Sunday 19 January 2014

*BREAKING NEEEEWZZZ!!!! MAWAZIRI WAPYA HAWA HAPA: WAPO MIGIRO, JUMA NKAMIA ,MWIGULU NCHEMBA NA JENISTA MHAGAMA


 Katibu Mkuu Kiongozi,Balozi Ombeni Sefue.akitangaza baraza la mwaziri leo.

  •   Hakuna Mabadiliko Ofisi ya Rais
  • Ofisi ya Makamu Wa Rais - Naibu Waziri Kitwanga amehamishwa na nafasi yake imejazwa na Mhe. Ali Mwalimu
  • Mwigulu Nchemba amekuwa Naibu Wizara ya Fedha (Sera). Aliyekuwa nafasi hiyo sasa ni Waziri Kamili
  • Uchumi na Mapato sasa anatoka Janet Mbene na inajazwa na Adam Malima
  • Dr. Asha rose Migiro sasa ni Waziri wa Katiba na Sheria
  • Kwenye Ulinzi na Kujenga Taifa ni Dr. Hussein Mwinyi
  • katika Mambo ya Ndani - Mathias Chikawe
  • Afya na Ustawi wa Jamii - Naibu wake sasa ni Waziri Kamili; naibu wa sasa ni Dr. Kebwe S. Kebwe
  • Waziri Mulugo amepigwa chini rasmi . Nafasi yake imejazwa na Jenista Muhagama
  • D. Sophia Simba amebaki na naibu wake akiwa ni Pindi chana katika wizara ya Jinsia na watoto.
  • Katika wizara ya Mifugo na Maendeleo yake ni Dr. Titus Kamani mbunge wa Busega atakuwa Waziri mpya. Naibu wake ni Saning'o Kaika Telele na hivyo Wizara nzima imepata mawaziri wapya
  • Mhe. Ole Medeye Amepigwa chini na nafasi yake kuchukuliwa na George Simbachawene katika wizara ya Ardhi ila bado waziri wake ni Prof. Tibaijuka)
  • katika kilimo na Chakula waziri ni yule yule na Naibu wake ni  Godfrey Zambi.
  • Wizara ya Habari na michezo waziri ni yule yule Dr. Fenella Mukangara ila naibu wake ni mpya , Mtangzaji wa zamani na mbunge wa Singida Bw. Juma Nkamia.
  • Maliasili na Utalii Nyalandu amekuwa Waziri Kamili. Naibu ni Mahmood Hassan Mgimwa
  • Katika Nishati na Madini ni Prof. Sospeter Muhongo na Naibu wake ni Charles Kitwagwa akiichukua toka kwa Simbachawene.

No comments:

Post a Comment