Wednesday 19 March 2014

DAKIKA 90 ZIMEMALIZIKA YANGA YALAZIMISHWA SARE NA AZAM FC NA KUGAWANA POINTI KWA BAO 1-1,BEKI YA YANGA YAFANYA UZEMBE MKUBWA


 Wachezaji wa Yanga kakifanya mazoezi kabla ya mechi dhidi ya Azam
 Wadau sambamba na camera yetu wakiingia uwanja wa Taifa
 Azam Tv wakiwa kazini
 Mashabiki wa Yanga akishangilia
 Ni mmoja wa mashabiki wa Yanga aliekuwa akifanya vituko uwanjani akiwa na njiwa wake
 Wachezaji wa timu zote wakisalimiana kabla ya mpambano kuanza
 Wachezaji wa Azam kabla ya mechi kuanza
 Ni yanga walipopata gori
 Yanga wakishangilia bao






Dakika 90 za Mtanange wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kati ya Yanga na Azam Fc, kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, zimemalizika kwa Mabingwa wa Soka Tanzania Yanga kulazimishwa sare na kufanya timu

kugawana pointi baada ya kutoka sare kwa kufungana bao 1-1. 

Bao la Yanga lilifungwa na Didier Kavumbagu katika dakika ya 14 kipindi cha kwanza huku bao la kusawazisha la Azam Fc, likifungwa na Kelvin Friday katika dakika ya 83. 

Katika dakika ya 70, Yanga walipata penati baada ya beki wa Azam, Said Morad, kuunawa mpira katika eneo la hatari. 

Penati hiyo ilipigwa na Hamis Kiiza na kupanguliwa na kipa Aishi Manula, na katika heka heka hizo Beki wa Azam Fc, Erasto Nyoni alizawadiwa kadi nyekundu. 

Kwa matokeo hayo sasa Azam Fc inaendelea kushikilia usukani wa ligi hiyo ikiwa na jumla ya Pointi 44 huku Yanga ikibaki nafasi ya pili ikiwa na pointi 40 lakini ikiwana na mchezo mmoja mkononi unaotarajiwa kupigwa mwishoni mwa wiki mjini Tabora na Rhyno,  na mbeya city wakibaki nafasi ya tatu. 

Heka heka langoni mwa Azam Fc.

No comments:

Post a Comment