Wednesday 28 August 2013

WALIMU WAWILI NA WAKULIMA WAWILI WAIBUKA WASHINDI WA PROMOSHENI YA AIRTEL YATOSHA


Washindi wa siku wa shilingi milioni moja wa promosheni ya Airtel yatosha bwana Thomasi Joackim Chali na Abdallah Omari Muhomba kwa pamoja wakionyesha furaha mara baada ya kukabithiwa zawadi za pesa
taslimu baada ya kuibuka washindi wa siku wa promosheni ya Airtel yatosha.
Meneja Uhusiano wa Airtel Bwana Jackson Mmbando akiongea na moja ya washindi wakati Airtel ilipochezesha droo ya saba ya washindi wa shilingi milioni moja kila siku wa promosheni ya Airtel yatosha
ambapo mpaka sasa zaidi ya shilingi million 44 zimeshatolewa. Akishuhudia ni Msimamizi wa bodi ya michezo ya Bahati nasibu.
 *   Zaidi ya shilingi million 39 bado kushindaniwa.
 *   Na washindi wa wiki ya sita wakabidhiwa zawadi zao.

Kampuni ya simu ya mkononi ya Airtel imetangaza  washindi wake saba wa wiki ya saba ya  Airtel Yatosha  promosheni na kukabidhi zawadi za  washindi wa wiki ya sita wa promosheni ya  Airtel Yatosha.

Airtel imechezesha droo ya wiki ya saba ya promosheni ya Airtel yatosha Jana  katika ofisi za makao makuu ya Airtel morocco jijini Dar es saalam ambapo wateja saba  wameibuka washindi wa kitita  cha
shilingi million 1 kila mmoja.

Washindi hao ni pamoja na Theresia Martine Komba wa Morogoro -Mkulima, John Kimoro wa kondo Dodoma -Mwalimu, Yohanna Masunga Zengo wa Maswa Shinyanga -Mkulima, Isabellah Joseph wa Chamwino Dodoma  -Mwalimu, Nassor Mohammed Nassor  wa Kariakoo DSM -Mfanyabiashara, Modest Laurian Mussa wa Bukoba Kagera  -Mfanyabiashara na  Masanja Mwanamenda
wa Nkyala Singida -Mfanyabiashara.
Wakati huo huo Airtel imeendelea kuwazawadia wateja wake kupitia promosheni ya Airtel Yatosha ambapo washindi wa wiki ya sita nao walikabidhiwa zawadi zao ambapo kila mmoja aliondoka na shillingi
milioni moja.

Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo katika ofisi za makao makuu ya  Airtel  bwana Abdallah Omari Muhomba  mmoja wa washindi  wa million  1 alisema, "nashindwa jinsi ya kuongea lakini nawashukuru sana Airtel kwa kuweza kunizawadia shilingi milioni 1 ambazo kwangu  nikama ndoto.
 Nategemea kutumia pesa hizi kujiendeleza kiuchumi na maaendeleo ya familia yangu. Binafsi nachukua fursa hii kuwaasa watanzania kushiriki katika promosheni hizi za Airtel na kwa hakika wataamka washindi kama
mimi hivi leo".

Kwa upande wake bwana Thomas Joachim Chali ambaye pia ni Mshindi wa wiki ya sita alisema, "anawashukuru Airtel kwa kuanzisha promosheni yaAirtel Yatosha , na kuahidi kuzitumia pesa zake kuendeleza na kupanua biashara kwa kuwa hiyo ndio shughuli kubwa anayoifanya"

Akiongea wakati wa makabidhiano hayo kwa washindi hao Meneja uhusiano wa Airtel bwana Jackson Mmbando alisema, "leo tunao washindi saba waliojishindia shilingi milioni 1 kila moja katika droo ya wiki.
Tumeendelea kushuhudia watanzania na wateja wetu wakiibuka mamilionea kila siku na kila mwezi kupitia promosheni hii ya Airtel Yatosha.

Tunaahidi kuendelea kuwazawadia wateja wetu huku tukiboresha huduma zetu , na kuwapata wateja wetu huduma bora zenye gharama nafuu kupitia huduma yetu poa ya Airtel Yatosha inayomuwezesha mteja kuwasiliana na mitandao mengine ya simu za mkononi kwa bei poa na kupata vifurushi
vya maongezi bila kulipia gharama ya ziada". Aliongeza Mmbando.

Promosheni ya Airtel Yatosha bado inaendelea na wateja wetu wa Airtel Yatosha bado wananafasi ya kuendelea kujishindia pesa taslim na Nyumba  mbili za kifahari zilizopo Kigamboni  bado kushindaniwa.

Droo itakayomchagua mshindi wa nyumba kwa mwezi huu inatarajiwa kuchezeshwa tarehe 5/9/2013 saa tano asubuhi. hii itachagua mshindi mmoja kati ya wateja wote waliotumia huduma ya Airtel yatosha kwa
mwezi huu.

Ili mteja wa Airtel aweze kushiriki  anatakiwa kujiunga na vifurushi vya Airtel Yatosha kwa kupiga *149*99# na kujiunga na vivurushi vya Airtel Yatosha. Kila unapojiunga na kifurushi unaingia moja kwa moja
kwenye droo ya kushinda.

GRAND MALT YAMWAGA VIFAA LIGI KUU ZANZIBAR

 Mwakilishi wa timu ya KMKM ya unguja  Said Mfaume akipokea jezi toka kwa Waziri wa habari,utalii na michezo Zanzibar Said Mbarouk tayari kabisa kwa kuanza kwa ligi kuu ya Grandmalt Zanzibar,Kulia ni meneja masoko wa GrandMalt Fimbo buttala na Rais wa ZFA Ravia Faina
 Mwakilishi wa timu ya Mafunzo  ya pemba  Khamis Ally akipokea jezi toka kwa Waziri wa habari,utalii na michezo Zanzibar Said Mbarouk tayari kabisa kwa kuanza kwa ligi kuu ya Grandmalt Zanzibar,Kulia ni meneja masoko wa GrandMalt Fimbo buttala na Rais wa ZFA Ravia Faina
 Mwakilishi wa timu ya jamhuri  ya pemba  Abdallah Abeid  akipokea jezi toka kwa Waziri wa habari,utalii na michezo Zanzibar Said Mbarouk tayari kabisa kwa kuanza kwa ligi kuu ya Grandmalt Zanzibar,Kulia ni meneja masoko wa GrandMalt Fimbo buttala na Rais wa ZFA Ravia Faina.
KINYWAJI kisicho na kilevi cha Grand Malt, walio wadhamini wa Ligi Kuu ya Zanzibar maarufu kama ‘Grand Malt Premier League’ jana walikabidhi rasmi vifaa kwa timu 12 zinazoshiriki ligi hiyo katika hafla iliyofanyika hoteli ya Bwawani, mjini hapa.
 
Mbali na kumwaga vifaa hivyo, Grand Malt pia wameamua kufanya kweli zaidi kwa kuongeza udhamini wao kwa waamuzi na uendeshaji wa ligi, ambapo msimu huu watatoa kiasi cha Sh milioni 200 kutoka Sh milioni 140 za msimu uliopita.
 
Hafla hiyo maalumu ya kukabidhi vifaa na kutangaza kiasi hicho kipya cha uendeshaji wa ligi,  ilihudhuriwa na viongozi na wanamichezo mbalimbali wakiongozwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Saidi Ali Mbarouk.
 
Akizungumza katika hafla hiyo, Mbarouk alisema wamefurahishwa mno na Grand Malt kwa kuongeza udhamini wao pamoja na kutoa vifaa bora vya michezo kwa timu zote zishiriki.
 
“Tuna uhakika sasa soka ndani ya Zanzibar itazidi kusonga mbele, ombi lenu kwenu ZFA (Chama cha Soka Zanzibar), pamoja na wadau wote kutumia fursa hii kuhakikisha tunafika kule tunakokutaka.
 
“Nawasifu zaidi Grand Malt kwa kuendelea kudhamini Ligi Kuu ya Zanzibar nah ii inadhihirisha tuko nao pamoja kwa mambo mengi, nasi pia tunapaswa kuwaunga mkono kwa kutumia kinywaji chao,” alisema.
 
Mkurugenzi wa Masoko wa Grand Malt, Kushillah Thomas naye alisema, kinywaji hicho kitaendelea kushirikiana na watu wa Zanzibar katika kuhakikisha wanafanikiwa kwenye malengo yao.
 
“Udhamini huu ni mwanzo tu na tunaamini utasaidia kwa kiwango kikubwa kufanikisha malengo ya soka ya Zanzibar,” alisema.
 
Viongozi wa ZFA nao walikiri kufurahishwa na udhamini huo na kusema, wanaamini Ligi Kuu ya Grand Malt msimu huu itakuwa na ushindani mkubwa zaidi.
 
KMKM ndio waliofanikiwa kutwaa ubingwa huo msimu uliopita, wakiwa ni mabingwa wa kwanza toka kuanza kwa udhamini wa Grand Malt.
 
Mbali na KMKM timu nyingine zinazoshiriki ligi hiyo ni Fuoni, Chuoni, Polisi, Malindi (Bandari), Zimamoto, Mafunzo, Jamhuri, Chipukizi, Kizimbani, Mtende na Miembeni.
 
Kinywaji cha Grand Malt kisicho na kilevi ndio walioingia mkataba wa kudhamini ligi hiyo, hivyo kujulikana kama Ligi Kuu ya Grand Malt.

No comments:

Post a Comment