Wednesday 23 April 2014

NEWS ALERT!!!MAKAMPUNI MBALIMBALI KUWEKEZA KWENYE SEKTA YA ELIMU NCHINI

Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa akifungua mkutano wa siku mbili wa wadau  wa Teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) kutoka nchi za ukanda wa Bonde la ufa leo jijini Dar es salaam.

Baadhi ya washiriki wa mkutano wa wadau wa TEHAMA kutoka nchi za Bonde la Ufa wakimsikiliza Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa (hayupo pichani) akifungua mkutano wa siku mbili wa wadau Teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) kutoka nchi za ukanda wa Bonde la ufa leo jijini Dar es salaam.


Kauli hiyo imemtolewa na Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Prof. Makame Mbarawa alipokuwa akifungua mkutano wa siku mbili wa wadau Teknolojia ya habari na mawasiliano (TEHAMA) kutoka nchi za ukanda wa Bonde la ufa leo jijini Dar es salaam.
“Nawasihi wajasiriamali katika mambo ya TEHAMA ndani ya nchi washirikiane na wenzao wa nje ya nchi ili waweze kujijengea uwezo wa kukuza uchumi wa nchi yetu” alisema Prof. Mbarawa.
Prof. Mbarawa aliwasihi washiriki wa mkutano huo kuwa Tanzania inawakaribisha wawekezaji kuja kuwekeza katika TEHAMA ili kuhakikisha Watanzania wote wanapata huduma ya mawasiliano katika maeneo yote nchini hadi vijijini.
Aidha, Prof. Mbarawa alizitaja changamoto zinazoikabili sekta ya TEHAMA ni pamoja na ukosefu wa nishati ya umeme vijijini, kumudu gharama za uendeshaji, ukosefu wa vifaa vya sekta hiyo na usalama wa taarifa mbalimbali katika mitandao.
Kwa upande wake Waziri wa Mawasiliano, Habari na Uhusiano wa Bunge kutoka Burundi, Tharcisse Nkezabahizi alisema kuwa TEHAMA ni moja ya Nyanja muhimu inayotumiwa katika nchi yake ikiwemo elimu na huduma za afya ambapo ni muhimu kwa nchi za bonde la ufa kutumia teknolojia hiyo ili kukuza uchumi wan chi husika.
Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Digital Network Oy nchini Finland, Cipa Ojala alisema kuwa mkutano huo umekuja wakati mwafaka ambapo nchi nyingi zinatumia fursa iliyopo ili vyombo vya habari ikiwemo televisheni kuhama kutoka analogia kwenda dijiti.
Tanzania mpaka sasa imekuwa miongoni mwa nchi zinazofanya vizuri katika kutekeleza hatua ya kuhama kutoka mfumo wa analogia kwenda dijiti mbapo hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu takribani mikoa yote itakuwa imezima mitambo ya analojia kwenda dijiti.
Nchi zinazoshiriki katika mkutano huo ni Burundi, Rwanda, Somaliland, Zambia, Sudani Kusini ikiwemo Tanzania ambayo imekuwa mwenyeji wa mkutano huo kwa mara ya pili mfululizo pamoja na wadau wengine katika sekta hiyo. 

No comments:

Post a Comment