Sunday 11 January 2015

MBUNGE WA MBEYA MJINI, JOSEPH MBILINYI ‘SUGU’ APATA AJALI YA GARI MLIMA KITONGA

Sugu Mbeya
Mheshimiwa Joseph Mbilinyi akiwa amesimama mbele ya gari alilopata nalo ajali

Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amenusurika katika ajali ya gari  ambayo imetokea jana mchana(Jan.10)   eneo la Mlima Kitonga, wilaya ya kilolo mkoani Iringa.
Chanzo cha ajali hiyo kinatajwa kuwa ni kufeli kwa break hali iliyopelekea gari hilo kuanguka kichwa chini miguu juu wakati mbunge huyo akitokea Mbeya kuelekea Mikimu mkoani Morogoro kwenye mkutano wa hadhara.
Katika gari hilo aina ya Totoya Land Cruiser ambalo lilikuwa likiendeshwa na mheshimiwa Sugu, lilikuwa limebeba   watu wanne ambao wote walisalimika na kutoka salama licha ya michubuko ya mkononi aliyoipata mbunge huyo wa Mbeya Mjini.
Sugu apata ajali
Gari la Mheshimiwa Sugu baada ya kupata ajali eneo la Mlima kitonga
sugu Mr.Sugu
muonekano wa gari la mheshimiwa Sugu mlima Kitonga mkoani Iringa
Sugu Mr 2
Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ akiwa amefungwa bandeji kwenye bega baada ya kunusurika katika ajali

No comments:

Post a Comment