Sunday 8 November 2015

NI MWAKA MMOJA TANGU KAPTEN JOHN BARONGO AFARIKI NA MIAKA 10 TANGU MA WINFRIDA BARONGO AFARIKI,FAMILIA WAWEKA MISA.

Ni familia ya marehemu John Barongo wa Kanazi Bukoba vijijini katika picha ya pamoja baada ya ibada ya misa takatifu ya kuwakumbuka wazazi wao,mwaka mmoja wa kumaliza matanga ya marehemu baba yao Kapten John Barongo na miaka kumi tangu mama yao Ma Winfrida Barongo afariki,misa ilifanyika nyumbani kwa marehemu Kanazi Bukoba,katika uhahi wa marehemu Barongo amekuwa kiongozi serikalini na katika chama cha mapinduzi katika nafasi za juu.
Kaburi la Kapten John Barongo.
Kaburi la Ma Winfrida Barongo.
Mzee Pius Ngeze, mmoja wa wazee waliofanya kazi na marehemu akisalimiana na wanafamilia.
Mc Rutakwa akitoa maelekezo na mpangilio wa shughuli nzima.
Mzee Rutaraka rafiki mkubwa wa familia, akieleza namna walivyoishi na marehemu Barongo katika maisha yao ya harakati za kisiasa.
Baba mdogo akitoa nasaha kwa wanafamilia na wageni waalikwa.
Mtoto mkubwa wa kiume Gordwin Barongo akitoa neno la shukrani kwa wote waliofika kwa niaba ya familia.
Dada mkubwa wa familia akitoa neno na kuwashukuru wadogo zake namna wanavyomuheshimu na kupendana.
Kwaya ya BCC wakitumbuiza.
Joanitha Barongo akicheza na wanakwaya.
Lilian Barongo akiwa katika maeneo ya makaburi ya wazazi wake.
Gordwin Barongo akiwa maeneo ya makaburi.
Picha ya marehemu Barongo.
Wakati wa ibada.
Mkate wa bwana.
Pumzikeni kwa amani wazazi wetu.

No comments:

Post a Comment