Saturday 17 January 2015

HALI SI SHWARI MANISPAA YA BUKOBA,PAMBANA KAMANDA MWAIBAMBE,MAJAMBAZI WASIJITAWALE.

Huyu Dada anahishi nje ya nchi katuma ujumbe huu,Tukio hili limetokea saa saba ya usiku maeneo ya Kibeta usiku wa kuamkia tarehe 17-1-2015.JINA LA HUYU DADA NI JULIA  ANETH MBAKILAKI.Leo usiku kwanzia saa 7 hapo katika Kijiji cha Magoti. Wezi wa 3 wanaume waliluka ukuta nakuingia kwa Mrs Zeulia Rweikiza wakavunja mlango wa nyumba ya uani na kumvamia binti yake Peace Rweikiza wakampiga kweli wakataka kumkata na panga, wakidai funguo za gari na kadi yake. Akawaambia gari iliisha haribika ni nzee iko stoa, alipokataa wakampiga kweli. Wapi dola?Wakamvamia mtoto wake mjukuu wakampiga naye wakamwambia lala chini wakawavuluta chumba cha pili kwa bibi mzee Ma Kostansia, wakasema tupe pesa na simu. Mkae hapa mama yuko wapi msipige kelele.

Wakati wote huo Peace akipiga kelele MSAADA waåpi, basi wakaendelea kupiga mlango nyumba kubwa nakutaka kuufungua ukakataa nyumba alalako Mrs Zeulia. Hapo ndipo Mrs Zeulia alisikia nakuogopa akakimbilia kufungua mlango wa mbele nakukimbilia mbele akiomba, mzaada akipiga mayowe kwa nguvu. Walimpomsikia walikuja kasi nakumkuta akikalibia karibu na barabara, wakampiga ngwala wakampiga saana, akaambiwa urudi utupe dora au pesa, akawaaambia pesa sina wakaendelea kumpiga akaanguta tena wakambuluza toka barabarani mpaka ndani wakamwambia utupe pesa, simu iko wapi akawapa,wakampiga tena wakaingilia masunduku wakavuruga kweli wakaanza kupakia mafuta, sabuni baadhi ya vitu dawa,nk mwisho wakapata pesa zake alikozificha wakazichukua wakamwacha hoi. Hakuna jirani,hakuna polisi nawalipofika polisi wanae wakiume wakaambiwa waje wenyewe wala hawakwenda kuona jinsi ali ilivyo. Baadaye walirudi nakuwapeleka polisi na hospitali.

Jamani mbona hakuna usalama nchi yetu hata ushirikiano wapi watu wameogopa kweli baada ya mauwaji yaliyotokea Bukoba mwisho wa mwaka jana?
Vipi waandishi wa habari hebu toeni historia kama hii kamili ili watu waone hali inapoelekea. Mrs Zeulia kaumizwa kweli kalazwa hospitali Bukoba GVT hospital.Mwende mkamwone atawapa maelezo
Mimi ni mwanae Victoria Rweikiza nilikuwa Bukoba mwezi wa desemba wakati mauaji yalipokuwa yanaendelea inaogopesha kweli.

1 comment:

  1. Hapo ni kununua upinde na mishale ya sumu unakuwanayo ndani ukiwasikia tu unadungua mmoja mmoja lakini ukitegemea majirani na polisi utakutananao jehanamu mi mwenyewe walinibomolea,apo watu waliosikia walikuja jamaa wakakimbia na kulikuwa hakuna mtu ndani ila baada ya tukio hilo niko fiti kujilinda

    ReplyDelete