Thursday 29 January 2015

TALGWU YATOA VITANDA KWA AJILI YA MAMA WAJAWAZITO,MASHINE KWA VITUO VYA AFYA BUKOBA.

 Chama cha wafanyakazi wa serikali za mitaa (TALGWU) kimetoa vifaa vya huduma ya afya vitanda maalumu kwa ajili ya mama wajawazito kujifungua na mashine kwa ajili ya kusaidia kutoa uchafu watoto wachanga wanapozaliwa,vifaa vyote vilivyotolewa vina thamani ya milioni kumi na mbili,vifaa hivyo vimetolewa katika vituo vya afya Manispaa ya Bukoba na Bukoba vijijini,Uongozi wa TALGWU Taifa ulikabidhi vifaa hivyo kwa katibu tawala wa Mkoa wa Kagera Bw Nassor Mnambila ambae alikuwa mgeni rasmi katika hafla fupi iliyofanyika katika viwanja vya ofisi ya Manispaa ya Bukoba.
 Mkuu wa wilaya Bukoba Bi Zippola Pangani akiwa na viongozi wa TALGWU Taifa.
 Kaimu mkurugenzi Manispaa ya Bukoba Bw Chibhunu Lukiko akisalimiana na mwenyekiti wa Talgwu Taifa Suleiman Abdalah Kikingo(kushoto)
 Mwenyekiti wa Talgwu Taifa akisaini kitabu cha wageni ofisini kwa Mkugenzi Manispaa ya Bukoba.
 Mgeni rasmi akiwasili.
 Mc wa hafla akiongoza ratiba.
 Wanachama wa TALGWU.
 wimbo wa shime tujiunge pamoja ukaimbwa.
 Dk Musa akifurahi na camera yetu.
 Wanachama wa TALGWU.
 Mwenyekiti wa TALGWU Taifa  Suleiman Abdalah Kikingo akieleza kwa kifupi umuhimu wa kusaidia mama wajawazito na watoto.
 Mgeni rasmi katibu tawala Mkoa wa Kagera Nassor Mnambila akitoa hotuba yake,amesema thamani ya msaada huu wa vifaa kwa ajili ya kusaidia mama wajawazito wakati wa kujifungua na mashine ni zaidi ya thamani ya fedha,maana watakaonufaika na vifaa hivi ni wamama wengi sana na hivyo kufanya thamani ya vifaa hivyi kuwa kubwa zaidi, pia amewataka wafanyakazi wa vituo vya afya kuvitunza vifaa hivyo.
 Mganga mkuu wa Mkoa wa Kagera Dk  Thomas Rutachunzibwa akisibitisha ubora wa vifaa vilivyoletwa.
 Katibu tawala wa Mkao akimbabidhi Kaimu Mkurugenzi wa Manispaa Bukoba vifaa kwa ajili ya vituo vya afya katika eneo lake.
 MWANDISHI WA HABARI WA CLOUDS TV Audax Mtiganzi akifanya mahojiano.
Jamcobukoba.blogspot.com kwa habari za uhakika,tupigie simu namba 0788-707027, 0754-757157.

No comments:

Post a Comment