Monday 2 June 2014

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AHUDHURIA SHEREHE ZA UTAMBULISHO WA RAIS WA MALAWI


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa ni miongoni mwa Viongozi wa Kitaifa waliohudhuria na kusikiliza hotuba ya kwanza ya Rais mteule wa Malawi, Prof. Mutharika zilizofanyika leo kwenye uwanja wa Kamuzu, jijini humo.

Miongoni mwa marais waliohudhuria ni pamoja na Rais Wa Botswana Ian Kama na Waziri wa nje Wa Msumbiji.

Prof. Mutharika aliapishwa rasmi siku ya jumamosi baada ya Tume ya uchaguzi nchini humo kumtangaza rasmi baada ya matokeo ambapo leo rais Mutharika amelihutubia rasmi Taifa hilo kwa mara ya kwanza tangu alipoapishwa jumamosi.

Baada ya Sherehe hizo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Bilal, amekuwa na mazungumzo ya tetea tete na Rais Prof.  Mutharika katika hoteli ya Sunbird. 
 Mke wa Makamu wa Rais, Mama Zakhia Bilal (nyuma) akiwa ni miongoni mwa waliohudhuria.
 Rais Prof. Mutharika, akiwasili uwanjani hapo akiwa katika gari la wazi.
 Wanahabari wakichacharika kunasa picha na matukio wakati Mutharika akiwasili kwenye uwanja wa Kamuzu Banda.
Sehemu ya umati wa watu waliohudhuria.

No comments:

Post a Comment