Tuesday 25 March 2014

KAMATI YA UONGOZI YA BUNGE MAALUM YAFANYA KIKAO CHAKE CHA KWANZA LEO


 Mwenyekiti wa Bunge Maalum Mhe. Samuel Sitta akiongoza kikao cha kwanza cha kamati ya Uongozi baada ya kuundwa leo. Kamati hiyo inayoundwa na wenyeviti wa Kamati za Bunge Maalum wote 12  pamoja na mambo mengine inajukumu la kaundaa ratiba ya Bunge Maalum. Kushoto kwake ni Katibu wa Bunge Maalum Yahya Khamis Hamad na aliyekaa kulia ni Makamu Mwenyekiti wa Bunge Maalum Mhe. Samia Suluhu Hassan.
 Mhe. Sitta akiendelea kuongoza Kikao cha Kamati ya Uongozi
 Naibu Katibu wa Bunge Maalum Dkt. Thomas Kashililah akitoa ufafanuzi kwa wajumbe wa kamati ya Bunge Maalum kuhusu uwezo wa kutumika kupigia kura vifaa vya kielekroniki vilivyofungwa katika ukumbi wa Bunge wakati kamati hiyo ilipokutana jana.
 Mjumbe wa Kamati ya Uongozi Mhe. Anna Abdalah akifafanua jambo wakati wa kikao cha kamati hiyo.
 Wajumbe wa Kamati ya Uongozi ya Bunge Maalum wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wakati wa kikao hicho.
Sehemu ya wajumbe..

No comments:

Post a Comment