Sunday 16 March 2014

BASI LA YANGA LAPATA AJALI LEO ASUBUHI MAENEO YA MIKESE MOROGORO



Kocha wa Yanga  HANS VAN PLUIJM (kulia), akifanya mawasiliano baada ya basi la timu yake kupata ajali eneo la Mikese. Kushoto ni Kocha wa Makipa, Juma Pondamali.
Kikosi cha mabingwa wa soka Tanzania Bara, Yanga kimepata msukosuko baada ya basi lao kutumbukia msingini katika eneo la Mikese mkoani Morogoro.
Basi hilo limepata ajali leo asubuhi wakati kikosi hicho kikiwa safarini kurejea jijini Dar, baada ya mchezo wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar uliopigwa jana jioni kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini humo, na kutoka sare ya bila kufungana.
Taarifa zinasema hakukua na majeruhi lakini baadhi ya wachezaji walilazimika kujiokoa baada ya basi hilo kulikwepa basi jingine ambalo lilikuwa linalifuata hilo la Yanga.

No comments:

Post a Comment