mapambo na ushauri wa kuboresha.
 Onyesha upendo kwa mama au mkeo unamsaidia mtoto nae apata raha,niliipenda sana hii big up  mkaka.
 Hapa ni swala la kisu,uma linatumika
 Mjukuu wa Rugemalira nae akapata nafasi ya kuongea aliyokuwa nayo moyoni.
 Katikati msanii Bahati akimtambuisha mama saverina mke wake, ni vijimambo tu unapokuwa kwenye harusi iliyotulia.
 Barnaba akichana live
 Bi harusi kaishabadilika nguo ya nne kwa siku ya leo.
 Mzee akimuelezea Victor mbele za watu kuwa ametambua ukaribu alionao na watu,maana alichokiona hakutegemea, na akaendelea kusema Victor is a fighter mpambanaji kapambana mwenyewe akitokea Bukoba akaingia mjini akaangaika mwenyewe mpaka mafanikio aliyonayo sasa.Hongera kijana wangu na iwe funzo kwa wengine simama mwenyewe.
 Wakisikiliza maneno mazito ya mzee Rugemarila akimzungumza Victor
 Baada ya maneno mazito akamvisha kanzu kuashiria sasa umekuwa msimamizi wa familia
 Vaa mwanangu
 Victor ndani ya kanzu
 Akavishwa na koti kisha akakabidhiwa mkuki kama siraha ya kumlinda yeye na familia
 Mama Rugemarila nae akatoa nasaha zake
 Akamkabidhi kiabu cha mungu biblia
  Zawadi ya picha nzuri ya msalaba
 Ghafla akaingia mtu wa watu kulii ni Ben Mulokozi akiwa na mmiliki wa blog hii
 Ikapigwa picha ya ukumbusho
 Hongereni sana maharusi
 Hongera dada yangu
 Mwenyekiti wa kamati na sherehe wilbrod Mutabuzi  akimpa akiwapa mikono  maharusi kuashiria kazi mliyonituma na kunikabidhi niisimamie na wajumbe wote leo tumeikamilisha kwa asilimia za juu sana.
 Mwenyekiti wa kamati na sherehe nzima Bw wilbrord Mutabuzi akitete na bw harusi
 Kijana makini sana kushoto John Mwendabantu katibu wa kamati akiwa na mdau wakiteta
 Kamati ya maandalizi nao wakaibuka kwa stail hii, mrushe Bw harusi juu,Kamera zilizofungwa kwenye stendi zake maalumu zikamfuata hukohuko juu.
 Tukachezee kipenzi wa roho yangu
 Watu wakipinda migongo na kubinuka
Barnaba akawapagawisha kwa burudani wageni waliobahatika kuhudhuria,Dada huyu hakika anaweza kutoka Bukoba akionyesha utaalamu wake kwenye swala zima la kuzungusha kiuno.

No comments:

Post a Comment