Tuesday 1 October 2013

KAPOTIVE STAR SINGERS-BUKOBA KUWASHA MOTO GOLD CREST HOTEL-MWANZA MWEMA JUMAPILI HII TAR.06/10/13.




Kikundi mahiri cha KAPOTIVE  Star Singers- Bukoba kitafanya uzinduzi wa album yake nzuri sana  ya Yesu ni Mwema, na utambulisho wa album nyingine kama “Nakushukuru Mungu”, “Zawadi ya Krismass n.k siku ya  Jumapili tar. 06/10/2013 katika ukumbi wa Gold Crest hotel- Mwanza.
Katika uzinduzi huo, mgeni rasmi atakuwa Mheshimiwa Samuel Sitta, Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, na mgeni maalum atakuwa Baba Akofu Method Kilaini, Askofu msaidizi wa Jimbo Katoliki la Bukoba ambae pia ni mlezi wa kikundi hiki.
MC katika uzinduzi huo atakuwa Bw. Bernard Mukasa, mtunzi ahiri wa nyimbo za Dini, na watasindikizwa na mwimbaji mahiri wa nyimbo za injili Dada Christina Shusho,  kwaya ya Mt. Benedicto parokia ya Bugando, na kwaya ya vijana ya AIC-Bwiru.
Kiingilio kitakuwa 15,000 kwa mtu mmoja (single size ticket) na 50,000 kwa watu 4 (Family size ticket).
KAPOTIVE Star Singers_Bukoba wamejizolea umaarufu katika uimbaji mahiri, na maonesho yao makubwa ambayo yamefanyika Bukoba na Dar-es-Salaam yaliwavutia wengi.
Watu wa Mwanza msikose burudani ya aina yake siku ya Jumapili tar. 06/10/13 katika ukumbi wa Gold Crest-Hotel, katikati ya jiji la Mwanza. Karibu tuwaunge mkono vijana wetu.



No comments:

Post a Comment