Monday 2 September 2013

MKUU WA MKOA WA KAGERA KANAL FABIAN MASSAWE AFUNGUA KIWANDA CHA KUTENGENEZA NGUO KATIKA KATA YA KIBETA MANISPAA YA BUKOBA

 Mkuu wa mkoa wa kagera akiongea na wageni waalikwa katika ufunguzi wa kiwanda cha kutengeneza nguo Endeavour group ltd kilichopo kata ya kibeta bukoba manispaa,mkuu wa mkoa amewataka wahaya wote wenye uwezo wa kuwekeza waje waitengeneze bukoba sasa,kanal massawe amesema duniani kote ukienda utamkuta muhaya, na wanauwezo mkubwa,sasa umefika wakati wa kuwekeza nyumbani,amewataka wawe na uchungu na bukoba,ambayo asilimia kubwa ya ya majengo yake yamechakaa,na nyumba nyingi mabati yamekuwa mekundu ,na hicho ni kielelezo tosha kuwa bukoba inapaswa kubadilika.
 kati ni mkurugenzi wa kiwanda akimtambulisha meneja wa kiwanda kwa mgeni rasmi kanal massawe
 mgeni rasmi akiangalia namna mashine za kushona nguo zinavyotumika ,na kufanya kazi kwa haraka zaidi na kwa muda mfupi
                                  picha ya pamoja mbele ya jengo la kiwanda cha kutengeneza nguo
 mwenye miwani mzee mashasi,mkuuwa chuo kikuu jokuko keshomshahara akiteta na mgeni rasm
 mkuu wa mkoa kagera kanal Fabian massawe akikata utepe kuzindua rasmi kiwanda cha kutengeneza nguo
                                     mkurugenzi wa kiwanda akitoa maelezo kwa mgeni rasmi
 Ndugu paskazia barongo, mmoja mwa wawekezaji bukoba maispaa akiwa na mdau wa maendeleo manispaa ya bukoba
                                mgeni rasmi akiangalia nguo mbalimbali zinazotengenezwa kiwandani hapo
 kiwnda hiki kinashona sare za shule,masuti, nguo za watoto ,wanawake na wanaume,sare za mashirika ,makampuni,mahotel, sare za viwandani nk
                                  wageni mbalimbali waliofika katika uzinduzi rasmi wa kiwanda

No comments:

Post a Comment