Tuesday 3 September 2013

JERRY MULO ATEMBELEA SHULE YA WASICHANA YA JOSIAH GIRL'S HIGH SCHOOL

Kwa siku chache mimi(Jamal kalumuna) nilizobahatika kuwa na mwandishi huyu Jerry Mulo nimeweza kuona utendaji kazi wake na umakini mkubwa kwa kile anachokifanya,lakini pia mimeshuhudia sehemu alizokuwa akifika jinsi watu walivyompa pongezi nyingi na wale waliokuwa hawjawahi kumuona ana kwa ana wanakuwa na shauku ya kumsalimia na kumpongeza kwa kazi zake ambazo amekuwa akifanya na kuonyeshwa katika vituo mbalimbali vya tv hapa nchini na nje ya nchi.Hali hii binafsi ilinifanya nijitahidi sana kuwa karibu na mtu huyu kwa nia ya kujifunza namna anavyofanya kazi zake,ndipo nikabahatika kutinga nae ghafla bini vuu katika shule ya sekondari ya  wasichana  josiah girl's yenye kidato cha kwanza mpaka kidato cha sita iliyoko katika kata ya ijuganyondo manispaa ya bukoba mkoa wa kagera,Hapo ndio nikaweza kushuhudia utendaji wa Jerry Mulo,mpendwa msomaji nimekutana na waandishi wengi na hasa wale kwa kiasi fulani hujiona wako juu kuliko wenzao huyu ni tofauti,nimeshudia akiohi maswali  yake na wakati mwingine kushika camera mwenye  ili aweze kufanya kazi yake vizuri. lakini kikubwa  leo katika habari hii  ni kujua  namna kampuni ya yokama ilivyoamua kwa mapenzi ya dhati kumpa mtoto wa kike elimu bora , na kumkomboa mwanamke katika wimbi la ujinga na kumuendeleza ili hapo badae wapatikane wataalamu wengi wa kike katika nyanja tofauti katika taifa la Tanzania na duniani kwa ujumla, na ndio maana ipo sasa Josiah girl's high school,yenye kidato cha kwanza mpaka cha sita.
Jerry mulo akiwa ametinga ghafla katika ofisi ya mkuu wa shule ,Alvera kashushura na kuanza mazungumzo
kazi ikiendelea hapo ni mwalimu wa taaluma Aziaki wangwa akieleza swala zima la kumuelimisha mtoto wa kike
                                     wanafunzi wakiwa darasani,hawa ni kidato cha pili
                   josiah girl's wameona mbali zaidi katika teknologia, maana hujifunza hata kwa njia ya tv
                                                     baadhi ya walimu wakiwa na furaha
                                 wanafunzi wakiwa mahabara wakijifunza kwa vitendo
                      mwanamke anaweza,wanachangaya chemical, ni masomo ya sayansi
                      Jerry mulo akiwa katika harakati zake za kazi hapo josia girl's high school
            Josiah girl's high school asikwambie mtu , wameshaona mbali wapo kididital zaidi usipime
                            jerry mulo akiwa na baadhi ya wanafunzi wa kidato cha sita
m,walimu akifundisha kwa njia ya tv, mitaala yote imeingizwa kwenye computer na mwalimu anafanya kazi zake kirahisi na kwa ufanisi mubwa, mlete mwanao wa kike josiah girl's kwa elimu bora
                                                              mambo ndo kama hivyo kwenye tv
wanapata chakula,jumapili  kama nyumbani kwa wengine ni zaidi ya nyumbani ,ni pilau, nyama, na kuku kidogo
                                                    hakusita kupata nao msosi jerry mulo
ndugu msomaji fuatilia jamco bukoba .blogspot.com,nilipata wasaa wa kumuuliza jerry mulo yale matukio yake ya hatari ya trafiki nk ,nilitaka kujiridhisha picha alikuwa akizipiga vipi,hana iyana akanieleza na kunipa mbinu ,kaani chonjo Jerry mulo wa bukoba anakuja

No comments:

Post a Comment