Friday 10 October 2014

BREAKING NEWS!!! MWALIMU WA SEKONDARI KAGEMU AMEUWA KWA MAPANGA KANISANI

Ili ndio eneo halisi ndani ya kanisa walipokatiwa mapanga watu hao.


Taarifa ya awali alizotoa mchungaji wa kanisa hilo ambaye amejitambulisha kwa jina moja la  FAUSTINE JOSEPH, amesema kuwa usiku saa 5, yeye alimaliza ibaada yao, ambapo mwalimu alisema kuwa hawezi kwenda nyumbani kwasababu anatokea mbali, hivyo akaamua kupumzika Kanisani na mwenzake ambaye jina lake halijafaamika aliyekatwa mguu, ndipo usiku wakavamiwa na kuawa Mwl huyo aliyekuwa anafundisha Kagemu sekondari, na aliyekuwa naye kukatwa mguu ambaye ni Temistocres.
Mchungaji  FAUSTINE JOSEPH
Mchungaji CREODWARD EDWARD, ambaye ni mwenyekiti wa makanisa ya Kipentekoste amesema wanakaa kikao na wacvhungaji wote wa makanisa ya kikristo kutoa tamko kwasababu matukio ya namna hii yamekuwa yakitokea katika makanisa yao yasiyo yakawaida na yanawasikitisha sana.
Mchungaji CREODWARD EDWARD
Polisi wamefika katika eneo hilo na kuondoka na mwili wa marehemu  pamoja na majeruhi, kwajili ya kumpeleka hospitali, na inaelezwa kuwa amelazwa katika hospitali ya mkoa ambapo wachungaji wanakuta saa5 leo kutoa tamko.

No comments:

Post a Comment