Sunday 7 September 2014

MWENYEKITI WA MAKAMPUNI YA IPP MEDIA MZEE REGINALD MENGI ACHANGIA MILIONI KUMI KUSAIDIA UKARABATI WA KANISA LA KILUTHERI USHARIKA WA KASHURA BUKOBA

 Hili ndio kanisa la kilutheri usharika wa Kashura Bukoba Manispaa lenye zaidi ya miaka mia moja tangu lijengwe na sasa litaanza kufanyiwa ukarabati hivi karibuni.
 Mzee Reginald Mengi,kupitia kwa Mbunge wa jimbo la Bukoba Balozi Khamis Kagasheki ametoa ahadi ya kiasi cha shilingi milioni kumi kusaidia ukarabati wa kanisa.
 Mh Balozi Khamis Kagasheki ambae alikuwa mgeni rasmi kwenye Ibada maalumu  na harambee ya kuchangia ukarabati wa kanisa la kilutheri usharika wa Kashura.akielezea kupokea mwaliko huu alibahatika kukutana na Mzee Reginald Mengi akiwa Dar-es-salamu na alimjulisha mwaliko wake wa kuwa mgeni Rasmi katika harambee yauchangiaji ukarabati wa kanisa alimwambia kupitia kwake atachangia kiasi cha shilingi milioni kumi.
 Mchungaji wa kanisa la usharikika wa kashura Alex Kasisi katika maubiri yake amewasihi waumini na watu wote kwa ujumla kuwa makini sana na  Ulimi na hasa unapokuwa unazungumza.Ulimi umekuwa ukichonganisha watu, ulimi umekuwa ukivunja ndoa za watu, ulimi umikuwa ukisababisha uvunjaji wa amani katika maeneo mengi.
 Wanafunzi wa Josiah Girls high school wakiwa kwenye shughuli, uongozi na shule umechangia kiasi cha laki moja.
 Washarika
 Mtangazaji wa Kasibante Redio Nicoras Ngaiza akirusha moja kwa moja LIVE  Matangazo kutoka kanisani
 Ndugu Ruge Masabara (katibu wa kamati ya maandalizi) akiwa na mkewe
 Mzee byolwango mwanakwaya mahiri wa kwaya ya vijana usharika wa kashura
 Kushoto ni Katibu mkuu wa  ELCT NWD Mchungaji Elmeck Kigembe akiwa na Mchungaji wa kanisa la Kashura Alex Kasisi
 Katikati ni Askofu mstaafu Mushemba
 Kushoto ni Naibu katibu mkuu ELCT NWD  Jonas Rwezaura.
 Wazee wakimpongeza mgeni rasmi baada ya kutangaza ahadi ya milioni kumi za Mzee Reginald Mengi
 Mnada wa vitu mbalimbali
 Tv nchi 32 iliyotolewa na Mzee Jonas Masabara yenye thamani ya  1,065,000 ilinunuliwa na mgeni rasmi kwa kiasi cha  2,800,000 na tv hiyo mh Balozi kagasheki mgeni rasmi alimpa zawadi Katibu mkuu wa ELCT  NWD Mchungaji  Elimeck Kigembe kwa matumizi yake ya nyumbani.
 Waumini wakishangiria baada ya mgeni rasmi kuinunua tv
 Mgeni rasmi akimkabidhi tv  Katibu mkuu wa ELCT
 Mgeni akikabidhi pesa kwa bw Musheshe
 Bw Stanley Byolwango akikusanya taslimu
 Mwenyekiti wa Bukoba Veteran Seif Mkude  akichangia harambee  kumuunga mkono mgeni rasmi ambae ni mlezi wa wanaveterani Bukoba
 Bingwa akimpongeza Balozi Kagasheki
Mgeni rasmi Balozi Khamis Kagasheki akiagana na Uongozi wa Kamati ya maandalizi .

1 comment: